Navigation Menu



image

Umuhimu wa uchumi katika uislamu

Post hii itakufundisha faida na umuhimu wa kijenga uchumi katika jamii ya kiislamu.

2. Umuhimu wa uchumi katika Uislamu
Mwanaadamu ameumbwa na mahitajio mengi ambayo hana budi kuyapata ili aweze kuishi kwa furaha na amani hapa ulimwenguni. Kwa kuwa mwanaadamu ni mchanganyiko wa mwili na roho, pia mahitajio yake yamegawanyika, ana mahitajio ya kiroho na kimwili. Mahitajio ya kiroho ambayo humuwezesha mwanaadamu kuishi maisha ya utulivu yenye furaha na amani, hupatikana kwa kufuata kwa utii na unyenyekevu mwongozo wa Allah (s.w).

 


Mahitajio ya kimwili kama vile chakula, mavazi, vipando na njia ya uchumi hupatikana kwa kuchapakazi chini ya mazingira yatokanayo na itikadi sahihi yenye kusimamiwa na viongozi wanaozingatia haki itokayo kwa Muumba. Katika Qur-an tunafahamishwa kuwa Allah (s.w) amejaalia mali anayoichuma mwanaadamu iwe ndiyo inayoboresha maisha yake: “Wala msiw ape w apumbavu mali zenu ambazo Mw enyezi Mungu amezijaalia kwa ajili ya maisha yenu …” (4:5)

 

Kutokana na aya hii, kuchuma mali si jambo la hiari kwa mwanaadamu kwani kwa namna Allah (s.w) alivyokadiria, maisha ya mwanaadamu kwa hapa ulimwenguni hayawezekani pasi na kuchuma. Ni kweli kwamba vitu vyote vilivyomzunguka mwanaadamu katika ulimwengu huu vimeumbwa kwa ajili yake kwa ushahidi wa Qur-an: “Yeye ndiye aliyekuumbieni vyote vilivyomo katika ardhi…” (2:29).

 


Lakini mara nyingi vitu hivi haviko katika hali ya kutumiwa na mwanaadamu moja kwa moja. Bali mwanaadamu analazimika kutumia elimu yake, Maarifa yake, juhudi zake na vipawa vyake vingine ili ayabadilishe mazingira yake yaweze kumtumikia na kukidhi haja zake.
Kwa mtazamo huu Uislamu unatuamrisha kuchuma kama unavyotuamrisha kusimamisha Swala, kutoa Zakat na kutekeleza Ibada nyingine maalumu kama hizi:

 

Na itakapokwisha swala, tawanyikeni katika ardhi mtafute fadhila za Mwenyezi Mungu na mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi, ili mpate kufaulu. (62:10)
Tunajifunza kutokana na aya hii kuwa, kuchuma ni wajibu unaompasa Muislamu mara tu baada ya kutekeleza Ibada maalum. Hili linabainishwa katika Hadithi ifuatayo:
“Abdullah bin Mus ’ud ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Kutafuta chumo la halali ni faradhi baada ya kutekeleza faradhi nyingine.” (Baihaqi).
Pia Mtume (s.a.w) amebainisha wazi ubora wa kujizatiti katika kutafuta chumo la halali kwenye Hadith ifuatayo:

 


“Miqdam bin Ma ’ad Yakrab ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Hapana mmoja wenu aliyekula chakula kizuri kuliko kile alichokula kutokana na kazi ya mkono wake mwenyewe. Na Daud, Mtume wa Allah, alikuwa anakula kutokana na kazi ya mikono yake.” (Bukhari)

 


Kwa upande mwingine Uislamu unalaani uvivu na kuwategemea wengine pasi na sababu au dharura maalum kama tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo:
“Jubair bin Awam ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Mmoja wenu kuchukua kamba na kisha akaja na mzigo wa kuni akiwa amebeba mgongoni mwake na akauuza, na kwakufanya hivyo Allah akailinda hadhi yake, ni bora kwake kuliko kuomba omba watu, wakimpa chochote au wasimpe (Bukhari.)

 


Mpaka hapo tumejifunza kuwa kwa mtazamo wa Uislamu, uchumi ndio msingi wa maisha ya mwanadamu hapa ulimwenguni na Uislamu umewajibisha kuchuma kwa kila mwenye uwezo. Ni makosa katika Uislamu mtu mwenye uwezo na afya kubweteka na kuwategemea wengine katika kukidhi mahitaji yake.

 






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1065


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Kufunga Mwezi wa ramadhani kisheria
Soma Zaidi...

Namna ya kuswali swala ya maiti: nguzo zake, sunnah zake na maandalizi juu ya maiti
3. Soma Zaidi...

Aina za swala..
Nguzo za uislamu,aina za swala (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Umuhimu na msisitizowa zakat na sadaqat katika uislamu
Nguzo za uislamu,umuhimu na msisitizowa zakat na sadaqat katika uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Ni watu gani wanaopewa Zaka
Soma Zaidi...

Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake. Soma Zaidi...

Kwanini funga imefaradhishwa mwezi wa ramadhani
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Usawa na uhuru wa kuchuma mali katika uislamu
Uchumi wa uislamu umeweka taratibu mbalimbali katika kuchuma mali. Soma Zaidi...

Nguzo za uislamu
Katika kipengele hiki tutajifunza nguzo za uislamu.aina tano za nguzo za uislamu,dhana ya nguzo za uislamu,lengo na umuhimu wa nguzo za uislamu Soma Zaidi...

Mambo yanayoweza kutoa udhu wako
Post hii itakufundisha mambo ambayo yanabatilisha udhu. Soma Zaidi...

Namna ya kutawadha yaani kuchukuwa udhu
Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu. Soma Zaidi...

Nguzo za swala ya maiti
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...