picha

Tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID

Posti hii inahusu zaidi tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID, tunaita tiba ya awali kwa sababu baada ya kupima na kugunduliwa kwamba una tatizo au changamoto ya PID ni vizuri kutumia tiba hiii baadae ndipo utumie dawa.

Tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID.

1. Kwanza kabisa napaswa kusisitiza kwamba hii tiba sio kwamba ni dawa ya kuponyesha bali ni maandalizi ya kutumia dawa ya PID kwa hiyo unapopatwa na tatizo la PID unapaswa kutumia tiba hii ndipo baadae unaweza kuendelea na dawa ulizoagizwa kufanya.

 

2. Unapaswa kuandaa tangawizi vipande vitatu na unaviosha vizuri kabisa ili kuondoa uchafu na wadudu wengine pia unazikuna kama hauna kikunio unaweza kuzitwanga na ziwe kama mfano wa unga hivi .

 

3. Baada ya kupata tangawizi zilizotwangwa unaandaa kitunguu swaumu punje kama kumi na tano hivi nazo uzitwange ziwe laini kama ilivyofanya kwa tangawizi .

 

4. Baada ya maandalizi ya vitunguu saumu andaa vitunguu maji vikate Kaye kwa vipande vidogo vidogo na hakikisha vimeoshwa kwa maji na kutakata vizuri.

 

5. Baada ya maandalizi ya tangawizi, kitunguu swaumu na vitunguu maji changanya vyote kwa ujumla weka maji ya moto na pia unaweza kuweka maji ya baridi , weka kiasi cha lita moja funika vizuri acha ikae kwa masaa sita baada ya hapo chuja vizuri unaweza kutunza kwenye jagi au kifaa chochote kile.

 

6. Tumia hayo maji kwenye glasi changanya na asali mbichi vijiko viwili tumia glasi moja asubuhi,moja mchana na nyingine jioni kwa mda wa siku moja baada ya hapo mwili utakuwa tayari umeuandaa vizuri kwa ajili ya kutumia dawa.

 

7. Pia tiba hii isitumiwe mara kwa mara na watu wenye matatizo ya vidonda vya tumbo kwa sababu ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha asidi.

 

8. Na kama nilivyotangulia kusema hii tiba sio kwa sababu ya kutibu PID bali ni kwa sababu ya maandalizi ya kuanza kutumia dawa za PID kwa hiyo ukitumia mchanganyiko huu unakusudia na kukupa maandalizi mazuri ya kutumia dawa za PID

 

 

 

 

 

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 10282

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Huduma kwa mama ambaye mimba imetoka moja kwa moja.

Post hii inahusu zaidi huduma kwa mama ambaye mimba imetoka moja kwa moja, aina hiyo ya mimba kwa kitaalamu huitwa complete abortion.

Soma Zaidi...
Dalili za maumivu ya hedhi

Maumivu ya hedhi (dysmenorrhea) ni maumivu makali au ya kubana sehemu ya chini ya tumbo. Wanawake wengi hupatwa na Maumivu ya hedhi kabla tu na wakati wa hedhi zao. Kwa wanawake wengine, usumbufu huo ni wa kuudhi tu. Kwa wengine,&nbsp

Soma Zaidi...
Mimi ni mama ninaye nyonyesha toka nimejefunguwa sijawai kuziona siku zangu lakini nilipo choma sindano za yutiai nikaaza kutokwa na tamu kama siku tano na mwanangu ana mwaka moja je ninahatali ya kubeba mimba

Kunyonyesha ni moja katika njia za asili za kuzuia upatikanaji wa miba nyingine. Hata hivyo hii haimaanishi kuwa huwezi kupata mimba ukiwa unavyonyesha.

Soma Zaidi...
Dalili za Utasa wa wanaume

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Utasa wa Mwanaume hutokana na uzalishaji mdogo wa mbegu za kiume, utendakazi usio wa kawaida wa manii au kuziba kwa manii ambayo huzuia utoaji wa mbegu za kiume. Magonjwa, majeraha, matatizo ya kiafya sugu, u

Soma Zaidi...
Maambukizi katika mfumo wa Uzazi wa mwanamke

Maambukizi kwenye Njia ya Uzazi kwa kifupi hujulikana Kama PID.ni Maambukizi ya mfumo wa Uzazi yanayoathiri wanawake, Maambukizi haya kwa Kawaida huhusisha sehemu Kama shingo ya uzazi,nyuma ya mfuko wa Uzazi na mirija ya uzazi.

Soma Zaidi...