Walio kwenye hatari ya kupata Maambukizi kwenye mifupa
Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata Maambukizi kwenye mifupa,
Walio katika hatari ya kupata Maambukizi kwenye mifupa.
1. Waliopata ajali na kushambuliwa kwa mifupa.
Hawa waliopatwa na ajali na mifupa ikishambuliwa wapo kwenye hatari ya kupatwa na ugonjwa huu wa Maambukizi kwenye mifupa, kwa sababu wadudu au bakteria wakishaingia kwenye mifupa na wakakuta tayari kuna udhaifu fulani na pengine mgonjwa hakutibiwa vizuri ipasavyo hali ya kuwepo kwa Maambukizi inakuwepo kwa kiasi kikubwa , kwa hiyo mtu aliyepata ajali anapaswa kutibiwa vizuri na kujilinda mda wote hasipatwe na magonjwa yoyote.
2. Kuwepo kwa vyuma kwenye mfupa au kitu chochote ambacho kimo na hakipaswi kuwepo kwenye mifupa kwa kitaalamu tunaweza kusema foreign body, kwa Sababu vitu hivi sio mahali pake vilipo pengine vimekuwepo ili kusaidia kazi mbalimbali kwenye mwili kwa sababu ya udhaifu, kwa hiyo watu wenye vitu kama hivi wana asilimia kubwa kupatwa na Maambukizi kwenye mifupa kwa hiyo wanapaswa kuwa makini ili kuepuka na maambuy kwenye mifupa .
3. Kushuka kwa kinga ya mwili.
Tunajua wazi kuwa kinga ya mwili ikishuka usababisha magonjwa mengi kuwepo kwa hiyo watu wale ambao kinga zao za mwili zimeshuka wanapaswa kuwa makini na kuhakikisha wanajikinga na ugonjwa huu wa Maambukizi kwenye mifupa, kwa hiyo wale walio na magonjwa yanayopunguza kinga ya mwili kama vile HIV na mengineyo wahakikishe kuwa wanatumia dawa ili kuweza kuweka kinga yao sawa na kuepuka ugonjwa huu wa Maambukizi kwenye mifupa.
4. Wenye umri mkubwa nao wana hatari ya kupata ugonjwa wa Maambukizi kwenye mifupa.
Tunajua kubwa umri ukiongezeka na baadhi ya viungo vinapungua kufanya kazi kwa hiyo wale wenye umri mkubwa ute ute uisha kwenye mifupa na baadhi yao mifupa uanza kuuma kwa hiyo kiasi cha kushambuliwa na bakteria inakuwa kubwa, kwa hiyo wenye umri mkubwa wanapaswa kula vyakula vya kuongeza ute ute kwenye mifupa na kula vyakula vya kuongeza kinga mwilini.
5. Kwa hiyo tukumbuke kwamba ugonjwa huu ukitibiwa mapema unatibika na pia tuwe na utaratibu wa kwenda hospitali mara baada ya kusikia mabadiliko kwenye mwili na tunaweza kupunguza magonjwa mengine ambayo ni nyemelezi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 ai web app ๐2 Kitau cha Fiqh ๐3 Simulizi za Hadithi Audio ๐4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) ๐5 kitabu cha Simulizi ๐6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Dalilili za kukosa oksijeni
Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalilili za kukosa oksijeni ambalo kitaalamu hujulikana Kama apnea.kukosa oksijeni ni tatizo ambapo kupumua kwako hukoma na kuanza unapolala.
Soma Zaidi...Madhara ya gonorrhea endapo haitotibiwa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya gonorrhea endapo haitotibiwa
Soma Zaidi...Homa ya matone (Mumps): Dalili na tiba yake.
Homa ya matone, inayojulikana kama Mumps, ni maambukizi ya virusi yanayoathiri tezi zinazozalisha mate (salivary glands), hasa tezi zilizopo pande zote mbili za shavu (tezi za parotidi). Ugonjwa huu huambukiza kwa urahisi kupitia matone ya maji yanayotoka unapopiga chafya, kukohoa, au kuzungumza. Ingawa kwa sasa ni nadra kutokana na chanjo, bado inaweza kuwapata watu ambao hawajapata chanjo hiyo. Makala haya yanakupa uelewa wa dalili zake na jinsi ya kutoa huduma ya kwanza.
Soma Zaidi...Shida ya kifua kubana inaweza kuwa dalili ya maambukizi ya ukimwi
Kubana kwa kifuwa ni katika hali ambazo si naweza kuhatarisha maisha. Huwenda kuwa ni miongoni mwa dalili za magonjwa mengi. Je unadhani na HIv na UKIMWI ni moja ya magonjwa hayo?
Soma Zaidi...Dalili za kwanza za ugonjwa wa kaswende na kisonono.
Kaswende (Syphilis) na Kisonono (Gonorrhea) ni magonjwa ya zinaa (STIs) yanayoambukizwa kupitia tendo la ndoa. Ingawa husababishwa na vimelea tofautiโKaswende (bakteria Treponema pallidum) na Kisonono (bakteria Neisseria gonorrhoeae)โyote yanaweza kusababisha madhara makubwa mwilini ikiwa hayatatibiwa mapema. Makala hii inaangazia dalili zao za awali ambazo mtu yeyote anayeshiriki ngono anapaswa kuzifahamu.
Soma Zaidi...Dalilili zinazotokea kwenye mrija wa mkojo
Mrija wa mkojo hutoa mkojo nje ya mwili lakini mrija huu unapoziba hufanya utoaji wa mkojo kutoka kwa shida au maumivu
Soma Zaidi...