Vyakula vya kuongeza damu
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula vya kuongeza damu
VYAKULA VYA KUONGEZA DAMU
Damu ni tishu iliyo katika kimiminika. Katika miili yetu damu ina kazi ya kusafirisha viinilishe na hewa ya oksijeni na kuondoa hewa chafu ya kabonidaiyoksaidi mwilini. Pia urekebishwaji wa joto na usafirishwaji wa homoni ndani ya mwili hutegemea damu. Kwa ufupi damu in akazi nyingi. Upungufu wowote wa damu mwilini unaweza kuleta athari nyingi mbaya za kiafya mwilini. Makala hii inakwenda kukueleza njia ya kuongeza damu kwa haraka.
Kazi za damu mwilini1.Kusafirisha viinilishe kutoka katika mfumo wa mmeng’enyo wa chakula kwenda maeneo mbalimbali ya mwili.2.Kusafirisha hewa ya oksijeni kutokakwenye mapafu kwenda maeneo mengine ya mwli.3.Kusafirisha hewa ya kabonikaiyoksaidi kutoka kwenye seli na kpeleka kwenye mapafu kwa ajili ya kutolewa nje4.Kudhibiti joto la mwili kwa kulipooza inapohitajika na kuliongeza inapohitajika5.Kusafirisha homoni kwenda maeneo mbalimbali ya mwili.
Vyakula vya kuongeza damu mwilini1.Nyama nyekundu kama nyama ya ng’ombe, mbuzi. Kondoo2.Maini3.Nyama ya figo4.Mboga za rangi ya kijani kama mchicha na apinachi5.Maharagwe6.Kunde7.Mayai8.Nafaka nyinginezo9.Njegere10.Koeosho na karanga11.Samaki12.Nyama ya ndege13.Karoti14.Matikiti15.Zabibu16.Viazi vitamu17.Matunda yenye uchachu kama machungwa, ndimu na limao.18.Polipili nyekundu
Dalili za kupungua kwa damu mwilini1.Uchovu wa hali ya juu2.Udhaifu wa mwili3.Ngozi kuwa na rangi ya njano au mauko4.Kupumua kwa shida5.Mapigo ya moyo kutokuwa ya kawaida6.Kizunguzungu na kichwa kuhisi chepesi7.Maumivu ya kifua8.Miguu na mikono kuwa ya ubaridi9.Maumivu ya kichwa
Sababu za upungufu wa damu mwilini1.Upungufu wa madini ya chuma mwilini2.Upungufu wa vitamini A na B-12 mwilini3.Maradhi kama HIV, UKIMWI, saratani, mardhi ya figo haya huweza kuleta upungufu wa damu4.Mfumo wa kinga mwilini kuuwa na kuharibu seli hai nyekundu (autoimmune)5.Uharibifu wa seli hai nyekundu kufanyika kwa haraka kuliko utengenezwaji.6.Kuwa na maradhi ya sickle cell
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Faida za kula viazi mbatata
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula viazi mbatata
Soma Zaidi...Umuhimu wa kula matunda na mboga mboga kila siku.
Mara nyingi tunasikia ushauri wa "kula matunda na mboga mboga," lakini je, umewahi kujiuliza kwa nini hii ni kanuni muhimu zaidi ya lishe bora? Vyakula hivi sio tu kwa ajili ya kuongeza ladha kwenye sahani yako; ni hazina ya virutubisho, viondoa sumu, na nguvu za kinga zinazouwezesha mwili wako kufanya kazi kwa ufanisi na kukuepusha na magonjwa sugu. Makala haya yanakupa sababu za msingi kwa nini unapaswa kuweka mboga na matunda kwenye kila mlo wako.
Soma Zaidi...Faida za kula fyulisi/peach
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula fyulisi/ peach
Soma Zaidi...Fahamu tiba ya lishe ya ugonjwa wa kisukari
Post hii inahusu zaidi tiba ya lishe ya ugonjwa wa kisukari ni tiba ambayo utumiwa sana na wagonjwa wa kisukari na walio wengi na wamefanikiwa kupona
Soma Zaidi...