Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi?
Malezi ya Mtoto Mchanga baada ya Talaka
Mtoto mchanga hataachanishwa na mama yake mpaka awe na umri wa miaka miwili - umri wa kuacha kunyonya. Matumizi ya mama na mtoto katika kipindi hiki cha kunyonya mtoto yatakuwa juu ya mume japo mkewe aliyemtaliki atakuwa kwa wazazi wake au penginepo nje ya nyumbani kwake. Lakini mume na mke walioachana, wakiridhiana wanaweza kumwachisha kunyonya kabla ya miaka miwili au wanaweza kumkodisha mwanamke mwingine amnyonyeshe. Hukumu hii ya malezi ya mtoto baada ya mume na mke kuachana inabainishwa vyema katika Qur-an:
Na wanawake waliozaa wawanyonyeshe watoto wao miaka miwili kamili; kwa anayetaka kukamilisha kunyonyesha; na ni juu ya baba (yake) chakula chao (hao watoto na mama) na nguo zao kwa sheria. Wala haikalflshwi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya wasaa wake. Mama asitiwe taabuni kwa ajili ya mtoto wake, wala baba (asitiwe taabuni kwa ajili ya mtoto wake).
Na kama wote wawili wakitaka kumwachisha ziwa (kabla ya miaka miwili), kwa kuridhiana na kushauriana, basi sio kosa juu yao. Na kama mkitaka kuwapatia watoto wenu mama wa kuwanyonyesha (wengine wasiokuwa mama zao) basi haitakuwa dhambi juu yenu kama mkitoa (kuwapa hao wanyonyeshaji) mlichowaahidi kwa sharia. Na mcheni Mwenyezi Mungu na jueni kwamba Mwenyezi Mungu anayaona yote mnayoyatenda. (2:233)
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katikabuislamu dhana ya uchumi imetofautiana na dhana ya kidunia hivi leo ambapo kamari na riba ni moja ya vitu muhimu katika uchumi.
Soma Zaidi...Haya ni mamno muhimu yanayozingatiwa kabla ya kuanza zoezi la kugawa mirathi ya marehemu.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha njia zinazotumika kujitwaharisha.
Soma Zaidi...Ili swala itimie utahitajika kutimiza nguzo zake na masharti yake. Hapa utajifunza nguzo 17 za swala.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ya haramu kwa mwenye hadathi kubwa
Soma Zaidi...Hspa utajifunza sasa jinsi ya kugawa mirathi kutokana na viwango maalumu.
Soma Zaidi...