Sifa na vigezo vya dini sahihi

Sifa na vigezo vya dini sahihi

1.

Download Post hii hapa

Sifa na vigezo vya dini sahihi

Vigezo vya dini sahihi na sifa zake

1.DINI SAHIHI ANAYOSTAHIKI KUFUATA MWANAADAMU.
Kulingana na umbile lake, mwanaadamu daima hutamani kuishi kwa furaha na amani ili kufikia lengo la kuumbwa, na hapo ndipo inambidi kuchagua dini (njia sahihi ya maisha) kati ya Uislamu, Ukafiri, Ushirikina au Utawa itakayomtimizia malengo yake.



1.1. Sifa au Vigezo Vya dini sahihi
Dini sahihi ni ile inayomuwezesha mwanaadamu kuishi kwa furaha na amani ya kweli hapa Duniani na Akhera, na ni lazima iwe na sifa zifuatazo;



(a)Dini sahihi lazima ieleze ukweli juu ya maumbile;
Ni lazima ieleze ukweli juu ya mwanaadamu, lengo la kuumbwa kwake, hadhi/nafasi yake, dhima/kazi yake na maumbile yanayomzunguka na viumbe vyote vilivyo hai na visivyo hai, na hatima ya kila kitu.



(b)Dini sahihi ni lazima iwe na kanuni na sheria zinazoendana na maumbile yote;


Kanuni na sheria za dini sahihi ni lazima ziwe sambamba na kanuni za kimaumbile ili kuepusha mgongano wowote wa kimahitajio wa kimwili na kimazingira pia.

(c)Ni lazima itosheleze mahitajio ya mwanaadamu ya kimwili na kiroho;


Pia ni wajibu kwa dini sahihi kuelekeza na kutosheleza hisia za mwanaadamu pindi anapokuwa na hali ya furaha au hali ya majonzi, namna ya kukabiliana nazo ili kubakia katika lengo lake la kuumbwa (maisha).



(d)Dini sahihi pia lazima iwe ni mfumo wa maisha uliokamilika;
Dini sahihi haina budi kuwa na utaratibu kamili wa kila kipengele na Nyanja ya maisha ya kila siku kiuchumi, kisiasa, kiafya, kiutamaduni, kisheria, kielimu, n.k.

(e)Pia dini sahihi ni lazima iwe na ibada maalum zinazombakisha mwanaadamu katika maadili na hadhi yake;


Ni wajibu kwa dini sahihi kuwa na muongozo wa kumuinua na kumbakisha mwanaadamu katika mwenendo mzuri wa kiroho (kiutu) unaoweza kuustawisha mwili na kuleta mahusiano mazuri ya kiutu yasiyo na chuki, husuda, tamaa, kiburi, vurugu, n.k.



(f)Dini sahihi haina budi kuwa ya walimwengu wote na ya nyakati zote;


Ili kufikia lengo la kuumbwa mwanaadamu, dini sahihi ni lazima iwe inawahusu watu wa aina zote (wote), isiwe na jina la mtu au mahali na isiwe na mipaka ya kijiografia, rangi za watu, mahali, nyakati, n.k.



(g)Dini sahihi ni lazima iainishe na kusimamia haki zote za mwanaadamu;


Ni wajibu kwa dini sahihi kutoa na kusimamia haki, hukumu na adhabu kwa usawa na uadilifu kwa watu wote kibinafsi na kijamii bila upendeleo na ubaguzi wowote wa kirangi, taifa, nasaba, cheo au hadhi.



                   

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Main: Dini File: Download PDF Views 1467

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

swala za tahiyatu al masjid, qabliya na baadiya
swala za tahiyatu al masjid, qabliya na baadiya

Muislamu anapoingia Msikitini kabla hajakaa anatakiwa aswali rakaa mbili za maamkizi ya msikiti, Tahiyyatul-Masjid.

Soma Zaidi...
MAANA YA HADITHI SUNNAH
MAANA YA HADITHI SUNNAH

Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila.

Soma Zaidi...
KUAMINI MALAIKA
KUAMINI MALAIKA

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
KUMUAMINI MWENYEZI MUNGU
KUMUAMINI MWENYEZI MUNGU

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
MAANA YA HADITHI SUNNAH
MAANA YA HADITHI SUNNAH

Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila.

Soma Zaidi...