picha

Umuhimu wa kupima virus vya ukimwi kwa wajawazito na wanaonyonyesha

Post hii inahusu umuhimu wa kupima virus vya ukimwi kwa mama wajawazito na wanaonyonyesha. Ni hatua ya kupima Mama akiwa mjamzito na wakati wa kunyonyesha ili kuepuka hatari ya kumwambikiza mtoto

Umuhimu wa kupima virus vya ukimwi kwa mama mjamzito na wakati anaponyonyesha.

1. Tunajua wazi Mama akiwa mjamzito pale anapogundua kubwa ana mimba tu anapaswa kuja kliniki kupima maambukizi pamoja na mme wake, pengine Mama anaweza kuja kupima kwa Mara ya kwanza hasikutwe na virusi na akija kupimwa mara ya pili kabla ya kujifungua hasikutwe navyo lakini anaweza kuwa navyo kwa sababu ya kuwepo kwa hali mbalimbali vinaweza visionekane kwa hiyo anapaswa kupima tena akiwa ananyonyesha kwa sababu anaweza kupata ndani ya mda huo lengo ni kumzuia mtoto hasipatwe na Maambukizi.

 

2. Kwa kufanya vipimo vya marudio kwa mara tatu na wengine wanapima zaidi wakati wa ujauzito na kunyonyesha huweza kutambua hali ya Wazazi kwa ujumla na ikiwa Maambukizi yakiwepo  ni rahisi kuanza Dawa mapema ili kuweza kufuvaza makali ya virusi vya Ukimwi kwa ajili kuimarisha afya ya mzazi na kumkinga mtoto dhidi ya Maambukizi, lakini Mama hasipoanza dawa mapema anaweza kumwambikiza mtoto na mtoto akazaliwa na Maambukizi.

 

3.Pia kwa kutumia dawa hizi umsaidie kuzuia magonjwa nyemelezi kwa Mama na mtoto pia kama vile ugonjwa wa kifua kikuu, Malaria, Magonjwa ya ngozi kupungukiwa na kinga ambapo upelekea Mama kubwa na mkanda wa jeshi na magonjwa mengine mengi uweza kutokea kwa sababu ya kuwepo kwa kinga ndogo ya mwili kwa hiyo Mama kama hajapima ugonjwa wa VVU na kuona magonjwa Mengi anapaswa kwenda kupima ili kujua afya yake na mtoto wake.

 

4. Kwa upande wa mtoto pale ikitokea Mama amejifungua mtoto huku mama ana Maambukizi mtoto anapaswa kuchukuliwa vipimo kama ifuatavyo, mtoto apimwe pale anapozaliwa,  mtoto akiwa na umri wa miezi sita, pia akiwa na umri wa miezi tisa, miezi mitatu baada ya kuacha kunyonya na baada ya miezi kumi na minane, kutokana na vipimo vyote hivyo kama Mtoto hajagundulika na Maambukizi tunaweza kusema kuwa mtoto ni salama.

 

5. Kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwa jamii nzima ili kujua umuhimu wa kupima maambukizi ya HIV ili kuepuka kuambukiza watoto hambao hawana hatia na wakati wa kwenda kliniki kwa Mara ya kwanza wazazi wanapaswa kwenda wote kupima maambukizi ili kuepuka kumwambukiza mtoto.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/02/01/Tuesday - 05:12:49 pm Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 2981

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Mambo yanayoweza kudhoofisha kinga ya mwili

Kinga ya mwili inapodhoofu mwili unakuwa hatarini kupata maradhi. Je unayajuwa mambo yanayodhoofisha kinga ysbmeili?

Soma Zaidi...
Ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha

Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha hii ni chanjo wanayopewa watoto wadogo chini ya miaka mitano kwa lengo la kuzuia kuharisha chanjo hiyo kwa kitaalamu huitwa Rotarix.

Soma Zaidi...
Upungufu wa vyakula vya madini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula vya madini

Soma Zaidi...
Fahamu kuhsu vitamini E na kazi zake mwilini

Je unazijuwa faida za kuwa na vitamini E mwilini mwako.Unahani utapata matatizo yapi ya kiafya endapo utakuwa na upungufu wa vitamini E mwilini? Makala hii ni kwa ajili yako.

Soma Zaidi...
Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walio na majeraha ya macho.

Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa walio na majeraha ya macho kutokana na aina mbalimbali ya jeraha

Soma Zaidi...
Huduma ya kwanza kwa mtu aliyeshambuliwa na moyo na kushindwa kupumua

Kushambuliwa kwa moyo na kupumua ni kitendo Cha moyo kusimama ghafla, Hali hii unapaswa kutolewa huduma ya kwanza Ili moyo ufanye kazi tena,

Soma Zaidi...
Namna ambavyo mwili unapambana na maradhi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ambavyo mwili unapambana na maradhi

Soma Zaidi...
Madhara ya kutotibu magonjwa ya vidonda vya tumbo

Post hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu magonjwa ya vidonda vya tumbo, ni hatari inayotokea kwa mtu ambaye haujatibiwa vidonda vya tumbo.

Soma Zaidi...
Njia za kujikinga na UTI

Somo hili linakwenda kukuletea njia za kujikinga na UTI

Soma Zaidi...