image

Viraa saba na herufi saba katika usomaji wa quran

Ni zipi hizo herufi saba, na ni vipi viraa saba katika usomaji wa Quran

Viraa saba na herufi saba.
Wataalamu wa tajwid wanaeleza kuhusu herufi saba za usomaji wa qurani. Itambulike kuwa qurani imeshuka kwa lugha ya kiarabu. Na pia itambulike kuwa waarabu wenyewe walitofautiana katika lahaja za lugha ya kiarabu. Lahaja hizi zilikuwa katika makabila saba ya kiarabu yaliyopo maka. Yaani ni kuwa waarabu walikuwa na makabila saba wakati ule. Na makabila haya ijapokuwa yalizungumza kiarabu lakini walikuwa wakitofautiana katika maneno, utamkaji na hata uandishi. Hivyo lahaja hizi zilijulikana kama herufi saba (za usomaji wa qurani).



Hivyo lahaja saba hizi ndizo chanzo za hizi herufi saba. Na hili linathibitika katika maneno ya Mtume (s.a.w) aliposema: ((Jibriyl alinisomea kwa herufi moja, nikaifanyia marudio mpaka akanifundisha nyingine, nikaendelea kumuomba nyinginezo mpaka mwishowe zikawa herufi (lahaja) saba)) (Bukhari na Ahmad).



Makabila haya yalikuwa Quraysh, Hudhayl, Thaqiyf, Hawaazin, Kinaanah, Tamiym na Yeman. Hivyo qurani ilishuka katika lahaja saba kulingana na makabila. Hivyo ikawa kila kabila linasoma qurani kwa namna ambavyo lahaja yao inawafanya waelewe. Wakawa watu wanaandika qurani kwa namna ambavyo wanaelewa wao. Kulingana na lahaja ya kabila lao. Hali hii ilifanya usomaji wa qurani utofautiaane. Mifano; “’alayhim” wengineo walitamka “’alayhimuw”, neno la “swiraatw” walitamka wengineo “zwiraatw” na wengine “siraatw”, “muumin” wengineo walitamka “muwmin” 



Amesimulia ‘Umar Ibn Al-khatab kuwa: “Nilimsikia Hishaam ibn Hakiym akisoma Suwratul-Furqaan tofuati na vile ninavyoisoma na alivyonifundisha Mtume ( لى لله عليه وسلم B). Nilikaribia kumsimamisha (asiswalishe) lakini nikamvumilia mpaka akamaliza kisha nikamshika nguo yake shingoni na kumvuta mpaka kwa Mtume لى لله عليه وسلم) B) nikasema: “Nimesikia huyu mtu akisoma (Suwratul- Furqaan) kinyume na ulivyonifundisha”. Mtume ( لى لله عليه وسلم B) akasema: ((Mwachie!)) Akamwambia (Hishaam): ((Soma)). Akasoma. Akasema ((Hivi ndivyo ilivyoteremshwa)). Kisha akaniambia mimi: ((Soma)). Nikasoma. Akasema: ((Hivi ndivyo ilivyoteremshwa. Hakika Qur-aan imeteremshwa kwa herufi saba, hivyo someni iliyokuwa sahali kwenu)



Uislamu ulipoenea zaidi ikawepo haja ya kuiandika qurani katika lahaja moja ambayo itasomwa. Na hii ni kutokana na kuwepo makosa katika usomaji wa qurani. Hivyo katika utawala Kikundi cha Maswahaba, kilichoongozwa na Hudhayfah bin al-Yamaaniy ambaye alikuwa Iraq, kilikuja kwa ‘Uthmaan ( رضي لله عنه ) na wakamsihi "auokoe ummah wa Kiislamu kabla haujatofautiana juu ya Quraan." ‘Uthmaan ( رضي لله عنه ) akaamrisha chini ya uongozi wa Zayd bin Thaabit رضي لله عنه) ) nakala za Qur-aan ziandikwe na nakala zote zisizo rasmi zichomwe moto.

 

Lahaja iliyotumika kuandika Qur-aan ni ile ya ki-Quraysh na Msahafu ukajulikana kuwa ni ‘Msahafu wa ‘Uthmaan’. Nakala hizo zilisambazwa miji mikuu ya Waislamu zikiwa kama nuskhah (kopi) rasmi. Na nuskhah ya asili ikabakishwa kwa Mama wa Waumini Hafswah ( رضي لله عنها ). Alimwacha Zayd bin Thaabit Madiynah, ‘Abdullaah bin Swaa’ib alitumwa Makkah,Mughiyrah bin Shu’bah alitumwa Syria, Abu ‘Abdir-Rahmaan As-Sulamy alitumwa Kuwfah, ‘Aamir bin ‘Abdil-Qays alitumwa Baswrah. (www.al-hidaayah.com)



Baada ya msahafu huu kusambazwa katika dola ya kiislamu lahaja zote ambazo siorasmi zilipotea. Msahafu huu ndio chimbuko la misahafu tulionayo leo. Ijapokuwa kuna tofauti kubwa za kiuandishi kati ya misahafu ya leo na msahafu huu. Kwa m fano msahafu huu haukuwa na dot kwenye herufi za dot au irabu pia hazikuwepo. Hayo yato yalifanyika baadaye kadiri uislamu ulipoenea maeneo mbalimbali ya dunia na ikaonekana ugumu wa kutumia msahafu ule kwa watu wasiokuwa waarabu.


Viraa saba.
Viraa hivi saba ndivyo ambavyo vimetokana na lahaja ya kikurayshi ambayo ndio msahafu wa ‘Uthmani umeandikiwa. Viraa hivi wataalamu wa elimu ya tajwid wamevizungumzia katika vitabu vya elimu hii.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1808


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Hukumu ya tafkhim na tarqiq katika usomaji wa Quran tajwid
Tarqiq ni kuisoma herufi kwa kuipa wepesi na tqfkhim ni kuisoma herufi kwa kuipa uzito. Soma Zaidi...

Je Qur-an ilikusanywa na kuandikwa katika msahafu wakati wa uongozi wa Abu-Bakr(r.a)
Je Qur-an ilikusanywa na kuandikwa katika msahafu wakati wa uongozi wa Abu-Bakr(r. Soma Zaidi...

Nini maana ya Iqlab katika hukumu za tajwid
Hapa utajifunza maana ya iqlab katika usomaji wa Quran kwa tajwid Soma Zaidi...

Dai kuwa Muhammad (s.a.w) aliitunga Qur-an ili Kuwania Madaraka na Ukubwa
(x) Dai kuwa Muhammad (s. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al bayyinah
Asbab nuzul surat al bayyinh. Sura hii imeteremka Madina na ina aya nane. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka Surat al Kafirun
Sura hii imekuja kukata rai ya Makafiri wa Makka kuhusu ibada ya ushirika. Hivi leo tungesema kuhusu dini mseto. Soma Zaidi...

Adabu za kusikiliza quran
ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI 1. Soma Zaidi...

Hukumu za Tajwid katika usomaji wa bismillah (basmalah)
Hapa utajifunza kanuni za tajwid katika kusoma bismillah au basmalah. Soma Zaidi...

Quran si maneno ya shetani
Soma Zaidi...

Kushuka na kuhifadhiwa kwa quran, hatua kwa hatua: mafunzo ya baadhi ya sura za quran
QUR’AN 5. Soma Zaidi...

HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Tafsiri na mafunzo ya sura zilizochaguliwa - Saratul-fiyl
Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...