Kutokana historia ya Nabii Daud (a.
Kutokana historia ya Nabii Daud (a.s) tunajifunza yafuatayo
(i) Katika kuchagua kiongozi wa kuendeleza harakati za kusimimisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuzingatia sifa nne za msingi zifuatazo:
(a) Elimu ya mwongozo na mazingira – (58:11)
(b) Ucha-Mungu-mwenye kujitahidi kufuata kwa unyenyekevu maamrisho ya Allah(s.w) na Mtume wake na kujitahidi hivyo hivyo kujiepusha na makatazo yao – Qur’an (49:13)
(c) Siha au Afya nzuri na ushupavu. Mtume(s.a.w)
amesema:
“Muumini mwenye afya nzuri (kawiyyu) ni bora zaidi kuliko muumini nyoronyoro (legelege).”
(d) Mwenye tabia njema – Pia Mtume (s..a.w) kasema;
“Aliye kipenzi changu kuliko wote katika nyinyi (Waislamu) ni yule aliyewazidi kwa tabia njema” (Al-Bukhari).
(ii) Utii kwa kiongozi muumini (mcha-mungu) ni msingi wa mafanikio kwa waislamu
(iii) Waumini wachache wenye msimamo na wenye kumtegemea Allah(s.w) wana uwezo wa kusimamisha haki (Uislamu) katika jamii.(2:249)
(iv)Tusitoe hukumu juu ya shutuma kabla hatujapata maelezo na kuyapima kutoka kwa yule anayeshutumu na anayeshutumiwa.
(v) Tushukuru neema na vipaji vya ziada alivyotutunukia Allah(s.w) na kuwa mstari wa mbele katika kusimamisha uadilifu katika jamii – Nabii Daud (a.s) alikuwa mfalme juu ya watu, milima, upepo na ndege, lakini hakutakabari.
(vi) Hatunabudi kuwaandalia maadui wa Uislamu silaha zinazolingana na wakati huu wa sayansi na teknologia – Nabii Daud(a.s)alitumia chuma kuandaa silaha na mavazi ya kivita – Pia rejea agizo la Allah(s.w) (8:60)
(vii) Hatunabudi kuwa na mazoezi ya kivita yatakayo tuwezesha kuwa jasiri na wavumilivu katika vita dhidi ya maadui wa Haki (Uislamu)
- Mfalme Twalut alilipa jeshi lake zoezi la kutokunywa maji ya mto ule ili kupima utii wao na uvumilivu wao.
Umeionaje Makala hii.. ?
MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena.
Soma Zaidi...Kutokana na kisa cha Nabii Shu’ayb(a.
Soma Zaidi...Mawaziri waliokuwa washauri wakuu wa Firauni wakataka wakusanywe magwiji waliobobea katika uchawi nchi nzima, kisha wapambanishwe na Nabii Musa(as).
Soma Zaidi...Kuanzishwa kwa Dola ya Kiislamu Madinah.
Soma Zaidi...Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Katika vita vya Uhudi waislamu walikufa wengi kulinganisha na makafiri. Lakini makafiri walikimbia uwanja wa vita baada ya kuzidiwa. Je ni nanibalishindwa vita vya Uhudi kati ya waislamu na makafiri?
Soma Zaidi...