Tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID
Posti hii inahusu zaidi tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID, tunaita tiba ya awali kwa sababu baada ya kupima na kugunduliwa kwamba una tatizo au changamoto ya PID ni vizuri kutumia tiba hiii baadae ndipo utumie dawa.
Tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID.
1. Kwanza kabisa napaswa kusisitiza kwamba hii tiba sio kwamba ni dawa ya kuponyesha bali ni maandalizi ya kutumia dawa ya PID kwa hiyo unapopatwa na tatizo la PID unapaswa kutumia tiba hii ndipo baadae unaweza kuendelea na dawa ulizoagizwa kufanya.
2. Unapaswa kuandaa tangawizi vipande vitatu na unaviosha vizuri kabisa ili kuondoa uchafu na wadudu wengine pia unazikuna kama hauna kikunio unaweza kuzitwanga na ziwe kama mfano wa unga hivi .
3. Baada ya kupata tangawizi zilizotwangwa unaandaa kitunguu swaumu punje kama kumi na tano hivi nazo uzitwange ziwe laini kama ilivyofanya kwa tangawizi .
4. Baada ya maandalizi ya vitunguu saumu andaa vitunguu maji vikate Kaye kwa vipande vidogo vidogo na hakikisha vimeoshwa kwa maji na kutakata vizuri.
5. Baada ya maandalizi ya tangawizi, kitunguu swaumu na vitunguu maji changanya vyote kwa ujumla weka maji ya moto na pia unaweza kuweka maji ya baridi , weka kiasi cha lita moja funika vizuri acha ikae kwa masaa sita baada ya hapo chuja vizuri unaweza kutunza kwenye jagi au kifaa chochote kile.
6. Tumia hayo maji kwenye glasi changanya na asali mbichi vijiko viwili tumia glasi moja asubuhi,moja mchana na nyingine jioni kwa mda wa siku moja baada ya hapo mwili utakuwa tayari umeuandaa vizuri kwa ajili ya kutumia dawa.
7. Pia tiba hii isitumiwe mara kwa mara na watu wenye matatizo ya vidonda vya tumbo kwa sababu ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha asidi.
8. Na kama nilivyotangulia kusema hii tiba sio kwa sababu ya kutibu PID bali ni kwa sababu ya maandalizi ya kuanza kutumia dawa za PID kwa hiyo ukitumia mchanganyiko huu unakusudia na kukupa maandalizi mazuri ya kutumia dawa za PID
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 ai web app 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Vyanzo vya kuharibika kwa mimba ya miezi kuanzia 0-3
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuharibika kwa mimba kuanzia miezi zero mpaka miezi mitatu, kwa sababu hii ni miezi ya kwanza kabisa Kuna sababu au vyanzo vya kuharibika kwa mimba katika kipindi hiki.
Soma Zaidi...Dalili za Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto
Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo ujitokeza kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu cha mtoto mdogo, kwa kawaida kitovu cha mtoto kama kiko vizuri kinapona kwa mda mchache na kinakauka mapema iwezekanavyo bila kuwa na tatizo lolote ila kama kuna Dal
Soma Zaidi...Sababu za kutoka mimba yenye miezi Saba na nane
Posti hii inahusu zaidi sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na miezi Saba na nane kwa kawaida mtoto wa hivi anakuwa hajafikisha mda wake kwa hiyo uzaliwa akiwa na miezi saba na nane, kwa hiyo kuna sababu mbalimbali kama tutakavyoona
Soma Zaidi...Nini kinasababisha uume kutoa maji meupe bila muwasho,na tiba yake ni ipi
Je unasumbuliwa na Majimaji kwenye uume. Je unapata miwasho, ama maumivu wakati wakukojoa.
Soma Zaidi...Ay ni iv kipimo cha mimb uanz kutoa majb ndan ya mda gan wik mwez au iko vipi?
Kipimo cha Mlimba huweza kuonyesha mimba changa mapema sana. Pia ni rahisi kutumia na kinapatikana kwa bei nafuu. Je ungeoendavkujuwa ni muda gani kinatoa majibu sahihi?
Soma Zaidi...