image

Tatizo la mapafu kuwa na usaha.

Post hii inahusu Zaidi tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,ni tatizo ambalo usababishwa na bakteria ambao uingia kwenye mapafu na kusababisha madhara na hatimaye mapafu kuwa na usaha .

Tatizo la mapafu kuwa na usaha.

1. Hili ni tatizo ambalo utoke pale bakteria wanapotoka sehemu mbalimbali za ndani ya mwili au nje ya mwili na kuingia kwenye mfumo wa hewa hali ambayo usababisha mapafu kushambuliwa na hao bakteria na kuanza kutoa usaha, na Kwa hiyo tunafahamu kabisa kazi ya mapafu Huwa ni kumsaidia katika kupumua ila yakisha shambuliwa na Hawa bakteria usababisha upumuaji Kuwa wa shida.

 2. Kuna sababu ambazo huangaliwa kama ni chanzo Cha kusababisha kuwepo Kwa hali ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,ni pamoja na kucheua hasa Kwa watu wenye matatizo ya meno yaliyooza, hali hii utokea Kwa sababu kwenye meno yaliyooza Kuna bakteria ambao usababisha uozo kwenye meno,Kwa hiyo mtu anapotafuna chakula na bakteria hao uwepo na kuingia tumboni pale mtu anapocheua chakula Kuna wakati wale bakteria uweza kuingia kwenye mfumo wa hewa na kuanza mashambulizi kwenye mapafu.

 

 

 

3. Pamoja na kuwepo bakteria waliotokana na mtu mwenye tatizo la kuoza Kwa meno,na wakati mwingine Ile asidi kutoka kwenye tumbo Kwa watu wanaocheua uweza kuingia kwenye mfumo wa hewa na kuanza kushambulia mapafu hali ambayo usababisha mapafu kuwa na usaha iwapo matibabu kama hayatafanyika mapema Kwa mgonjwa. Pia Kuna wakati mwingine mtu akipaliwa  na bakteria wakaingia kwenye mfumo wa hewa usababisha mapafu kuwa na usaha.

  

 

 

4. Tunapaswa kufahamu kwamba kwenye Kila sehemu ya mwili kunapaswa kuwepo Kwa bakteria wake wazuri tu ambao hawana madhara Kwa mtu, ila wakihama kutoka kwenye sehemu moja ya mwili na kwenda nyingine huweza kuleta matatizo na kusababisha hali isiyotarajiwa,Kwa hiyo bakteria wakitoka kwenye tumbo na kuingia kwenye mfumo wa hewa uleta maafa au kutoka mdomoni kuingia kwenye mfumo wa hewa uleta shida,Kwa hiyo kitendo Cha bakteria kutoka ndani au nje na kuingia kwenye mfumo wa hewa usababisha kuoza Kwa mapafu na kuleta usaha.

 

 

 

 

5. Pamoja na kuwepo Kwa bakteria kwenye mfumo wa hewa Kuna na Sababu nyingine ambazo ni pamoja na kuwepo Kwa Kansas ya mapafu,ambapo kwenye mapafu uzalishwa seli zisizo za kawaida Kwa kitaalamu huitwa abnormal sell,seli hizi zikixalushwa usababisha kuishiwa au kupungua Kwa seli za kawaida ambazo ufanya kazi kwenye mapafu na kusababisha mapafu kuoza na kuanza kutoa usaha na kushindwa kufanya kufanya kazi yake ya kawaida,hali hii ya Kansa ya mapafu inabidi kutambuliwa mapema lli kuanza matibabu Kwa sababu madhara yake Huwa ni makubwa isipotibiwa mapema.

 

 

 

6. Vile vile kuwepo Kwa uchafu au material mengine kwenye mfumo wa hewa ambayo usababishwa na vitu mbalimbali kama vile kuzalishwa Kwa tissue kwenye mfumo wa hewa au kemikali za sumu ambazo utokana mtido wa maisha wa mtu kama wale wanaovuta sigara Kwa mda mrefu ule Moshi uzalisha sumu ambao usababisha kuwepo Kwa sumu kwenye mfumo wa hewa na hivyo usababisha mapafu kuoza na utoa usaha.

 

 

 

 

7. Vile vile na wagonjwa wa kifua kikuu ambao hawatumii dawa usababisha kuwepo Kwa usaha kwenye mfumo wa hewa,tukumbuke kwamba, kifua kikuu hasa hasa usababishwa na bakteria ambao ushambulia mapafu na kusababisha matatizo kwenye mfumo wa hewa, Kwa hiyo kama mgonjwa ana tatizo hilo na pia akakosa kutumia dawa za kutibu kifua kikuu anaweza kusababisha bakteria kuendelea kushambulia mapafu na hatimaye mapafu kuoza na kutoa usaha.

 

 

 

 

8. Pia na mashambulizi ya virusi na fungasi kwenye mfumo wa hewa,Kuna wakati mwingine mfumo wa hewa haushambuliwa na bakteria peke yake pengine inawezekana wakawa virus na fungasi,Kwa hiyo Hawa uweza kushambulia mfumo wa hewa na kusababisha mgonjwa kupata kikohozi Cha mda mrefu na kusababisha madhara makubwa kwenye mfumo wa hewa hatimaye kusababisha  mapafu kuoza na kuanza kutoa usaha.

 

 

 

9. Vile vile matumizi ya dawa za kupitia kwenye mishipa Kwa kitaalamu huitwa intravenous injection au iv injection,hizi dawa zikitumiwa mara Kwa mara na isivyosahihi yakifika kwenye mapafu ushambulia mapafu na kusababisha kuoza na kutoa usaha,Kwa hiyo wataalamu wa afya peke yao ndio wenye majukumu ya kuagiza dawa na jinsi ya kuzitumia ili kuepuka madhara kama haya.

 

 

 

10. Tatizo jingine ni kuwepo Kwa aleji au Kwa kiswahili kizuri ni mzio,utokea Kwa wale wagonjwa ambo Huwa na aleji kubwa na vitu mbalimbali kaama vile chakula, maua , manukato na mambo kama hayo, iwapo mgonjwa huyapata mara Kwa mara na kusababisha kutumia madawa Makali kwenye mfumo wa hewa mara Kwa mara usababisha mapafu kuharibika taratibu na hatimaye kusababisha madhara kwenye mfumo wa hewa na kuanza kutoa usaha.pia Kwa wale wenye aleji hizona hawako tayari kuanza matibabu na kusababisha maambukizi ya mara Kwa mara kwenye mfumo wa hewa usababisha tatizo hilo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.

 

 

 

11. Kwa hiyo tunapaswa kuwa makini kuhakikisha kwamba tunaepuka na tatizo hili ambalo utokea kwenye mapafu Kwa kutibu kwanza tatizo la magonjwa ya kinywa Kwa sababu bakteria wengi huweza kujificha kwenye meno na ikitokea wakaenda kwenye mfumo wa upumuaji usababisha madhara makubwa mno ambayo ni pamoja na kushambulia mfumo wa hewa na kusababisha mapafu kuoza na kutoa usaha.

 

 

 

 

12. Pia tunapaswa kutumia dawa mapema pindi tunapoona dalili za kifua kikuu na kuanza dawa mara moja, Kuna wengine wanaweza  kupenda kufahamu dalili za kifua kikuu ingawa unaweza kuona dalili hizi ila usiwe na kifua kikuu ,dalili za mwanzoni ni pamoja na kukohoa wiki mbili Kwa mfululizo, kutokwa na jasho hasa wakati wa usiku,mwili kuhisi hauna nguvu pamoja na homa za mara Kwa mara,uzito kupungua Kila wakati,baada ya kuona dalili kama hizo ni vizuri kabisa kwenda hospital Kwa ajili ya matibabu ili kuweza kuepuka madhara  katika mfumo wa hewa ambayo usababisha kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.

 

 

 

13. Pia ni vizuri kabisa kutibu Kansa kwenye wakati wa hatua za kwanza Kwa sababu Kansa ya mapafu mtu  kama haijagundulika mapema na yenyewe usababisha kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu, Kwa hiyo matibabu ni mapema.

 

 

 

14. Vile vile ni vizuri kuepuka matumizi ya dawa zenye kemikali ambazo pia uweza kuleta madhara kwenye mfumo wa hewa,hasa Kwa wavutaji wa sigara zile kemikali zikiingia kwenye mfumo wa hewa utengeneza sumu ambayo uingia kwenye mapafu na kuyashambulia na kusababisha madhara kwenye mfumo wa ambao ni kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.

 

 

 

15. Pia Kwa wale wanaopenda kutumia dawa za kupitia kwenye mishipa ya damu Kwa kitaalamu intravenous injection wanapaswa pasipokuwa na maagizo kutoka Kwa wataalamu wa afya nao wapo kwenye hatari ya kuambukizwa kwenye mfumo wa hewa na kusababisha mapafu kuoza na kutoa usaha,Kwa hiyo wapendwa tunapaswa kutunza mfumo wa hewa Kwa sababu mapafu yakisha shambuliwa ni hatari,Kwa sababu ya kazi yake kubwa ya kusafirisha hewa,ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya ikitokea hali isiyo ya kawaida kwenye mapafu au kwenye mfumo wa upumuaji.

 

 

 

 

 

a

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 394


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Ninashida Kuna mtu anaumwa pressure Kila anap pima Iko juu il mwil aumuumi at kidg n dawa anatumia unawez kunisaidiaj
Kama unasumbuliwa na presha post hii ni kwa ajili yako. Hapa tutakuoatia ushauri kutokana na swali alilouliza mdau wetu. Soma Zaidi...

Namna ya Kuzuia Mtoto mwenye kifua kikuu (TB).
posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano. Kifua kikuu ni ugonjwa sugu wa kuambukiza na anuwai ya magonjwa ya kliniki yanayosababishwa na Mycobacterium tuberculosis complex. Soma Zaidi...

Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.
Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo Soma Zaidi...

Je kwa mfano mimi nmeupata ukimwi leo na sihitaji kwenda kupima yaaan uanza kujionyesha baada ya muda gani
Watu wengi wamekuwa wakijiuliza kuwa ukimwi huonekana baada ya muda gani toka kuathirika? Soma Zaidi...

Sababu za Ugonjwa wa pumu
Pumu ni ugonjwa wa njia ya upumuaji unaojulikana na kizuizi cha muda mrefu cha njia ya upumuaji. Inahusisha mfumo wa upumuaji unaobana njia ya hewa, Inaweza kuwa ya nje (hii hutokea kwa vijana kutokana na mizio) au ya ndani (hutokea kwa wazee) Soma Zaidi...

UGONJWA WA MALARIA NA TAKWIMU ZA ATHARI YAKE KIDUNIA
Malaria ni katika maradhi ambayo husambazwa na na mbu jike aina ya anopheles. Soma Zaidi...

JITIBU KWA MUAROBAINI: faida za kiafya za muarobaini
1. Soma Zaidi...

ninasumbuliwa Sana na mapunye ya kichwani nimetumia dawa takribani miaka 3
Habari, samahani ninasumbuliwa Sana na mapunye ya kichwani nimetumia dawa takribani miaka 3 ila yanapona Tena baada ya Muda flani yanatokea. Soma Zaidi...

Athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa wajawazito
Post inahusu zaidi athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa wajawazito au ugonjwa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri.ugonjwa huu uleta madhara kwa wajawazito kama tutakavyoona Soma Zaidi...

Dalili za fangasi kwenye mapafu
Posti hii inaonyesha dalili za fangasi kwenye mapafu. Soma Zaidi...

AINA ZA MINYOO: tapeworm, livefluke, roundworm, hookworm, flatworm
AINA ZA MINYOO Minyoo ambao wanaweza kuishi ndani ya mwili wa binadamu wapo aina nying, lakini hapa nitakueleza aina kuu tatu za minyoo hawa. Soma Zaidi...

MATIBABU YA FANGASI
Karibia fangasi wote hawa wanatibika bila ya ugumu wowote maka mgonjwa atakamilisha dozi. Soma Zaidi...