Tofauti kati ya sura za makkah na madinah
Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)
- Tofauti kati ya Sura za Makkah na Madinah
|
Sura za Makkah |
Sura za Madinah |
|
1. Walengwa. Walengwa walikuwa waumini waliosimu mwanzo wa Utume. |
Zililenga Maadui wa Dola ya Kiislamu Madinah wakiwemo; Wanafiq, Washirikina, Wayahudi na Wakristo. |
|
2. Ujumbe. Sehemu kubwa ya ujumbe ni kujenga imani juu ya Mwenyezi Mungu (s.w), Malaika, Vitabu, Mitume, Siku ya Mwisho na Qudra yake. |
Ujumbe ulilenga ujenzi wa Dola na jamii ya Kiislamu Madinah kupitia sheria na hukumu mbali mbali. |
|
3. Muundo wa sura. Sura nyingi ni fupi na zina aya fupi fupi zenye lengo moja. |
Sura nyingi ni ndefu na zina aya ndefu zenye ufafanuzi zenye lengo la utekelezaji wa sheria.. |
|
4. Mbinu Zimetumia lugha fupi ya mchomo kwa walengwa kwa kutumia viapo, historia ya watu waliopita, kuwahofisha na kuwakatisha tamaa maadui wa Uislamu na kuwatia moyo na kuwaliwaza waumini katika kutekeleza ujumbe wa Qur’an. |
Zimetumia lugha ya sheria na ufafanuzi katika ujenzi wa Dola ya Kiislamu Madinah, kwa kutumia historia ya Mitume ili kuwaliwaza waumini kupigania Dini na kuwakatisha tamaa maadui wao wakiwemo; makafiri, washirikina, wanafiq na Wakristo. |
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 web hosting 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Dai kuwa Muhammad (s.a.w) aliitunga Qur-an ili Kuwania Madaraka na Ukubwa
(x) Dai kuwa Muhammad (s.
Soma Zaidi...Amri ya Kuchinja Ng'ombe
Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr.
Soma Zaidi...Hoja juu ya kukubalika hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Je Qur-an ilikusanywa na kuandikwa katika msahafu wakati wa uongozi wa Abu-Bakr(r.a)
Je Qur-an ilikusanywa na kuandikwa katika msahafu wakati wa uongozi wa Abu-Bakr(r.
Soma Zaidi...