Fahamu vitamini K na kazi zake, vyakula vya vitamini k na athari za upungufu wake

kuhusu vitamini K, wapi tutavipata, ni zipi athari zake na ni zipi kazi zake mwilini.

Fahamu vitamini K na kazi zake, vyakula vya vitamini k na athari za upungufu wake

VITAMIN K NA FAIDA ZAKE MWILINI

Vitamini K ni moja kati ya vitamini ambavyo miili yetu inavihitaji kwa ajili ya shughuli mbalimbali. Endapo upungufu wa vitamini hivi utatokea basi madhara makubwa ya kiafya yatamkumba mtu. Katika makala hii nimekuandalia somo hili ambalo litakwenda kuangalia zaidi kuhusu vitamini K, wapi tutavipata, ni zipi athari zake na ni zipi kazi zake.



YALIYOMO:

  1. Nini maana ya vitamini
  2. Vitamini K ni nini?
  3. Wapi nitapata vitamini K
  4. Ni zipi kazi za vitamin K
  5. Ni zipi athari za upungufu wa vitamini K
  6. Ni zipi athari za kuzidi kwa vitamin K


NINI MAANA YA VITAMINI?

Vitamini ni kampaudi ogania ambazo zinahitajika na mwili kwa ajili ya ukuaji wa mwili na utendaji wa michakato ya kibaiolojia ndani ya miili (metabolism), na ni viruubisho ambavyo havitengenezwi ndani ya miili yetu. Vitamini vipo katika makundi makuu mawili ambayo ni fat soluble na water soluble. Pia makundi ya vitamini ni A, B, C, D na K.



Fat soluble ni titamini ambavyo mwili unaweza kuvihifadhi kwa ajili ya matumizi ya baadaye vitamini hivi ni kama A, D, E na K. Hii ina maana hatuhitaji tule vyakula vyenye vitamin hivi kila siku. Watwer soluble ni vitamini ambavyo mwili hauwezi kuvihifadhi mwilini hivyo baada ya kula chakula mwili hufyonza kiasi cha vitamini hivi na kuvitumia. Hivyo tunahitajika tule vyakula vyenye vitamini hivi kila siku. Vitamini hivi ni kama D na C.



VITAMIN K NI NINI?

Hivi ni vitamini katika kundi la fat soluble ambavyo vimetokana na kampaundi za naphthoquinone. Vitamin hivi vimeitwa K, hii K asili yake ni neno la lugha ya Danish kutoka neno koagulation neno hili ukilileta kwenye lugha ya kiingereza unapata coagulation yaani kuganda. Hasa hapa kunazungumziwa kuganda kwa damu. Kwani vitamin K huhitajika mwilini katika kusaidia mchakato wa kuganda kwa damu pindi mtu anapopata jeraha.



Kwa mara ya kwanza vitamin K vimeanza kuletwa kwenye maandishi na mwanasayansi wa Danish mwaka 1929 Bwana Henrik Dam pindi alipokuwa akifanya tafiti juu ya kazi za Cholesterol kwenye mwili. Wataalamu wa lishe wameigawa vitamin K katika makundi ya K1 na K2. hivi vya K1 kitaalamu huitwa phytonadione huweza kupatikana kwenye mboga za majani na hivi vya K2 kitaalamu huitwa menaquinone hupatikana kwenye nyama, mayai na maziwa.


VYAKULA VYA VITAMIN K

Kama ulivyosoma hapo juu kuwa vitani K vipo katika makundi kma Vitamin K1 na vitamin K2 na pia umeona kwa ufupi vyanzo vya kila vitamini K. Sasa hapa nitakuorodheshea tena vyanzo vya vitamin K

Vitamin K1:

Vitamini hivi unaweza kuvipata kwenye mboga za majani za rangi ya kijani kama

  1. Mchicha
  2. Kabichi
  3. Spinach
  4. Kisamvu
  5. Mboga nyinginezo za majani
  6. Mapalachichi
  7. Zabibu
  8. Na matunda mengineyo


Vitamin K2

Hivi unaweza kuvipata kwenye;-

  1. Nyama
  2. Mayai
  3. Siagi
  4. Maziwa
  5. Na vyakula vinginevyo vya mfanano na hivi

KAZI ZA VITAMIN K MWILINI

Kama tulivyokwisha kuona maana ya K kweye vitamini K, sasa hebu tuone baadhi tu ya kazi za Vitamin hivi.

  1. Husaidia katika kuganda kwa damu
  2. Husaidia katika afya ya ubongo
  3. Husaidia katika kulinda afya ya mifupa
  4. Husaidia katika kuimarisha afya ya moyo
  5. Husaidia katika uthibiti wa matumizi ya madini ya calcium (chumvi) mwilini


  1. Kuganda kwa damu:

Hii ndiyo kazi kuu ya vitamin K, ni kuwa pindi unapopata jeraha lolote ambalo litapelekea damu kutoka, basi ili kuhakikisha damu haitoki zaidi katika jeraha lile,na hatimaye damu hukata, kazi hii yote hufanya na vitamin K hasahasa hapa tunazungumzia K1. vitamini K hutumika katika kutengeneza prothrombin, factors VII, IX, pamoja na X, kwa pamoja huitwa cloting factor na ndizo ambazo huhusika katika kusimamisha damu isiendelee kutoka kwenye jeraha. Upungufu wa vitamin K unaweza kusababisha damu kutokuganda ama utoka hata kama hakuna jeraha.



  1. Husaidia katika Afya ya Mifupa

Kuna ugonjwa unatambulika kama osteoporosis haya ni maradhi ya mifupa kuwa midhaifu, kuuma na kuweza kupasuka kwa urahisi sana. Mara nyingi maradhi haya yanawapata watu wenye umri wa kuanzia miaka 50, lakini pia unaweza kuwapata watu wenye chini ya hapo.

Wataalamu wa afya wanahusianisha upungufu wa vitamin K na kupata maradhi haya. Tafiti zinaonyesha kuwa vitamin K husaidia katika kuboresha afya ya mifupa, kuthibiti ujazo na tungamo la mifupa pia kuzuia mipasuko kwenye mifupa. Hatahivyo tafiti zaidi zinahitajika kuthibitisha zaidi.



  1. Afya ya ubongo na utunzaji wa kumbukumbu;

Tafiti zinahusisha uwezo wa kukumbuka na vitamin k. baadhi ya tafiti zilizofanywa zinaonyesha kuwa watu wenye umri wa zaidi ya 70 huwa uwezo wao wa kukumbuka unapungua, ila kwa wale ambao wana vitami K vya kutosha kwenye damu zao uwezo wao wa kukumbuka unakuwa mkubwa. Na hapa pia tunazungumzia sana vitamin K1.



  1. Kuboresha na kulinda afya ya moyo

Vitamin K husaidia katika kushusha presha ya damu kwa kuzuia kuganda kwa madini ndani ya mishipa ya damu. Hali hii huweza kusaidia moyo uweze kusukuma damu bila ya matatizo yeyote. Tafiti zinaonyesha kuwa kuwa na vitami K vya kutosha huzuia ama kupunguza athari za kupata stroke yaani kupalalaizi.



  1. Hulinda mwili dhidi ya kukuwa kwa seli za sartani.

Baadhi ya waandishi wanaeleza kuwa vitamin K huweza kusaidia kuondosha ama kulinda mwili zidi ya kupata vimbe za saratani. Lakini bado hakuna ushahidi wa kisayansi wa kutosheleza kuthibitisha madai haya.


ATHARI ZA VITAMIN K

Ijapokuwa vitamin K vinafida kubwa ndani ya miili yetu kama tulivyoona hapo juu. Basi pia itambulike kuwa vitamin K vikizidi zaidi ndani ya miili yetu vinaweza kusababisha madhara ya kiafya kama;-



Kama vitamin K itakuwa ni nyingi ndani ya mwili inaweza kupelekea athari kwenye figo. Pia inaweza kuhatarisha afya ya ini kama itatumika kwa kiwango kikubwa zaidi. Inaweza kuhatarisha ugandaji wa damu kwenye ini. Ni K vinaweza kushusha kiwango cha sukari hivyo kwa wenye kisukari itakuwa ni vyema akiwa chini ya uangalizi wa daktari kama anatumia dozi ya vitamin K.


UPUNGUFU WA VITAMIN K

Kama tulivyoona kazi za vitamin K katika miili yetu sasa hebu tuone ni zipi Athari za upungufu wa vitamin hivi ndani ya miili yetu

  1. Kuchelewa kuganda ama kusimama kwa damu katika jeraha ama kidonda
  2. Kutokwa na damu hata kama hakuna jeraha
  3. Ni rahisi kupata maradhi ya saratani (cancer)
  4. Ni rahisi kupata maradhi ya moyo
  5. Kupunguza hadira na misongo ya mawazo
  6. Kutoweza kuthibiti kumbukumbu
  7. Kuchoka kwa mifupa.

Mwisho

Vitamini K unaweza kuvipata kwa njia ya chakula ama kwa kumeza vidonge. Kwa wale ambao wana upungufu na vitamin unaweza kununua vidonge vya vitamin kwa kufuata maelekezo ya daktari. Usiwache kuwa nasi kwa kupata makala nyingine zaidi za afya hapa kwetu.



                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 936


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-