TARATIBU ZA KUCHAGUWA MCHUMBA KATIKA UISLAMU


image


Hapa utajifunza hatuwa kwa hatuwa za kuchaguwa mchumba kulingana na sheria za kiislamu.


Kuchagua Mchumba

Jambo Ia kwanza katika kuendea taratibu za kukamilisha ndoa ya Kiislamu ni kuchagua mchumba. Katika kuchagua mchumba, Mtume (s.a.w) anatunasihi katika hadithi ifuatayo:

 


Abu Hurairah amesimulia kuwa: Mtume (s.a.w) amesema: 'Mwanamke anaolewa kwa vitu vine: kwa utajiri wake, hadhi yake, uzuri wake wa sura na kwa dini yake (Uchaji-Mungu wake). Mchague yule mwenye msimamo mzuri wa dini " (Bukhari na Muslimu)

 


Hadithi hii inatufahamisha kuwa vitu vinavyoweza kuwa vichocheo vya mtu kumchagua mchumba ni hivyo vinne vilivyotajwa, lakini Mtume (s.a.w) anatusisitizia tukifanye kichocheo cha dini kiwe namba moja kisha ndio vifuatie hivyo vingine. Ukweli ni kwamba mke mcha-Mungu atatii amri za AIIah(sw) na Mtume wake ambazo zitampelekea kumtii na kumheshimu mumewe. Halikadhalika, mume mcha-Mungu, atamtii Allah (s.w) na huchunga mipaka aliyomuwekea, jambo litakalompelekea kumhurumia mkewe na kumtendea haki inavyostahiki. Hivyo, maisha ya wacha-Mungu hawa katika familia yatakuwa ni yale ya kuhurumiana, kusaidiana na kushirikiana katika kuilea na kuiendeleza familia katika misingi ya ucha-Mungu.

 


Pia katika suala Ia kuchagua mchumba mtume (s.a.w) anazidi kutuasa katika hadithi ifuatayo:
Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema "Utakapochumbiwa na mwanamume unayempenda kwa dini (ucha-Mungu wake) basi kubali uolewe naye. Kama hutafanya hivyo patakuwa na huzuni na vurugu katika ulimwengu.

 

Msisitizo wa kuwaoa wanawake wacha-Mungu au kuolewa na wanaume wacha-Mungu uko bayana katika Qur-an kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:

 

Wala msiwaoe wanawake makafiri mpaka waamini. Na mjakazi mwenye kuamini ni bora kuliko muungwana kafiri, hata ingawa kakupendezeni. Wala msiwaoze wanaume makafiri (wanawake Waislamu) mpaka waamini. Na mtumwa mwenye kuamini ni bora kuliko muungwana kafiri, hata akikupendezeni. Hao makafiri wanaitia kwenye moto. Na Mwenyezi Mungu anaitia kwenye Pepo na Samahani, kwa amri yake. Naye hueleza aya zake kwa watu iii wapate kukumbuka." (2:221)

 

Wanawake wabaya ni wa wanaume wabaya; na wanaume wabaya ni wa wanawake wabaya; na wanawake wema ni wa wanaume wema; na wanaume wema ni wa wanawake wema " (24:26)

 


Mwanamume mzinfu hafungamani ila na mwanamke mzinfu au mwanamke mshirikina; na mwanamke mzinfu hafungamani ila na mwanamume mzinfu au mwanamume mshirikina, na hayo yam eharamishwa kwa waislamu." (24:3)

 


Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa waislamu si tu wameharamishiwa kuwaoa au kuoelewa na makafiri na washirikina bali pia wameharamishiwa kuwaoa au kuolewa na watu wazinifu na waliozama katika maasi mengineyo hata kama watadai kuwa ni waislamu.La muhimu tunalopata hapa ni kuwa waumini wanatakiwa wawe makini katika kuchagua wachumba. Wazingatie wema na ucha-Mungu wa hao wanaowatarajia wawe wake au waume zao.

 


Na (mmehalalishiwa kuwaoa) wanawake wema wa Kiislamu na wanawake wema katika wale waliopewa kitabu kabla yenu, mtakapo wapa mahari yao na kufunga nao ndoa, bila ya kufanya uzinfu au kuwaweka vimada " (5:5)

 


Katika aya hii inatolewa ruhusa kwa wanaume wa Kiislamu kuwaoa wanawake wema wa ah-lal-kitaab ambao ni wanawake wema wa Kiyahudi na Kikristo kama inavyofafanuliwa katika Qur-an. Pametokea kutofautiana miongoni mwa wanazuoni wa Kiislamu juu ya ruhusa hii ya kuoa Ahlal-kitaab.

 


Kulingana na Sheikh Abdallah Saleh Alfarsy katika sherehe ya aya hii (5:5) ameeleza kuwa Mkristo aliyeruhusiwa kuoelewa na Muislamu ni yule tu ambaye ukoo wake umeingia katika dini hiyo kabla ya Uislamu haujaja.Amezidi kusisitiza Sheikh "Ama hawa wanaoitwa Misheni wanaoingia katika Ukristo sasa Si halali kuwaoa. ni haram wala ndoa haisihi".

 


Kulingana na maoni ya lbn Abbas (r.a), Muislamu anaweza kumuoa mwanamke wa Ahlal-Kitaabi aliye katika himaya ya Dola ya Kiislamu tu, na haruhusiwi kumuoa mwanamke wa Ahlal-Kitaabi ambaye yuko katika dola ambazo ni maadui wa Dola ya Kiislamu au yuko katika dola za Kikafiri. Tofauti na maoni haya ya lbn Abbas, Said bin Masayyab na Hassan Basri wanasema kuwa ruhusa hii ya kuwaoa wanawake wema wa Ahial-Kitabi imetolewa kwa ujumla.

 


leleweke kuwa kuwaoa Ahlal-Kitaabi si amri bali ni ruhusa kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w) kama ruhusa nyingine zilizotolewa katika Qur-an. Kuitumia ruhusa hii pasina haja na pasina kuzingatia malezi ya watoto katika misingi ya Uislamu ni hatari kubwa. Ikitokea mtu anaishi katika nchi ya Ahial-Kitabi na hana namna ya kumpata mwanamke mwema wa Kiislamu wa kumuoa, itakuwa kwake vyema kumuoa mwanamke mwema miongoni mwa hao Ahlal-Kitaabi badala ya kufanya uzinifu au kukaa na mwanamke bila ndoa. Ama pale ambapo kuna mabinti wema wa Kiislamu kuna haja gani ya kumuoa binti wa Kikristo? Jambo Ia msingi Ia kusisitiza hapa ni kwamba, aliyetoa ruhusa hii ni Mwenyezi Mungu (s.w), Mjuzi mwenye Hekima. Hivyo, kwa vyovyote vile kuna hekima kubwa katika ruhusa hii.

 


Ni haramu kwa wanawake wa Kiislamu kuoelewa na wanaume Wakristo au Mayahudi. Hivyo kwa mtazamo wa Kiislamu hapana ndoa kati ya mwanamume Mkristo au Myahudi na mwanamke Muislamu. Mtu atakayemwozesha binti yake kwa Mkristo, ajue wazi kuwa ameruhusu zinaa. Vile vile kwa waislamu ni haramu kushiriki katika sherehe za ndoa za namna hiyo kama ilivyo haramu kushiriki katika sherehe zote za kidini za Makafiri, Washirikina na Ahlal-Kitaabi. Kusherehekea pamoja nao, moja kwa moja, ni kuwaunga mkono katika hayo wanayosherehekea kinyume na Mwenyezi Mungu (s.w).

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    2 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    3 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    5 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    6 Magonjwa na afya    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Sifa nyingine za kuchaguwa mchumba ambazo watu wengi hawazijui
Hizi ni sifa za ziada za mchumba katika uislamu. Sifa hizi wengi hawazijui ama hawazingatii. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa
Post hii itakufundisha taratibu za kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa. Soma Zaidi...

image Umuhimu wa swala yaani kuswali kwa mwanadamu
Kwa nini ni muhimu kuswali? Post hii itakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kusimamisha swala. Soma Zaidi...

image Namna ya kurithisgha hatuwa kwa hatuwa.
Hspa utajifunza sasa jinsi ya kugawa mirathi kutokana na viwango maalumu. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kushona sanda ya maiti na kumvisha yaani kumkafini
Hapa utajifunza taratibu za kumkafini maiti wa kiislamu. Yaani kushona sanda yake na kumvisha. Soma Zaidi...

image Haki ya kumiliki mali na mipaka yake katika uislamu
Je unaijuwa mipaka yako katika kumiliki mali. Ama unajuwa haki zako katika mali inayomiliki. Endelea na somo Soma Zaidi...

image Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu
Uislamu umeweka taratibu maalumu za kuzifata katika kusherehekea siku ya idi. Soma Zaidi...

image Mifumo ya benki na kazi zake
Hapa utajifunza kazi za benki. Soma Zaidi...

image Namna ya kuswali hatuwa kwa hatuwq
Post hii itakufundisha jinsi ya kuswali hatuwa kwa hatuwa. Soma Zaidi...

image Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kukaa eda kwa mwanamke ambaye amefiwa na mume. Soma Zaidi...