Upungufu wa homoni ya estrogen
Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni ya estrogen na dalili zake, aina hii ya homoni ikipungua mwilini uleta madhara na matatizo mbalimbali kwenye mwili.
Upungufu wa homoni ya estrogen na dalili zake.
1.aina hii ya mvurugiko wa homoni upo kwa wingi kwa wanawake wale waliofikia ukomo wa kujifungua hasa hasa kuanzia miaka thelathini na tano na kuendelea na hasa hasa wale waliofikia ukomo wa hedhi ambapo kwa kitaalamu huitwa menopause, kwa upande wa kimo wanawake wembamba uathiriwa zaidi kuliko wanawake wanene, zifuatazo ni dalili za mvurugiko wa homoni ya estrogen.
2. Kuwepo kwa ukavu ukeni.
Hii ni dalili Mojawapo inayowapata sana akina Mama wenye mvurugiko au upungufu wa homoni ya estrogen, kwenye uke kunakuwepo ukavu na hali hii usababisha maumivu au kutopelekea kufurahia kwa tendo la ndoa na sababu ya kukosa Ute Ute usababisha mikwaruzo kwenye uke.
3. Maumivu makali wakati wa kushiriki tendo la ndoa.
Kwa kawaida Ili mwanaume aweze kushiriki na kufurahia tendo la ndoa ni lazima maandalizi yawepo Ili kuweza kuwepo kwa Ute ambao usababisha uboo kupita kwa hiyo kama Ute haupo lazima mama atapata maumivu wakati wa kushiriki tendo la ndoa.
4. Kuwepo kwa homa za vipindi vipindi.
Kwa sababu ya kuwepo kwa upungufu au mvurugiko wa homoni ya estrogen na mwili nao pia uvurugika ambapo homa za vipindi utokea mara kwa mara hali ambayo usababisha mwili kutokuwa kwenye hali yake ya kawaida.
5. Kuvuja jasho wakati wa usiku.
Kwa sababu ya kuwepo kwa homa za vipindi usababisha Mama kuwa na jasho wakati wa usiku, hata kama Kuna baridi kiasi gani yeye mhusika uhisi joto wakati wa usiku.
6. Matatizo ya kupoteza kumbukumbu uweza kutokea.
Kwa sababu ya maumivu au mwli kupungukiwa kwa homoni muhimu ya estrogen uendana na tatizo la kupoteza kumbukumbu kwa hiyo utawakuta akina Mama wengi wenye umri wa kuingia menopause Wana shida ya kusahau sana hii ni kwa sababu ya kupoteza homoni ya estrogen.
7. Kujisikia mvivu na mzito hasa wakati wa kufanya kazi.
Kwa kawaida katika hali ya kupoteza homoni hii mama ujihisi ana uchovu wa mara kwa mara na mara nyingine uhisi mchovu wa mara kwa mara
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 web hosting 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Fahamu madhara ya Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke PID
Posti hii inazungumzia kuhusiana na mathara yanayosababisha Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke
Soma Zaidi...Uzazi wa mpango kwa njia ya kumwaga manii nje.
Posti hii inahusu zaidi uzazi wa mpango kwa njia ya kumwaga shahawa nje, hii ni njia mojawapo kati ya njia za uzazi wa mpango ambapo mwanaume humwaga nje mbegu ili asimpatie Mama mimba.
Soma Zaidi...Mimi imepita miezi mitatu sioni hedhi na wala sioni dalili ya kuwa na mimba unaweza ukaniambia tatizo la kuwa na hali hii
Kama na wewe una tatizo la kupitiliza siku zako za hedhi hli ya kuwa huna ujauzito, soma post hii ina majibu yako.
Soma Zaidi...Changamoto za ujauzito
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu changamoto za ujauzito na dalili zake endelevu
Soma Zaidi...Njia za kugundua kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa
Post hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo mtoa huduma anaweza kuzitumia kuangalia kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa.
Soma Zaidi...Je, mwanamke anapataje Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi PID?
Posti hii inaelezea namna mwanamke anavyoweza kupata Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi.
Soma Zaidi...