DARSA ZA TAWHID

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

DARSA ZA TAWHID

 Tawhiid.
oKimaana: Ni Umoja au Upweke wa Mwenyezi Mungu (s.w).
oKimatumizi: Ni fikra, mtazamo wa kimapinduzi katika kumkomboa mwanaadamu na aina zote za utumwa wa kibinaadamu na kuwa mtumishi huru wa Muumba wake.

Aina za Tawhiid.
Kuna aina kuu tatu za Tawhiid kama zilivyoainishwa katika aya za Qur’an.
(i) Tawhid Al-Uluuhiyyah – Upweke wa Allah (s.w) katika Uungu wake. Nayo ni Kumpwekesha Mwenyezi Mungu (s.w) katika Uungu wake kwa kutokuwa na mungu mwingine yeyote wa kumuelekea kwa ibada au maombi isipokuwa yeye peke yake. Rejea Qur’an (2:163), (3:62) na (112:1-4).

(ii) Tawhiid Al-Asmaa Wassifaat – Upweke wa Mwenyezi Mungu (s.w) katika Majina na Sifa. Nayo ni kutomsifu Mwenyezi Mungu (s.w) kwa sifa za viumbe au majina ya viumbe na pia kutomsifu kiumbe yeyote kwa sifa za Mwenyezi Mungu (s.w). Rejea Qur’an (57:1-6) na (59:22-24).

(iii) Tawhiid Rabbuubiyya – Upweke wa Mwenyezi Mungu (s.w) katika Ubwana,Utawala na Mamlaka Yake. Kumpwekesha Allah (s.w) katika Ubwana na Utawala wake ni kutofuata na sheria na taratibu za maisha kinyume na zile alizoziweka yeye kwa kumfanya ndiye Mlezi, Mlinzi, Mwendeshaji wa kila kitu. Rejea Qur’an (4:59), (31:14-15), (25:52), (3:149), (3:100) na (5:57). bofya hapa


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Main: Dini File: Download PDF Views 4339

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

KUAMINI MALAIKA

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke?

Je, Mahari inashusha hadhi ya mwanamke?

Soma Zaidi...
DARSA ZA TAWHID

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Lengo la swala

Lengo la Kusimamisha SwalaBila shaka swala imepewa umuhimu mkubwa kiasi cha kufanywa nguzo kubwa ya Uislamu kutokana na lengo lake.

Soma Zaidi...
HISTORIA YA UANDISHI WA HADITHI

Historia fupi ya uandishi wa Hadith za Mtume (s.

Soma Zaidi...