Umuhimu wa kupima virus vya ukimwi kwa wajawazito na wanaonyonyesha
Post hii inahusu umuhimu wa kupima virus vya ukimwi kwa mama wajawazito na wanaonyonyesha. Ni hatua ya kupima Mama akiwa mjamzito na wakati wa kunyonyesha ili kuepuka hatari ya kumwambikiza mtoto
Umuhimu wa kupima virus vya ukimwi kwa mama mjamzito na wakati anaponyonyesha.
1. Tunajua wazi Mama akiwa mjamzito pale anapogundua kubwa ana mimba tu anapaswa kuja kliniki kupima maambukizi pamoja na mme wake, pengine Mama anaweza kuja kupima kwa Mara ya kwanza hasikutwe na virusi na akija kupimwa mara ya pili kabla ya kujifungua hasikutwe navyo lakini anaweza kuwa navyo kwa sababu ya kuwepo kwa hali mbalimbali vinaweza visionekane kwa hiyo anapaswa kupima tena akiwa ananyonyesha kwa sababu anaweza kupata ndani ya mda huo lengo ni kumzuia mtoto hasipatwe na Maambukizi.
2. Kwa kufanya vipimo vya marudio kwa mara tatu na wengine wanapima zaidi wakati wa ujauzito na kunyonyesha huweza kutambua hali ya Wazazi kwa ujumla na ikiwa Maambukizi yakiwepo ni rahisi kuanza Dawa mapema ili kuweza kufuvaza makali ya virusi vya Ukimwi kwa ajili kuimarisha afya ya mzazi na kumkinga mtoto dhidi ya Maambukizi, lakini Mama hasipoanza dawa mapema anaweza kumwambikiza mtoto na mtoto akazaliwa na Maambukizi.
3.Pia kwa kutumia dawa hizi umsaidie kuzuia magonjwa nyemelezi kwa Mama na mtoto pia kama vile ugonjwa wa kifua kikuu, Malaria, Magonjwa ya ngozi kupungukiwa na kinga ambapo upelekea Mama kubwa na mkanda wa jeshi na magonjwa mengine mengi uweza kutokea kwa sababu ya kuwepo kwa kinga ndogo ya mwili kwa hiyo Mama kama hajapima ugonjwa wa VVU na kuona magonjwa Mengi anapaswa kwenda kupima ili kujua afya yake na mtoto wake.
4. Kwa upande wa mtoto pale ikitokea Mama amejifungua mtoto huku mama ana Maambukizi mtoto anapaswa kuchukuliwa vipimo kama ifuatavyo, mtoto apimwe pale anapozaliwa, mtoto akiwa na umri wa miezi sita, pia akiwa na umri wa miezi tisa, miezi mitatu baada ya kuacha kunyonya na baada ya miezi kumi na minane, kutokana na vipimo vyote hivyo kama Mtoto hajagundulika na Maambukizi tunaweza kusema kuwa mtoto ni salama.
5. Kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwa jamii nzima ili kujua umuhimu wa kupima maambukizi ya HIV ili kuepuka kuambukiza watoto hambao hawana hatia na wakati wa kwenda kliniki kwa Mara ya kwanza wazazi wanapaswa kwenda wote kupima maambukizi ili kuepuka kumwambukiza mtoto.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Simulizi za Hadithi Audio ๐2 Kitabu cha Afya ๐3 Kitau cha Fiqh ๐4 web hosting ๐5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina ๐6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Zijue kazi za uke (vagina)
Uke ni sehemu ambayo imo ndani ya mwili wa mwanamke, sehemu hii ufanya kazi mbalimbali hasa wakati wa kujamiiana, kubarehe na kujifungua kwa mama.
Soma Zaidi...Mem mtoto ang almeza sumu yapanya ila tulimpa maziwa kwan inaweza leta madhara kwabaadae mana atukumpeleka hosptal
Maziwa ni mojakati ya vinywaji ambavyo ni dawa na hutumikakutoa huduma ya kwanza pale mtu anapomeza ama kula sumu. Huduma ya kwanza hii inaweza kuokoa maisha na wakati mwingine inaweza kuwa ndio dawa kabisa wala hakuna haja ya kufika Kituo cha afya.
Soma Zaidi...Mbinu za kuponyesha majeraha
Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo hutumika kuponyesha majeraha kwa haraka zaidi,tunajua majereha utokana na kupona kwa vile vidonda au kupona kwa sehemu ambayo imekuwa na majeraha kwa hiyo ili kuponyesha majeraha hayo tunapaswa kufanya yafuatayo.
Soma Zaidi...Zijue hasara za magonjwa ya ngono
Posti hii inahusu zaidi hasara za magonjwa ya ngono, ni magonjwa yanayoambukizwa kwa kujamiiana bila kutumia kinga.
Soma Zaidi...HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENGโATWA NA NYUKI
Kungโatwa na nyuki kunaweza kukahitaji huduma ya kwanza kwa haraka kama mgonjwa ana aleji na nyuki.
Soma Zaidi...