picha

NAMNA YA KUSWALI: NIA YA SWWALA, NA KUPIGA TAKBIRA (yaani kusema Allah akbar)

Mtume (s.

NAMNA YA KUSWALI: NIA YA SWWALA, NA KUPIGA TAKBIRA (yaani kusema Allah akbar)

Mtume (s.a.w) ametuagiza katika Hadith maarufu kuwa tuswali kama alivyokuwa akiswali. Hivyo katika sehemu hii tutajitahidi kuonesha utekelezaji wa swala hatua kwa hatua kwa kurejea Hadith Sahihi za Mtume (s.a.w):

1. Nia na Takbira ya kuhirimia
Nia ni kudhamiria moyoni kuwa unaswali, swala unayoikusudia kisha unaanza swala kwa kusema: “Allaahu Akbar” Allah ni Mkubwa kwa kila hali”. Wakati wa kuhirimia swala ni sunnah kuinua viganja vya mikono,mkabala na mabega. Kuhusu unyanyuaji wa mikono mkabala na mabega imeripotiwa kuwa Mtume (s.a.w) alikuwa akifanya hivyo katika sehemu nne tofauti:
1. Wakati wa kuhirimia swala (kuanza swala).
2. Wakati anaposema Allaahu Akbar kwa ajili ya rukui.
3. Wakati anaposimama kutoka kwenye rukuu.
4. Wakati anaposimama kutoka kwenye tahiyyatu ya kwanza ili kuendelea na rakaa ya tatu.

Hii tunaipata katika Hadith aliyosimulia Abdullah bin ‘Umar kuwa: “Mtume (s.a.w) aliposimama kwa ajili ya swala alinyanyua mikono yake mkabala na mabega yake na kisha kuhirimia (kusema Allahu Akbar). Alipotaka kurukuu alinyanyua mikono kama alivyofanya kwanza na aliposimama kwa ajili ya itidali alifanya hivyo hivyo na alisema Allah anamsikia yule anayemsifu. (Bukhari, Muslim na Bayhaqi). Nafa’a(r.a) ameeleza kwamba Ibn ‘Umar (Abdullah)(r.a) aliposimama kwa ajili ya rakaa ya tatu alikuwa akinyanyua mikono; jambo ambalo alilihusisha na Mtume (s.a.w). (Bukhari, Abu Dawud, Nasai).

Baada ya kuhirimia swala mwenye kuswali hushusha mikono yake na kuiweka kifuani, mkono wa kulia ukiwa juu ya mkono wa kushoto kwa mujibu wa Hadith zifuatazo: Hulab At-Tai(r.a) amesimulia: “Nilimuona Mtume (s.a.w) akiswali hali ameweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wa kushoto juu ya kifua chake.” (Ahmad na At-Tirmidh)

Naye Wail bin Hijr (r.a) ameripoti: “Niliswali pamoja na Mtume (s.a.w) na aliweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wa kushoto juu ya kifua chake”. (Ahmad na At-Tirmidh).

Imamu Abu Dawud na Nasai wamepokea kutoka kwa Ibn Khuzaimah kuwa Mtume (s.a.w) alipokuwa akiswali alikuwa akiweka mkono wake wa kulia juu ya kiwiko (wrist) cha mkono wa kushoto na sehemu ya mkono inayofuatia kiganja .


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Jiunge nasi WhatsApp
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2228

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Kwanini wengi wanaoswali hawafikii lengo la swala zao

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Hija ya Kuaga na Kutawafu kwa Mtume (s.a.w)

Hija ya Kuaga na Kutawafu kwa Mtume (s.

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya zakat na sadaqat

Nguzo za Imani, tofauti kati ya sadaqat na zakat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo mtu anazuiliwa kurithi mali ya marehemu

Endapo mtu yupp katika orodha ya wanaotakiwa kutithi, anaweza kuzuiliwa kurithi kwa kuzingatia haya.

Soma Zaidi...
Swala ya kuomba mvua swalat istiqaa na jinsi ya kuiswali.

Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali.

Soma Zaidi...