UGONJWA WA DONDAKOO NA NAMNA UNAVYOWEZA KUENEA


image


Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.


Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

1. Dondakoo ni ugonjwa unaosababishwa na sumu ya bakteria ambaye kwa kitaalamu huitwa corynebacterium diphtheria, bakteria huyu ushambulia sehemu za pua, koo na wakati mwingine maumivu kwenye masikio hali hii upelekea mgonjwa kushindwa kupumua na wakati mwingine kushindwa kumeza, kwa sababu ugonjwa huu usababishwa na bakteria kuna dawa mbalimbali za antibiotics zinaweza kuponya ugonjwa huu, antibiotics hizo ni kama vile penicillin au erythromycin.

 

2. Ugonjwa huu ushambulia hasa watoto na unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwa njia zifuatazo kama vile  mtu akipiga chagua yale maji maji yakimgusa mtu mwingine hasa kinywani mtu huyo anaweza akapata, kwa hiyo wakati wa kupiga chafya tunapaswa kuwa makini au tunapopiga chafya tunapaswa kupigia kwenye vitambaa ili kuepuka kusambaza ugonjwa kutoka sehemu moja kwenda kwa mwingine, au kama mama au mlezi wa watoto wadogo wanapaswa kuwa makini sana wasije kuambukiza watoto.

 

3. Ugonjwa huu pia unaweza kusambaa kwa njia ya kutumia vitu vyenye bakteria kama vile kunywea maji kwenye kikombe au glass ya mtu mwenye Maambukizi, au kutumia kijiko bila kuosha kutoka kwa mtu mwenye Maambukizi kwa hiyo bakteria usambaa kutoka kwa mwenye Maambukizi kwenda kwa hasiye na Maambukizi, kwa hiyo kila mtu anapaswa kutumia vifaa vyake hasa hasa vile vinavyoongozwa moja kwa moja kinywani au ni vizuri kuosha vyombo kwa maji moto ili kuweza kuua wadudu wanaosambaza na Kuleta madhara.

 

4. Pia hawa wadudu wanaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwa kutumia vitu kwa pamoja kama vile taulo na nguo zenye jasho kutoka kwa mtu mwenye Maambukizi na vile vile watu wanaokula peni, penseli na vfutio ambavyo vimetumbukizwa kinywani na mtu mwenye maambukizi na ambaye hana Maambukizi naye akija kutumia na kuweka mdomoni anaweza kupata, kwa hiyo kila mtu anapaswa kutumia vifaa vyake hasa kwa watoto ambao wako chekechekea wanapaswa kuangaliwa kwa makini ili kuepuka kuongeza kwa Maambukizi.

 

5. Kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua kuwa ugonjwa huu upo kwenye jamii na usipotibiwa mapema unaweza kuleta madhara makubwa kwa hiyo tunapaswa kuwapeleka watoto  watoto wapewe chanjo mapema ili kuweza kuepuka madhara  mbalimbali ambayo yanaweza kutokea pia jamii inapaswa kujua Dalili zote za ugonjwa huu ili kuweza kuwahi mapema kwenda hospitalini na pia watu wajifunze kujua jinsi ugonjwa huu unavyoenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    2 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    4 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    5 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    6 Magonjwa na afya    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Dalili za Kiharusi Cha joto la mwili.
Kiharusi cha joto ni hali inayosababishwa na joto la juu la mwili wako, kwa kawaida kama matokeo ya kufichuliwa kwa muda mrefu au bidii ya mwili katika joto la juu. Aina hii mbaya zaidi ya jeraha la joto, kiharusi cha joto kinaweza kutokea ikiwa joto la mwili wako litapanda hadi 104 F (40 C) au zaidi. Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa kisonono, sababu zake nanjia za kujilinda.
Kisonono husababishwa na bakteria. Bakteria ya kisonono mara nyingi hupitishwa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine wakati wa kujamiiana, ikiwa ni pamoja na kujamiiana kwa mdomo, mkundu au uke. Soma Zaidi...

image Aina kuu tatu za vyakula na kazi zake
Posti hii inahusu zaidi Aina kuu tatu za vyakula na kazi zake, hii ni Aina tatu za vyakula na kazi zake jinsi zinavyofanya kazi, hufanya kazi kama ifuatavyo, Soma Zaidi...

image Fahamu Ugonjwa wa misuli kuwa dhaifu.
hali ambayo misuli unayotumia kwa hotuba ni dhaifu au unapata shida kuidhibiti mara nyingi inaonyeshwa na usemi wa kufifia au polepole ambao unaweza kuwa mgumu kuelewa. Sababu za kawaida za Ugonjwa huu ni pamoja na matatizo ya mfumo wa neva (neurolojia) kama vile kiharusi, jeraha la ubongo, uvimbe wa ubongo, na hali zinazosababisha ulemavu wa uso au udhaifu wa ulimi au koo. Dawa fulani pia zinaweza kusababisha dysarthria. Soma Zaidi...

image Tiba mbadala ya fangasi wa uumeni
Somo hili linakwenda kukuletea tiba mbadala ya fangasi wa uumeni Soma Zaidi...

image Namna Ugonjwa wa UKIMWI unavyoambukizwa.
UKIMWI (acquired immunodeficiency syndrome) ni hali ya kudumu, inayoweza kutishia maisha inayosababishwa na virusi vya ukimwi (VVU) Kwa kuharibu mfumo wako wa kinga, VVU huingilia uwezo wa mwili wako wa kupambana na viumbe vinavyosababisha magonjwa. Inaweza pia kuenea kwa kugusa damu iliyoambukizwa au kutoka kwa mama hadi kwa mtoto wakati wa ujauzito, kuzaa au kunyonyesha.Inaweza kuchukua miaka kabla ya VVU kudhoofisha mfumo wako wa kinga hadi kuwa na UKIMWI. Hakuna tiba ya VVU/UKIMWI, lakini kuna dawa ambazo zinaweza kupunguza kasi ya kuendelea kwa ugonjwa.Dawa hizi zimepunguza vifo vya UKIMWI katika mataifa mengi yaliyoendelea. Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa UTI
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa UTI Soma Zaidi...

image Sheria za kutunza usafi wakati wa upasuaji.
Posti hii inahusu zaidi sheria za kutunza usafi wakati wa upasuaji, iwapo sheria mojawapo ikienda kinyume ijulikane kuwa usafi haujaenda sawa na pengine kwa kitaalamu huitwa contamination. Soma Zaidi...

image Fahamu Magonjwa yanayowapata watoto chini ya miaka mitano
Posti hii inaelezea kuhusiana na Magonjwa mbalimbali ambayo watoto chini ya miaka wanaweza kuyapata kiurahi. Soma Zaidi...

image Walio kwenye hatari ya kupata UTI
Posti hii inahusu zaidi watu walio kwenye hatari ya kupata UTI, ni watu ambao wako kwenye hatari ya kupata ugonjwa wa UTI kwa sababu ya mazingira mbalimbali kama ifuayavyo. Soma Zaidi...