image

USALITI (sehemu ya tatu)

Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi.

Basi kama tulivyoona kwenye sehemu iliyopita kwamba Rhoda baada ya kuambiwa kwamba hakuna mwanamke mzuri duniani kama wewe alilia mno bila kunyamaza kama masaa matatu hivi na wakamwacha akalia hiyo ilikuwa ni dalili ya kuondoa maumivu yaliyompata, aliyemwambia maneno hayo alikuwa ameandaliwa kusudi amwambie ili kuona matokea au jinsi atakavyopokea neno hilo, wakaamua kuendesha gari huku Rhoda akilia mpaka nyumbani, baada ya kumaliza kulia alitumia siku nane bila kuongea na mtu yeyote  ila kwa siku hizo alikuwa na uwezo wa kuoga ,kufua ,kusafisha chumba chake na kufanya shughuli mbalimbali hapo nyumbani bila kuongea na mtu yeyote, na akaanza kuwasogelea hata watoto wa kiume kwa sababu hapo awali alikuwa hapendi kuona jinsia ya kiume na alianza kushiriki chakula na familia ila akiwa kimya.

 

Baada ya wataalamu wa saikolojia walikuja kuangalia maendeleo ya mgonjwa wao walikuta yuko kwenye hali ya usafi na alikuwa haongei,yule dada akavaa nguo alizokuwa anampenda kuvaa Rhoda akiwa bado yupo na akili nzuri,Rhoda alifurahi sana na yeye akavalishwa nguo ila akazivua akaenda nazo chumbani mwake akaoga akanawa akavaa na kupendeza basi wale wanasaikolojia wakamwambia apande kwenye gari akajipandisha mwenyewe wakaenda Rock City, walipofika pale akakutana na watu anaowafahamu akawasalimia wakaenda hotelini akaagiza chakula ambacho ni chips na kuku akakaa kwa heshima wakala akaanza kupiga story kama kawaida na walipomaliza kula wakaenda kwenye swimming pool akaogelea vizuri na ilipofika saa kumi na mbili akawaambia waondoke usiku umeingia.

 

Kabla hawajaingia kwenye gari aliwasihii wamnunulie nguo, alisema mda wote niliokaa nyumbani sikuwa na nguo kwa kuwa sasa nitaanza kutembea kwa watu naomba na mimi mnisaidie ni pate nguo nzuri, wakampigia baba simu wakamtaarifu kuhusu kinachoendelea baba alifurahi sana akatuma Hela ya kutosha wakampatia mwenyewe akaanza kununua alipomaliza akafunga vizuri akaweka kwenye gari wakaondoka akaomba mziki wakamwekea akaenda anaimba mpaka nyumbani, alipofika nyumbani akawasalimia, akamshukuru sana baba yake akachukua nguo akaenda kufua,akaoga na akaja kuongea na wanasaikolojia na walipotaka kuondoka akawasindikiza nje wakaenda na yeye akarudi ndani.

 

Kadri siku zilivyokuwa zinaenda akili yake ilirudi kabisa n mpaka sasa huyo dada yupo anaendelea na Kazi yake kwenye bank ila shida hapendi kutolewa , kwa hiyo wasomaji wote wa story hii ni ya ukweli kabisa na kama kuna mtu ambaye ameumizwa na tatizo lolote anione Ili kuweza kupata matibabu kutokana na wataalamu wa kisaikolojia, ila pia kutokana na story hii nawasihi sana watoto wa kike  kama mvulana au boyfriend wako ana mpango wa kukuoa na unaona Kuna nia kweli jaribu kujiwekea misimamo ya maisha kwa sababu Moses alimpenda Rhoda ila kwa sababu ya hali Ile ya kutoa mimba mara kwa mara ilimfanya  amwache kwa kuhofia kukosa watoto.

 

Vile vile na watoto wa kiume jaribu kuwa na huruma jamani hata kama msichana unaona hutaweza kumuoa usimwaribie maisha ,kama Moses angekuwa na moyo wa upendo na huruma kwa Rhoda pale walipobebeshana mimba wakiwa chuoni wangekubali kutunza hiyo mimba na kuendelea na masomo hatimaye baadae wangeoana, kwa sababu kitendo ambacho Moses alimfanyia Rhoda sio kizuri kwa sababu kimegharimu maisha yake na kufanya hata familia kutengwa na jamii,kwa hiyo inawezekana kitendo cha kumwacha Rhoda na kukimbilia mwanamke mwingine kwa wazo la kupata watoto inawezekana na kwa mwanamke aliyemuoa wasipate watoto kwa sababu damu ya zile mimba Bado unalia na pia Moses anapaswa kukumbuka machozi na mateso sliyoyapitia Rhoda ,kwa hiyo achana na tabia ya kuchezea maisha ya wenzenu miliojidai kwamba mnapendana.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 948


Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Hadithi katika kijiji cha burugo
Β Posti hii inahusu zaidi jinsi ya watu walivyoishi katika kijiji cha burugo .tunajuwa hadithi ni sehemu mojawapo ya kubirudisha na kujifunza kitu flani kutoka kwenye jamii . Soma Zaidi...

NIMLAUMU NANI part 1
Post hii inahusu hadithi Moja ya kijana maaalufu aliyeitwa Frank, ni kijana aliyekuwa mwaminifu ila amekumbana na wasichana wengi wanamasaliti ukizingatia Frank alikuwa kijana mstaalabu na mwaminifu sana ila anafikia kufanya maamuzi magumu kufuatana na ku Soma Zaidi...

Hadithi ya Mama mchoyo na mwehu
Posti hii inahusu zaidi habari za Mama mmoja aliyekuwa mchoyo akampa mkate mwehu na kuutia Sumu ila kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu sana aliutunza mkate na kuwapatia watoto wa yule mama waliokuwa wakitoka shule na njaa kali Soma Zaidi...

NIMLAUMU NANI (sehemu ya nne)
Post hii inahusu zaidi kijana Frank anayelazimishwa kuolewa na Amisa yeye hayuko tayari ila kwa sababu ya maisha kuwa magumu anaamua kulala na Amina na kumbebesha Mimba ya watoto mapacha. Soma Zaidi...

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, tunajua kuwa mama yake na binti alimtorisha yule binti mbali kabisa ila kijana naye aliamua kutoroka na kumfuata binti mfalme na hatimaye akampata alipo. Soma Zaidi...

NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tano)
Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya Nimlaumu nani ambapo juma anapanga na madaktari wanaopima DNA ili kuweza kutambua kwamba mtu mimba ni ya kwake na sio ya Frank kwa hiyo tuendelee kusikiliza mpaka tutakapoona mimba itakuwa ya Frank au juma. Soma Zaidi...

Kila kitu ambacho wanaume wanatakiwa kufahamu kuhusu wanawake.
Hii ni siri kubwa kuhusu wanawake. Hapa utajifunza jinsi ya kumfanya mwanamke asikuache. Soma Zaidi...

Mtoto wa tajiri na maskini (sehemu ya pili)
Post hii inahusu zaidi watoto wa wawili ambapo mmoja ni mtoto wa tajiri na mwingine ni mtoto wa maskini. Soma Zaidi...

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme (sehemu ya nne)
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya nne ni pale bibi anawachanganya kwa maneno yake yaani mke wa kwanza anaambiwa aandae malkia na mke mdogo atafute njia za kufanya kijana wake kuwa mfalme. Soma Zaidi...

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano, baada ya bibi kuachana na mke mdogo wa mfalme alienda kwa kijana wa kiume wa mfalme na kuona udhaifu wake kwamba anapenda sana mali. Soma Zaidi...

USALITI (sehemu ya tatu)
Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi. Soma Zaidi...

NIMLAUMU NANI (sehemu ya sita)
Post inahusu zaidi hadithi ya NIMLAUMU NANI ambayo ni sehemu ya sita, katika kipengele hiki tunaenda kumwona msichana Amina anapambana na hatimaye anafunga ndoa ya kiserikali na Frank Soma Zaidi...