Navigation Menu



Swala ya kuomba mvua swalat istiqaa na jinsi ya kuiswali.

Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali.

12. Swala ya Kuomba Mvua - (Swalatul Istisqaa)’

Istisqaa ina maana ya kuomba maji. Uislamu unatuhimiza kumuelekea Allah kwa msaada wakati wa matatizo na dhiki. Kwa hiyo panapokuwa na ukame Waislamu wanahimizwa kumuomba Allah(s.w)kwa unyenyekevu katika jamaa. Maombi haya yanajulikana kama “Swalatul Istisqaa”. Kutokana na Hadithi mbali mbali maombi haya yanaweza kuombwa katika namna tatu zifuatazo:

 


(a)Kuomba Dua bila ya swala.
(b)Kuomba dua katika khutuba ya Ijumaa au mwisho wa swala za faradhi.
(c)Namna ya tatu ambayo ni muhimu sana ni ile ya kuswali rakaa mbili zinazofuatiwa na khutuba na kumalizia na Dua.
Maombi haya hapana budi yaombwe kwa unyenyekevu mkubwa ukiambatana na imani kamili juu ya uwezo waAllah usio mipaka.

 


Swalatul Istisqaa Inavyoswaliwa

 


Swala hii ni sunnah iliyokokotezwa wakati wa ukame na huswaliwa katika jamaa uwanjani kama inavyo swaliwa swala ya Idd. Kama swala ya Idd katika rakaa ya kwanza kuna takbira saba baada ya Takbira ya kuhirimia na kuna Takbira tano kabla ya kuanza Suratul Fatiha katika rakaa ya pili. Ni sunnah katika rakaa ya kwanza, baada ya Al-fatiha kusoma Surat-Qaf au Al-A’laa na katika rakaa ya pili kusoma baada ya Alfatiha. suratul-Qamar au Al-Ghashiyah. Imamu ni sharti awe kiongozi wa ngazi ya juu au naibu wake anayeshughulikia mambo ya Waislamu.

 


Swala hii hufuatiwa na khutuba mbili kama ilivyo katika khutuba za Idd. Ni sunnah Imamu kuleta istighf'aari mara tisa kabla hajaanza khutuba ya kwanza na ya pill.

 

Istighfaari hii ni kusema
"Astaghafirullahil-aladhim alladhii laa ilaaha illa huwal-hayyul-qayyuum-almudabbiru kullu-shayin wa-atubu ilaihi"

 

Ni sunnah wakati wa kuomba dua kugeuza mikono au kuelekeza mbinguni migongo ya viganja vya mikono . Tunafahamishwa hill katika Hadith za Mtume (s.a.w) zifuatazo kuwa:
Abduilah blrs 7.aid Al-Arrsarl (r.a) amesimuiia kuwa Mtume (s.aw) aWaaenda rye ya rryi Qi Iwswali swaIatu1-IsiisgaaAUpotaka. kuorrtba dua, alielekea Qibia nra alaageura. kiiemba choke. (Muslim).
Arras bin MaWc (r.a) amestmuIia kuu~a Mturne (s.a w) katika kuomba dua ya mvua alielekaezaJuu mtgongo yaviganfa uyake vya miknno. (Muslim).

 

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1170


Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zifazofanana:-

Watu wanaolazimika kufunga mwezi wa Ramadhani
Hapa utajifunza watu ambao wanalazimika kufunga mwezi wa Ramadhani. Soma Zaidi...

Nguzo za kufunga ramadhani
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga. Soma Zaidi...

Adhabu ya mzinifu katika jamii ya kiislamu
(iii) Adhabu ya UzinifuKatika Sheria ya Kiislamu mtu haadhibiwi mpaka atende kwa uwazi matendo yenye kuvuruga utaratibu na amani ya jamii. Soma Zaidi...

Wanaorithi katika wanaume na wanawake na kiwango wanachorithi
Soma Zaidi...

Hekma katika hukumu za mirathi katika uislamu, na ni kwa nini wanaume wanazidi katika kurithi katika uislamu
Soma Zaidi...

Jinsi ya kufanya suluhu kati ya mume na mke.
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa. Soma Zaidi...

Uislamu unakataza mtu kulaani hovyo
20. Soma Zaidi...

Jinsi ambavyo mtu anazuiliwa kurithi mali ya marehemu
Endapo mtu yupp katika orodha ya wanaotakiwa kutithi, anaweza kuzuiliwa kurithi kwa kuzingatia haya. Soma Zaidi...

Kukaa itiqaf na sheria zake hasa katika mwezi wa ramadhani
Soma Zaidi...