Post hii inahusu zaidi upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo dalili zake na namna ya kumsaidia mgonjwa mwenye tatizo hilo.
Upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo na dalili zake na jinsi ya kuzuia.
1. Upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo, utokea sana kwa watu wanaoishi sehemu za ziwani au kwenye majimaji mbalimbali na mnyoo huyo kwa kitaalamu huitwa Necatir Americans na Aina hii ya upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo huitwa Hookworms Anemea.
Dalili za mgonjwa wa Anemia inayosababishwa na minyoo.
-ukifunua kwenye jicho utakuta Kuna weupe na kiasi kidogo Cha damu kinachoonekana na kama damu Iko kidogo jicho uonekana jeupe kabisa na pia kwenye mikono huwa nyeupe kuliko kawaida na hivyo hivyo kwenye ulimi hali ya ulimi uwa nyeupe kuliko kawaida na midomoni hasa kwenye lips napi pia uwa peupe.
2. Mgonjwa wa kupungukiwa damu usikia uchovu, hii ni kwa sababu damu ndiyo inayohusika na kusafisha chakula pamoja na hewa ya oksijeni kwa hiyo vitu hivyo vikikosa mwilini na kuwepo kwa kiwango kidogo lazima mwili utakosa chakula na hewa itakuwa ndogo kwa hiyo mtu ataanza kusikia uchovu mara kwa mara na kushindwa kufanya kazi zake za kila siku hatimaye kama damu haitaongezewa haraka anaweza kuzimia .
3.Dalili za moyo kushindwa kufanya kazi ujitokeza.
Hii ni pamoja na mapigo ya moyo kubadilika yanaweza kwenda mbio kwa Sababu ya kutumia nguvu kusukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili kuliko kawaida kwa sababu damu haifiki sehemu zote na siyo ya kutosha kwa hiyo moyo utumia nguvu Ili kusfilisha damu kila mahali hali ambayo usababisha mishipa ya damu kupasuka na kusababisha madhara makubwa.
4. Kiasi Cha madini ya chuma kupungua.
Kama mtu ana upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo kiasi Cha madini ya chuma upungua kwa kiasi kikubwa kwenye damu hii ni kwa sababu ya kuwepo kwa minyoo kwenye mwili ambao usababisha kupungua kwa madini ya chuma.
5. Kupumua kwa shida.
Kupumua kwa shida utokea kwa sababu ya kutokuwepo kwa hewa ya kutosha kwenye damu, tukumbuke kuwa kazi ya damu ni kubeba hewa kutoka kwenye mapafu kwenda sehemu mbalimbali za mwili na kwa sababu ya maambukizi hewa haitoshi kwa hiyo lazima mgonjwa atapumua kwa shida kwa sababu ya kutokuwepo kwa hewa ya kutosha kwenye mwili.
6.Mapigo ya moyo upungua.
Kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi kwenye mwili na idadi ya damu kwenye mwili ni kidogo na mapigo ya moyo upungua kwa sababu ya kupungua kwa kiwango Cha damu mwilini.
Angalisho:tunajua kuwa damu ni muhimu mwilini na ikipungua ni hatari sana kwenye mwili kwa hiyo tuwe makini ikiwa damu itapungua kuliko kawaida na tule vyakula vya kuongeza damu na pia tutumie sana dawa za kuua minyoo inayosababishwa upungufu wa damu.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Ugonjwa wa degedege ni ugonjwa unaowapata sana watoto chini ya miaka mitano ingawa na watu wazima wanapatwa na ugonjwa huo
Soma Zaidi...Katika somo hili na yanayofuata utajifunz akuhusu ini. Post hii ina muendelezo wa post zinazofuat. Katika mfululizo huuutajifunz akuhusu ini na maradhi yake na kujiking nayo.
Soma Zaidi...posti hii inahusu dalili za Homa ya Manjano ni maambukizi ya virusi yanayoenezwa na aina fulani ya mbu. Maambukizi hayo ni ya kawaida zaidi na kuathiri wasafiri na wakazi wa maeneo hayo.
Soma Zaidi...Dalili za HIV zina utofauti na dalili za UKIMWI. Kwani HIV huwezakuonyesha dalili wiki ya pili hadi ya sita baada ya kuathirika kisha zinapotea, lakini dalili za UKIMWI huwezakutokea baada ya miaka 5 hadi 10.
Soma Zaidi...DALILI ZA MINYOO Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote.
Soma Zaidi...Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni.
Soma Zaidi...Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kujikinga na magonjwa, kwa kawaida tunajua wazi kuwa magonjwa yapo na yanasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na mengine hayasambai yanaweza kumpata mtu mmoja akapona au magonjwa mengine si ya kupona
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye milija (follapian tube) kwa kitaalamu huitwa salpingitis, ni maambukizi kwenye milija ambayo husababishwa na bakteria.
Soma Zaidi...