picha

Swala ya kuomba mvua swalat istiqaa na jinsi ya kuiswali.

Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali.

12. Swala ya Kuomba Mvua - (Swalatul Istisqaa)’

Istisqaa ina maana ya kuomba maji. Uislamu unatuhimiza kumuelekea Allah kwa msaada wakati wa matatizo na dhiki. Kwa hiyo panapokuwa na ukame Waislamu wanahimizwa kumuomba Allah(s.w)kwa unyenyekevu katika jamaa. Maombi haya yanajulikana kama “Swalatul Istisqaa”. Kutokana na Hadithi mbali mbali maombi haya yanaweza kuombwa katika namna tatu zifuatazo:

 


(a)Kuomba Dua bila ya swala.
(b)Kuomba dua katika khutuba ya Ijumaa au mwisho wa swala za faradhi.
(c)Namna ya tatu ambayo ni muhimu sana ni ile ya kuswali rakaa mbili zinazofuatiwa na khutuba na kumalizia na Dua.
Maombi haya hapana budi yaombwe kwa unyenyekevu mkubwa ukiambatana na imani kamili juu ya uwezo waAllah usio mipaka.

 


Swalatul Istisqaa Inavyoswaliwa

 


Swala hii ni sunnah iliyokokotezwa wakati wa ukame na huswaliwa katika jamaa uwanjani kama inavyo swaliwa swala ya Idd. Kama swala ya Idd katika rakaa ya kwanza kuna takbira saba baada ya Takbira ya kuhirimia na kuna Takbira tano kabla ya kuanza Suratul Fatiha katika rakaa ya pili. Ni sunnah katika rakaa ya kwanza, baada ya Al-fatiha kusoma Surat-Qaf au Al-A’laa na katika rakaa ya pili kusoma baada ya Alfatiha. suratul-Qamar au Al-Ghashiyah. Imamu ni sharti awe kiongozi wa ngazi ya juu au naibu wake anayeshughulikia mambo ya Waislamu.

 


Swala hii hufuatiwa na khutuba mbili kama ilivyo katika khutuba za Idd. Ni sunnah Imamu kuleta istighf'aari mara tisa kabla hajaanza khutuba ya kwanza na ya pill.

 

Istighfaari hii ni kusema
"Astaghafirullahil-aladhim alladhii laa ilaaha illa huwal-hayyul-qayyuum-almudabbiru kullu-shayin wa-atubu ilaihi"

 

Ni sunnah wakati wa kuomba dua kugeuza mikono au kuelekeza mbinguni migongo ya viganja vya mikono . Tunafahamishwa hill katika Hadith za Mtume (s.a.w) zifuatazo kuwa:
Abduilah blrs 7.aid Al-Arrsarl (r.a) amesimuiia kuwa Mtume (s.aw) aWaaenda rye ya rryi Qi Iwswali swaIatu1-IsiisgaaAUpotaka. kuorrtba dua, alielekea Qibia nra alaageura. kiiemba choke. (Muslim).
Arras bin MaWc (r.a) amestmuIia kuu~a Mturne (s.a w) katika kuomba dua ya mvua alielekaezaJuu mtgongo yaviganfa uyake vya miknno. (Muslim).

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/08/15/Monday - 11:18:23 am Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2090

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 web hosting    👉6 ai web app   

Post zinazofanana:

Maana ya Mirathi na kurithi katika uislamu

Maana ya MirathiMirathi katika Uislamu ni kanuni na taratibu alizoziweka Allah (Sw) katika kuwagawawia na kuwarithisha familia na jamaa, mali aliyoiacha marehemu.

Soma Zaidi...
Maandalizi kwa ajili ya kifo

Mwanadamu anatakiwa aishi huku akikumbuka kuwa ipo siki atakufa. Hivyo basi inatupata lujiandaa mapema kwa ajili ya kifo.

Soma Zaidi...
Yaliyo haramu kwa mwenye hadathi kubwa.

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ya haramu kwa mwenye hadathi kubwa

Soma Zaidi...
Taratibu za kufanya kazi na kuajiri katika uislamu

Post hii itakufundisha taratibu za kuajiri, kufanya kazi na malipo.

Soma Zaidi...
Nguzo za swaumu (kufinga)

Hapa utajifunza nguzo kuu za swaumu. Kama hazitatimia nguzo hizi basi swaumu itakuwa ni batili.

Soma Zaidi...
Ni zipi najisi katika uislamu

Post hii inakwenda kukupa orodha ya vitu vilivyo najisi.

Soma Zaidi...