picha

Ujue ugonjwa wa tauni

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa tauni ambao kwa kitaalamu huitwa plague ni Ugonjwa unaosababishwa na wadudu ambao huitwa kitaalamu huitwa yersinia pestis ambao ukaa ndani ya panya.

 Ujue ugonjwa wa tauni.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kuwa ugonjwa wa tauni ni Ugonjwa unaosababishwa na wadudu wanaoitwa kwa kitaalamu yersinia pestis wadudu hawa uishi ndani ya panya na viroboto ambao ufyonza damu kwenye panya ufyonza pamoja na wadudu hawa, na pia viroboto uweza kung'ata binadamu na kuingiza wadudu wanaoitwa yersinia pestis ambao usababisha ugonjwa wa tauni ambao uwatesa watu wengi na kusababisha madhara mbalimbali kwenye jamii.

 

2. Ugonjwa huu umeenea katika sehemu mbalimbali za Afrika, Asia, na Amerika inavyokadiriwa ni kuwa kuanzia mwaka elfu moja mia tisa tisini na nne mpaka elfu mbili na tatu watu elf mbili mia nane na hamsini wameripotiwa na shirika la WHO, asilimia tisini waliokuwa wameugua ugonjwa huu ni waafrika ukilinganisha na mataifa mengine ,kwa hiyo na Tanzania mpaka sasa kuna sehemu ambapo ugonjwa bado upo na unaowasumbua watu sehemu ambazo zinapatwa na Ugonjwa huu ni sehemu zenye unyevunyevu kwa wingi ukilinganisha na sehemu nyingine.

 

3. Ugonjwa huu kwa ujumla unaweza kutibiwa na kupotea kabisa kwenye jamii kwa sababu watu wanapaswa kuzingatia usafi ili kuepuka kuwepo kwa panya ambao wanatunza hawa wadudu na pia kwenye kipindi cha mavuno watu wanapaswa kuwa makini ili kuweza kuepuka kuongezeka kwa panya ambao ndio chanzo cha Ugonjwa huu,kwa wakati mwingine dalili za Ugonjwa huu uchanganya watu na kuwa kama Dalili za kawaida kama vile homa na mwili kuishiwa nguvu ila zinabadilika kadri ugonjwa inavyoongezeka.

 

4.Dalili nyingine ambazo zinaweza kujitokeza ni kama vile miwasho kwenye mwili, maumivu ya kichwa ambayo yanaweza kuanza taratibu na ukitumia dawa yanaisha na baadae yanaanza tena  maumivu kwenye mwili, kichefuchefu na kutapika, kuwepo kwa vipele kwenye kwapa, na Dalli hizi utofautiana na kuongezeka kadri siku na mda unavyoenda.

 

5.Kwa hiyo jamii nzima inapaswa kuelimishwa kuhusu Ugonjwa huu na kujua Dalili zake kwa sababu wakati mwingine Dalili hizi ufanana na magonjwa mengine ya kawaida kwa hiyo ni lazima kuzijua kwa uhakika ili kuweza kupata huduma sahihi na kuepukana na madhara mengine makubwa.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 4499

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 ai web app     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Zifahamu sofa za seli

Seli ni chembechembe hai ambazo zimo ndani ya mwili wa binadamu na hufanya kazi mbalimbali kwenye mwili, binadamu hawezi kuishi bila seli.

Soma Zaidi...
Dalili za awali za ugonjwa wa kizukari

ugonjwa wa kisukari ni moja katika magonjwa hatari sana, na mpaka sasa bado hauna matibabu ya kuponya moja kwa moja

Soma Zaidi...
Dalili za madonda ya koo

Posti hii inahusu zaidi magonjwa ya koo, ni ugonjwa unaoshambulia sana sehemu ya koo la hewa, na na huwa na dalili zake kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Dalili za uvimbe kwenye kinywa

Post hii inahusu dalili za uvimbe kwenye kinywa ambapo kitaalamu hujulikana Kama oral candidiasis Uvimbe kwenye kinywa husababisha vidonda vyeupe, kwa kawaida kwenye ulimi au mashavu ya ndani. Wakati mwingine uvimbe kwenye kinywa huweza ku

Soma Zaidi...
Aina za kisukari

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu aina za kisukari

Soma Zaidi...
Yajuwe maradhi mbalmbali ya ini na chanzo chake

Ini ni moja ya ogani za mwili ambazo husumbuliwa na maradhi hatari sana. Katika post hii utakwend akuyajuwa maradh hatari ambayo hushambulia ini. Pia utajifunza jinsi a kujikinga na maradhi hayo.

Soma Zaidi...