Taratibu za mahari katika uislamu

Taratibu za mahari katika uislamu

Hapa utajifunza taratibu za kutaja mahari katika uislamu.

Mahari

Kabla ya mkataba wa ndoa kupitishwa jambo muhimu ni mwanamke kutaja kiasi cha mahari atakacho penda kupokea kama hidaya au zawadi anayopewa kwa amri ya Mwenyezi Mungu (s.w) kutoka kwa anayemuoa. Uhuru wa kutamka kiasi cha mahari uko kwa muolewaji na bila ya mahari hayo kutolewa taslimu au kwa ahadi ya kulipa baadaye, ndoa haiswihi. Msititizo wa mahari unapatikana katika aya zifuatazo:

 

Na wapeni wanawake mahari yao, hali ya kuwa ni hidaya (aliyowapa Mwenyezi Mungu). (Lakini hao wake zenu) wakikupeni kwa radhi ya nafsi zao kitu katika hayo (mahari) basi kuleni kwafuraha na kunufaika. (4:4).

 

"...Na (mmehalalishiwa kuwaoa) wanawake wema wa Kiislamu na wanawake wema katika wale waliopewa Kitabu kabla yen u,mtakapowapa mahari yao, kafunga nao ndoa..." (5:5)

 


Katika aya hizi tunajifunza kuwa kutoa mahari kuwapa wanawake tunaowaoa ni jambo Ia lazima aliloliamrisha Mwenyezi Mungu (s.w), lakini wenye kuolewa kwa hiari yao wenyewe, wakiamua kuyasamehe mahari hayo au kuyapunguza hata baada ya kutaja, hapana ubaya wowote bali ni jambo zuri pia Ienye kuzidisha mapenzi baina ya mume na mke. Pia mume anaweza kukopeshwa mahari na mkewe akaja kumlipa baadaye.

 


Lakini kulingana na hadithi ya Mtume (s.a.w) mtu akimlaghai mwanamke kuwa atamlipa mahari hapo baadaye iii akubali wafunge naye ndoa na huku ana nia ya kutomlipa, basi hiyo ndoa haitosihi na huyo mwanamume atahesabiwa kuwa anakaa kimada na huyo mwanamke mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w). Mahari ndiyo inayomuhalalishia mume tendo Ia ndoa kwa mkewe kama tunavyojifunza katika hadithi:

 


Uqbah bin Amir (r. a) ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w) amesema: Jambo ?a msingi katika ndoa ni kwamba utimize kwanza kutoa idle kilichofanya sehemu za sin (za mwanamke) kuwa halali (kwako). (Bukhari Muslim).

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views: 4867

Share On:

Share follows: 1 | Unique share links followed: 1
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Namna ya kutawadha yaani kuchukuwa udhu

Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu.

Soma Zaidi...
Aina za Najisi na twahara katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha aina za najis. Pia utajifunza aina za twahara katika uislamu

Soma Zaidi...
Haki za kiuchumi za mwanamke katika uislamu

Haki za UchumiKuwa imara kiuchumi ni sababu mojawapo kubwa ya kumpa mtu hadhi katika jamii.

Soma Zaidi...
Mambo yanayopunguza malipo ya funga au swaumu

Mambo haya yanaweza kuharibu funga ya mtu ama kupunguza malipo ya funga.

Soma Zaidi...