WAKATI WA KUFUMBUKA SEHEMU YA 2
Post hii ni mwendelezo wa hadithi ambayo Kwa jina inaitwa wakati wa Kufumbuka, ni mwendelezo wa pale maria anawekwa mbele ya wazee Ili akili kwamba John sio mtoto wa Mzee maganga ila maria akikumbuka wazi kwamba John ni mtoto wa Mzee maganga anakataa kuki
WAKATI WA KUFUMBUKA.
palikuwemo na mti mmoja uliyoitwa kwa jina la bwamahelu, mti huo ulikuwa mkubwa sana na ulisadikika kuwa Kuna mizimu ambayo usema ukweli hasa kwa mtu ambaye ni mwongo, na walikuwa na desturi kwamba wanaacha kula siku nzima na chakula kile wanakiwekea mizimu na wakikuta kimeliwa ni dalili wazi kwamba jambo walilokuwa wanahofia ni kweli ikiwa chakula kikikutwa ni kwamba jambo hilo sio la kweli,ila chakula hicho kililiwa na wazee hao endapo kama hawapendi mwenye tatizo ila kama wanampenda chakula walikikuta na kwa sababu kati ya watoto wa Mzee maganga Kuna mtoto alikuwa Bado anajifunza namna ya kuwahudumia mizimu kwa hiyo alijua kila kitu kilichokuwa kinaendelea na aliwajuza ndugu zake kinachoendelea.
Basi chakula kilipikwa vizuri na watu wote hawakuruhusiwa kula chochote wakiwa kwenye maandalizi ya kujua ukweli kuhusu mtoto John, basi na yule mtoto wa kiume aliyekuwa anajifunza namna ya kuwahudumia mizimu aliwaalika ndugu zake wawe makini Ili chakula kisiliwe wakiwa na na Nia za kumwokoa ndugu yao na pia kumwokoa mama yao, basi wale wazee walipoona kuwa nyama ni nzuri na zinavutia kwa macho wakazitamani Sana na kujiandaa kwa ajili ya kula, basi zilipowekwa wakaamua mtoto wa Mzee maganga aliyekuwa anajifunza kuhudumia mizimu atolewe wakdai kwamba ni kesi ya mama yake . Kwa sababu wazee walikuwa na nguo maalumu na sehemu hiyo illkuwa na giza Kuna mtoto mwingine wa Mzee maganga alivaa nguo za wazee bila kuonekana akaingia ndani ya mti penye chakula , wazee walipoonza kula na watu wapo huko nje wakidhani kwamba wazee wapo wanaongea na miungu kumbe wapo wanakula chakula.
Baada ya mda mrefu wazee walitoka na kwenda nje kwa mda wakidai kwamba miungu bado inakula na watu wakaendelea kusali, baada ya mda wale wazee warirudi kwenye pango na wakamwambia watu kwamba ni kweli John sio mtoto wa Mzee maganga na ndugu wakashangilia kwa sauti kubwa wakidai kwamba Mali alizonazo John anyanganywe,
Itaendelea
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 web hosting 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
USALITI (sehemu ya pili)
Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya Usaliti kati ya Rhoda na Moses ambapo Moses anampenda sana Rhoda na wakati wa kuoa umefika ila akagikilia kwamba akimuoa Rhoda inawezekana wasipate watoto kwa sababu ya mimba ambazo Rhoda alikuwa anatoa mara kwa mara.
Soma Zaidi...Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, baada ya kijana wa kiume wa binti mfalme kuoa yule ndugu yake baba anafanya sherehe kubwa na wake wenza wamepata habari kwamba kijana wa kiume wa mfalme ameoa ndugu yake wakaamuru kunyamaza il
Soma Zaidi...Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme (sehemu ya nne)
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya nne ni pale bibi anawachanganya kwa maneno yake yaani mke wa kwanza anaambiwa aandae malkia na mke mdogo atafute njia za kufanya kijana wake kuwa mfalme.
Soma Zaidi...Hadithi hii inahusu hasara za wivu na kutokuwa wazi
Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu, kwa sababu ya kuwepo kwa marafiki wasio waaminifu wanasababisha kuharibiana maisha bila kujua kwa sababu ya kuonekana wivu na kutokuwa wazi.
Soma Zaidi...USALITI (sehemu ya kwanza)
Post hii inahusu zaidi vijana wawili ambao ni msichana na mvulana walioingia kwenye mahusiano wakiwa sekondari na wakahaidiana kuoana ila kwa sababu mbalimbali walizokutana nazo kwenye safari yao ya mahusiano mmoja akamsaliti mwingine na kusababisha kupo
Soma Zaidi...Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi mafundisho ambayo tunayapata kutoka kwa binti mfalme, tunapotoa hadithi sio kusoma na kufurahia tu ila kuna mafundisho muhimu katika maisha yetu.
Soma Zaidi...