picha

Ujue ugonjwa wa tauni

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa tauni ambao kwa kitaalamu huitwa plague ni Ugonjwa unaosababishwa na wadudu ambao huitwa kitaalamu huitwa yersinia pestis ambao ukaa ndani ya panya.

 Ujue ugonjwa wa tauni.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kuwa ugonjwa wa tauni ni Ugonjwa unaosababishwa na wadudu wanaoitwa kwa kitaalamu yersinia pestis wadudu hawa uishi ndani ya panya na viroboto ambao ufyonza damu kwenye panya ufyonza pamoja na wadudu hawa, na pia viroboto uweza kung'ata binadamu na kuingiza wadudu wanaoitwa yersinia pestis ambao usababisha ugonjwa wa tauni ambao uwatesa watu wengi na kusababisha madhara mbalimbali kwenye jamii.

 

2. Ugonjwa huu umeenea katika sehemu mbalimbali za Afrika, Asia, na Amerika inavyokadiriwa ni kuwa kuanzia mwaka elfu moja mia tisa tisini na nne mpaka elfu mbili na tatu watu elf mbili mia nane na hamsini wameripotiwa na shirika la WHO, asilimia tisini waliokuwa wameugua ugonjwa huu ni waafrika ukilinganisha na mataifa mengine ,kwa hiyo na Tanzania mpaka sasa kuna sehemu ambapo ugonjwa bado upo na unaowasumbua watu sehemu ambazo zinapatwa na Ugonjwa huu ni sehemu zenye unyevunyevu kwa wingi ukilinganisha na sehemu nyingine.

 

3. Ugonjwa huu kwa ujumla unaweza kutibiwa na kupotea kabisa kwenye jamii kwa sababu watu wanapaswa kuzingatia usafi ili kuepuka kuwepo kwa panya ambao wanatunza hawa wadudu na pia kwenye kipindi cha mavuno watu wanapaswa kuwa makini ili kuweza kuepuka kuongezeka kwa panya ambao ndio chanzo cha Ugonjwa huu,kwa wakati mwingine dalili za Ugonjwa huu uchanganya watu na kuwa kama Dalili za kawaida kama vile homa na mwili kuishiwa nguvu ila zinabadilika kadri ugonjwa inavyoongezeka.

 

4.Dalili nyingine ambazo zinaweza kujitokeza ni kama vile miwasho kwenye mwili, maumivu ya kichwa ambayo yanaweza kuanza taratibu na ukitumia dawa yanaisha na baadae yanaanza tena  maumivu kwenye mwili, kichefuchefu na kutapika, kuwepo kwa vipele kwenye kwapa, na Dalli hizi utofautiana na kuongezeka kadri siku na mda unavyoenda.

 

5.Kwa hiyo jamii nzima inapaswa kuelimishwa kuhusu Ugonjwa huu na kujua Dalili zake kwa sababu wakati mwingine Dalili hizi ufanana na magonjwa mengine ya kawaida kwa hiyo ni lazima kuzijua kwa uhakika ili kuweza kupata huduma sahihi na kuepukana na madhara mengine makubwa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 4272

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Sababu za mngurumo wa moyo

Mngurumo wa moyo ni sauti wakati wa mzunguko wa mapigo ya moyo wako kama vile kutetemeka inayotolewa na damu yenye msukosuko ndani au karibu na moyo wako. Sauti hizi zinaweza kusikika na kifaa kinachojulikana kama stethoscope. Mapigo ya moyo ya kawaida

Soma Zaidi...
Dalili, chanzo, sababu na vmambo hatari kuhusu kifua kikuu

Katika makala hii utajifunza kuhusu kifua kikuu, dalili zake, sababu zake, chanzo chake na mambo hatari kwa mgonjwa.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujilinda na maradhi ya ini

Hapa nitakueleza namna ambavyounaweza kupunguza hatari ya kupata maradhi ya ini. Kwa njia hizi unaweza kujikina wewe na wengineo na maradhi haya hatari ya ini.

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kushoto

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa upungufu wa Adrenali.

Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa upungufu wa Adrenali ni ugonjwa ambao hutokea wakati mwili wako hutoa kiasi cha kutosha cha homoni fulani zinazozalishwa na tezi zako za adrenali. ugonjwa huu hutokea katika makundi yote ya umri na huathiri

Soma Zaidi...
MARADHI MENGINE 10 YANAYOTOKANA NA MBU ( matende, ngirimaji, homa ya manjano, n.k

Tofauti na maradhi yaliyotajwa hapo juu pia tafiti za kisayansi zimethibitisha kuwepo kwa maradhi mengine hatari yanayosambazwa na mbu, kama vile ngirimaji pamoja na matende.

Soma Zaidi...