picha

Tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID

Posti hii inahusu zaidi tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID, tunaita tiba ya awali kwa sababu baada ya kupima na kugunduliwa kwamba una tatizo au changamoto ya PID ni vizuri kutumia tiba hiii baadae ndipo utumie dawa.

Tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID.

1. Kwanza kabisa napaswa kusisitiza kwamba hii tiba sio kwamba ni dawa ya kuponyesha bali ni maandalizi ya kutumia dawa ya PID kwa hiyo unapopatwa na tatizo la PID unapaswa kutumia tiba hii ndipo baadae unaweza kuendelea na dawa ulizoagizwa kufanya.

 

2. Unapaswa kuandaa tangawizi vipande vitatu na unaviosha vizuri kabisa ili kuondoa uchafu na wadudu wengine pia unazikuna kama hauna kikunio unaweza kuzitwanga na ziwe kama mfano wa unga hivi .

 

3. Baada ya kupata tangawizi zilizotwangwa unaandaa kitunguu swaumu punje kama kumi na tano hivi nazo uzitwange ziwe laini kama ilivyofanya kwa tangawizi .

 

4. Baada ya maandalizi ya vitunguu saumu andaa vitunguu maji vikate Kaye kwa vipande vidogo vidogo na hakikisha vimeoshwa kwa maji na kutakata vizuri.

 

5. Baada ya maandalizi ya tangawizi, kitunguu swaumu na vitunguu maji changanya vyote kwa ujumla weka maji ya moto na pia unaweza kuweka maji ya baridi , weka kiasi cha lita moja funika vizuri acha ikae kwa masaa sita baada ya hapo chuja vizuri unaweza kutunza kwenye jagi au kifaa chochote kile.

 

6. Tumia hayo maji kwenye glasi changanya na asali mbichi vijiko viwili tumia glasi moja asubuhi,moja mchana na nyingine jioni kwa mda wa siku moja baada ya hapo mwili utakuwa tayari umeuandaa vizuri kwa ajili ya kutumia dawa.

 

7. Pia tiba hii isitumiwe mara kwa mara na watu wenye matatizo ya vidonda vya tumbo kwa sababu ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha asidi.

 

8. Na kama nilivyotangulia kusema hii tiba sio kwa sababu ya kutibu PID bali ni kwa sababu ya maandalizi ya kuanza kutumia dawa za PID kwa hiyo ukitumia mchanganyiko huu unakusudia na kukupa maandalizi mazuri ya kutumia dawa za PID

 

 

 

 

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 10212

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Zijue mbegu za kiume zilizo bora.

Posti hii inahusu zaidi mbegu ambazo ni nzima na ambazo zina sifa ya kutungisha mimba kwa hiyo mbegu hizi utazigundua kwa kuwa na sifa zifuatazo.

Soma Zaidi...
Sababu za mimba ya miezi 4-6 kutoka.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mimba ya miezi kuanzia minne mpaka sita kutoka , Kuna kipindi mimba kuanzia miezi mimne mpaka sita utoka kwa sababu mbalimbali.

Soma Zaidi...
Mke Wang Ana tatizo la tumbo kuuma chini upande wa kushoto akishika ni pagumu ,anapatwa na kichefuchef tumbo kujaa ges na kujiisi kusiba he mtanisaidije ili kuondoa tatizo Hilo Ila anaujauzito wa wiki mbili

Miongoni mwa changamoto za ujauzito ni maumivu ya tumbo. Maumivu haya yanawezakuwaya kawaida ama makali zaidi. Vyema kufika Kituo cha Afya endapoyatakuwa makali.

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo wakatu wa tendo la ndoa

Jifunze sababu kuu zinazosababisha kuhisi maumivu makali ya tumbo wakati wa kushiriki tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Tatizo la kutokwa na utelezi wenye damu baada ya hedhi

Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali za kutokwa na damu baada ya hedhi hili ni tatizo ambalo uwapata wanawake wengi pamoja na akina Mama kwa sababu ya kutokwa na damu yenye utelezi baada ya hedhi.

Soma Zaidi...
Ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito, ni ugonjwa unaowapata sana akina mama wajawazito na uisha tu pale Mama anapojifungua kwa hiyo tunapaswa kujua wazi sababu za ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.

Soma Zaidi...