UFUPISHO WA ALIFU LELA ULELA KITABU CHA KWANZA

Posti hii inakwenda kukisimulia kuhusu hadithi za alifu lela ulela KITABU CHA KWANZA

UFUPISHO WA ALIFU LELA ULELA KITABU CHA KWANZA

Katika nchi za China, Hindi, Uarabuni na Uajemi alikuwepo mfalme aliyefahamika na kuheshimika sana kwa uhodari wake na utawala wake mzuru. Mfalme huyu alikuwa na watoro wawili ambao ni Shahariyar na Shahzaman. Watoto hawa walikuwa mahodari na walifahamika sana. Alipofariki baba yao mtoto mkubwa alitawala kiti cha baba yake kuanzia makao makuu na mdogo wake akaendelea kutawala maeneo ya Samarqand.

 

Baada ya kutengena kwa muda ndugu wawili hawa walipanga kukutana. Makutano yao yalifanikiwa kupangwa na hatimaye wakakutana. Katika wakati kama huu wa kukutana kwa ndugu wawili hawa kulitokea hali za kusalitiwa na wakezao. Shahariyar alikuwa na mkewake aliyempenda sana na hakuamini kuwa inaweza kutokea siku akasalitiwa na mkewe. Baada ya usaliti huu aliamini kuwa hakuna tena mwanamke mkweli duniani kote. Hivyo akaweka nadhiri ya kuoa mke mpya aliye kigori na kumuuwa kila ifikapo asubuhi.

 

Kiapo hiki cha Sultani huyu kilikuwa kweli na alikuwa akifanya hivyo yaani anaowa jioni na asubuhi anauwa. Hali ilikuwa ngumu kiasi kwamba watu wakawa wanawakimbiza mabinti zao mjini. Sifa zote nzuri za Sultani huyu zikaanza kuwa mbaya kwa kitendo chake cha kuuwa watoto wa kike. Kazi yote ya kutafuta mabinti wa kuolewa na mfalme pamoja na kazi ya kutekeleza ahadi ya mfalme kuwauwa mabinti hawa alipewa mmoja katika mawaziri wa Sultani huyu.

 

Sultani huyu alikuwa na mabinti wawili ambao ni Schehrazade na Dinarzade. Mabinti hawa walikuwa ni wazuri sana na walipendana na hata hivyo walipata upendo mkubwa sana kutoka kwa mbaba yao. Schehrazade ambaye ndiye mkubwa alikuwa ni mrembo zaidi na alikuwa na taaluma mbalimbali na alikuwa na elimu za mambo mengi hata ya kisayanzi na masimulizi ya fasihi. Watu wa nchi hii waliamini kuwa uzuri alonao Schehrazade anafaa kuilewa na mfalme au mtoto wa mfalne na si mtu mwingine.

 

Sikumoja katika mazungumzo ya kifamilia kati ya waziri na watoto wake Schehrezade alitowa ombi la kushangaza kwa baba yake na kumwambia kuwa anatakakukomesha tabia ya mfalme ya kuuwa mabinti hivyo anataka siku ifiataya aolewe yeye. Waziri alishangaa na kumuonya mwanae lakini hakusikia. Akajaribu kumtisha na akamsimulia hadithi ya mfugaji na mkewe lakini msmamo wake hauku badilika. Basi harusi ikafanyika na Shehrazadw akapanga mpago na Dinarzade juu ya kutaka kukomesha tabia ya Sultani.

 

Usiku nyumbani kwa mfalme Dinarzade alisikika akimuamsha dadayake Schehrazade ambaye anatarajiwa kuuliwa ifikap asubuhi. Dinarzade alimwambia dada yake apigie hadithi nzuri iwe kama ndio mazungumzo ya kuagana. Schehrazade aluimtaka idhini mfalme na kukubaliwa. Akaanza kumsimulia hadithi ya mfanya biashara na jini. Masimulizi ya hadithi hii yalionekana kumvutia na Sultani pia. Schehrazade kwa ufundi wake wa kusimulia hadithi aliikata hadithi hii na kumwambia Sultani akimuongeza siku zaidi ya kuishi ataimaliza.

 

Sultani alimpa siku zaidi Schehrazade ili amalizie hadithi zake. Utamu uliendelea kumpanda Sultani na kila siku hadithi zilikuwa zinaishia patamu. Hivyo Schehrazade akaendelea kupata muda zaidi wa kuishi. Dada huyu alisimulia hadithi ya mvuvi na jini, hadithi ya chongo watatu na mabinti wa baghadad na nyinginezo hata akafikia kwenye hadithi ya Sinbad. Dada huyu alipomaliza hadithi hii akabakiwa na kuelezea yalotokea kwa mtoto wa Sinbad.

 

Basi siku ilofata baada ya kuisha kwa hadithi ya Sinbad Scheherazade akaanza kusimulia kilichotokea kwa mtoto wa Sinbad alozaliwa na bint ‘Aisha mtoto wa mfalme. Scheherazade akamueleza kuwa atahaya ya msimulia hadithi nzuri zaidi ya ile a mtoto wa Sinbad. Hapo Sulltani akamwambia asimulie hiyo hadithi nzuri zaidi ya mtoto wa Sinbad. Hapo Scheherazade akaanza kusimulia hadithi ifuatayo.



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021-11-07     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 690


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Kuingia kwa wageni
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Ndani ya pango la makaburi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Safari saba za sinbad
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Hadithi ya mfalme na waziri wake
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Ujio wa wageni wa baraka
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Safari ya pili ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Kujiandaa kwa ajili ya kumuona daktari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya mambo ya kujiandaa kwa ajili ya kumuona daktari Soma Zaidi...

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, baada ya kijana wa kiume wa binti mfalme kuoa yule ndugu yake baba anafanya sherehe kubwa na wake wenza wamepata habari kwamba kijana wa kiume wa mfalme ameoa ndugu yake wakaamuru kunyamaza il Soma Zaidi...

simulizi za hadithi, burudani na riwaya za kusisimua zenye visa na mikasa mbalimbali
Hadithi za alif Lela U Lela kitabu cha kwanza Soma Zaidi...

Hadithi ya Kaka wa pili wa kinyozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Hadithi iliyosimuliwq na mlevi mbele ya sultani
Posti hii inakwenda kukusimulia hadithi iliyosimuliwa na mlevi mbele ya sultan Soma Zaidi...

Dalili za vidonda vya tumbo
Vidonda vya tumbo no tatizo linalotokea baada ya kuta za tumbo au utumbo mdogo kuwa na vidonda,hutokea baada ya ukuta wenye ute unaozuia kemikali za kuyeyusha chakula unaitwa mucus kuharibika. Vidonda vya tumbo (peptic ulcers) imegawanyika katika ma Soma Zaidi...