Utaratibu wa kuzuru makaburi na dua zinazosomwa wakati wa kuzuru kaburi

Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika katika kuzuru kaburi la muislamu.

UTARATIBU NA DUA YA KUZURU MAKABURI

Kuzuru makaburi ni katika matendo ya sunah yaani unapata thawabu kwa kwenda klizuru kaburi. Ni katika matendo yanayotukumbusha kifo. Hata mtume allikuwa akienda kuzuru makaburi mara kadhaa. Hata mwishoni mwa siku za mwisho za uhai wake alikwenda kuzuru makaburi na kuwaaga waliokufa na kuwaombea dua.
 
 
 
Hapo mwanzo wanawake walikatazwa kuzuru makaburi kwa maneno ya Mtume aliposema “wamelaaniwa wanawake wenye kuzuru makaburi”. lakini baadaye mtume akawaruhusu wanawake kuzuru makaburi. Kwa ufupi ibada hii ni kwa waislamu wote na haina siku maalumu ama wakati maalumu. Kwani Mtume alikuwa anakwenda kuzuru makaburi hadi wakati wa usiku.
 
 
 
Kuzuru makaburi sio lakima uwe na udhu. Unaweza kuzuru hata ukiwa hupo twahara. Ukifika kwanza unaanza kusalimia (kutoa salamu) kisha unaomba dua pia ukiwa makaburini unaweza kulimia ama kusafishai kaburi ama makaburi. Ama kujazia udongo haya yote sio ya lazima. Kisha utaomba dua
 
 
 
Dua ya kuzuru kaburi
لسَّلامُ عَلَـيْكُمْ أَهْلَ الدِّيارِ مِنَ المؤْمِنيـنَ وَالْمُسْلِمينَ، وَإِنّا إِنْ شاءَ اللهُ بِكُـمْ لاحِقُـونَ، (وَيَرْحَمُ اللَّهُ الْمُسْتَقْدِمِينَ مِنَّا وَالْمُسْتَأْخِرِينَ) أَسْـاَلُ اللهَ لَنَـا وَلَكُـمْ العَـافِيَةَ.
 
Assalaamu ’alaykum ahlad-diyaar minal Mu-uminiyna wal Muslimiyn, wainnaa In Shaa Allaahu bikum laahiquwn. (Wa yarhamu-Allaahu al-mustaqdimiyna minnaa wal musta-akhiriyna). As-alu-Allaaha lanaa walakumul-’aafiyah
 
 
Amani ishuke juu yenu watu wa nyumba za Waumini na Waislamu, nasi apendapo Allaah tutakutana nanyi (Na Allaah Awarehemu wa mwanzo na wa mwisho). Namuomba Allaah Atupe sisi nanyi Al-’Aafiyah
al-hidaayah.com
 
 
Mwenye kuzuru makaburi anaruhusiwa kwenda akiwa peke yake ama akiwa na wenzie. Halikadhalika hakuna mavazi ya rangi maalumu wakati wa kuzuru ama kuzika. Hakuna haja ya kunyoa nywele wana kuandaa vyakula. Hairuusiwi kuyataja mabaya ya aliuyefariki ama kukaa juu ya kaburi. Pia hairuhusiwi kuzungumza mabo maovu maeneo ya makaburi.
 
 
Kwa hakika kuzuru makaburi ni ibada inayotaka utulivu wa nafsi. Kwani inatakikana moyo upate mawaidha kutokana na kutembelea kaburi. Mwenye kuzuru kaburi apate athari ya kuyaogopa mauti ili apate kufanya maandalizi.
 
 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1969

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

benki za kiislamu na njia zake za kuingiza kipato

Benki za KiislamuBenki za Kiislamu ambazo hutoa huduma kama benki nyingine zinaendeshwa katika msingi wa biashara na sio ule wa riba.

Soma Zaidi...
Miiko au Mambo yanayoharibu/kubatilisha funga

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Hukumu ya talaka iliyotolewa kabla ya tendo la ndoa

Endapo mtu atamuacha mke wake kabla hata ya kukutana kimwili, basi talaka hii itahukumiwa kwa namna hii.

Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo msafiri anatakiwa aswali akiwa safarini

Postvhiibinakwenda kukufundisha kuhusu swala ya msafiri na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Misingi ya fiqh

Kwenye kipengele hichi tutajifinza vyanzo mbalimbali vya sheria ua kiislamu.

Soma Zaidi...
Haki za raia katika dola ya kiislamu

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...