Walio kwenye hatari ya kupata Maambukizi kwenye mifupa
Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata Maambukizi kwenye mifupa,
Walio katika hatari ya kupata Maambukizi kwenye mifupa.
1. Waliopata ajali na kushambuliwa kwa mifupa.
Hawa waliopatwa na ajali na mifupa ikishambuliwa wapo kwenye hatari ya kupatwa na ugonjwa huu wa Maambukizi kwenye mifupa, kwa sababu wadudu au bakteria wakishaingia kwenye mifupa na wakakuta tayari kuna udhaifu fulani na pengine mgonjwa hakutibiwa vizuri ipasavyo hali ya kuwepo kwa Maambukizi inakuwepo kwa kiasi kikubwa , kwa hiyo mtu aliyepata ajali anapaswa kutibiwa vizuri na kujilinda mda wote hasipatwe na magonjwa yoyote.
2. Kuwepo kwa vyuma kwenye mfupa au kitu chochote ambacho kimo na hakipaswi kuwepo kwenye mifupa kwa kitaalamu tunaweza kusema foreign body, kwa Sababu vitu hivi sio mahali pake vilipo pengine vimekuwepo ili kusaidia kazi mbalimbali kwenye mwili kwa sababu ya udhaifu, kwa hiyo watu wenye vitu kama hivi wana asilimia kubwa kupatwa na Maambukizi kwenye mifupa kwa hiyo wanapaswa kuwa makini ili kuepuka na maambuy kwenye mifupa .
3. Kushuka kwa kinga ya mwili.
Tunajua wazi kuwa kinga ya mwili ikishuka usababisha magonjwa mengi kuwepo kwa hiyo watu wale ambao kinga zao za mwili zimeshuka wanapaswa kuwa makini na kuhakikisha wanajikinga na ugonjwa huu wa Maambukizi kwenye mifupa, kwa hiyo wale walio na magonjwa yanayopunguza kinga ya mwili kama vile HIV na mengineyo wahakikishe kuwa wanatumia dawa ili kuweza kuweka kinga yao sawa na kuepuka ugonjwa huu wa Maambukizi kwenye mifupa.
4. Wenye umri mkubwa nao wana hatari ya kupata ugonjwa wa Maambukizi kwenye mifupa.
Tunajua kubwa umri ukiongezeka na baadhi ya viungo vinapungua kufanya kazi kwa hiyo wale wenye umri mkubwa ute ute uisha kwenye mifupa na baadhi yao mifupa uanza kuuma kwa hiyo kiasi cha kushambuliwa na bakteria inakuwa kubwa, kwa hiyo wenye umri mkubwa wanapaswa kula vyakula vya kuongeza ute ute kwenye mifupa na kula vyakula vya kuongeza kinga mwilini.
5. Kwa hiyo tukumbuke kwamba ugonjwa huu ukitibiwa mapema unatibika na pia tuwe na utaratibu wa kwenda hospitali mara baada ya kusikia mabadiliko kwenye mwili na tunaweza kupunguza magonjwa mengine ambayo ni nyemelezi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Maumivu ya shingo na mabega kutokana na kazi za ofisini.
Msongo wa mawazo (stress) ni hali ya kawaida ya kisaikolojia na kimwili inayotokana na shinikizo la maisha. Ingawa kiasi kidogo cha msongo kinaweza kuchochea ubunifu na utendaji, msongo wa muda mrefu ni hatari kwa afya ya mwili na akili. Makala haya yanachunguza kwa kina dalili za msongo wa mawazo—kuanzia mabadiliko ya kihisia, kimwili, hadi kitabia—pamoja na mikakati ya kitaalamu ya kuyatambua na kuyadhibiti mapema ili kuzuia madhara ya kudumu.
Soma Zaidi...Athari za ugonjwa wa Homa ya inni
Posti hii inahusu zaidi adhari za ugonjwa wa Homa ya inni, hizi ni athari ambazo zinaweza kutokea ikiwa ugonjwa huu wa inni haujatibiwa, zifuatazo ni athari za ugonjwa wa inni
Soma Zaidi...Kiungulia, dawa yake na namna ya kuzuia kiungulia
Tambuwa kiungulia, sababu zake, dawa za kiungulia na namna ya kupambana na kiungulia
Soma Zaidi...Tofauti kati ya msongo wa mawazo na unyogovu (Depression).
Watu wengi hutumia maneno "msongo wa mawazo" na "unyogovu" kwa kubadilishana, wakidhani ni hali moja. Hata hivyo, kisaikolojia na kimatibabu, hizi ni hali mbili tofauti zenye visababishi, dalili, na mbinu za utatuzi zinazotofautiana. Makala hii inafafanua tofauti za kimsingi kati ya msongo wa mawazo (stress) na unyogovu (depression), jinsi ya kuzitambua, na hatua za kuchukua ili kudhibiti afya yako ya akili.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa Malengelenge sehemu za siri
Malengelenge sehemu za siri ni maambukizi ya kawaida ya zinaa ambayo huathiri wanaume na wanawake. Makala ya malengelenge sehemu za siri ni pamoja na maumivu, kuwasha na vidonda katika sehemu yako ya uzazi. Lakini huenda usiwe na dalili au ishara za mal
Soma Zaidi...