WATU HAWA HURUHUSIWI KUWAOA KATIKA UISLAMU


image


Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa.


Umaharimu

Maharimu ni wanawake na wanaume walioharamishwa kuoana kutokana na ukaribu wa nasaba kama ilivyobainishwa katika Qur-an na Sunnah. Wanaume wa Kiislamu wameharamishiwa kuwaoa wanawake wanaobainishwa katika aya zifuatazo:

 

Wala msiwaoe wake waliowaoa baba zenu; isipokuwa yale yaliyokwishapita. Bila shaka jambo hili ni uovu na chukizo na ni njia mbaya (kabisa). Mmeharamishiwa (kuoa) mama zenu, watoto wenu, dada zenu, shangazi zenu, ndugu za mama zenu, watoto wa ndugu zenu, watoto wa dada zenu, na mama zenu waliowanyonyesheni, na dada zenu wa kunyonya, na mama wa wake zenu, na watoto wenu wa kambo walio katika ulinzi wenu, walio zaliwa na wake zenu mliowaingilia. Lakini kama nyinyi hamjawaingilia basi si vibaya kwenu (kuwaoa). Na mmeharamishiwa wake wa watoto wenu waliotoka katika migongo yenu. Na (mmeharamishiwa) kuwaoa madada wawili wakati mmoja, isipokuwa yale yaliyokwisha pita. Hakika Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kurehemu na Mwenye kusamehe. (4:22-23)

 

"Na pia mmeharamishiwa wanawake wenye (waume zao) isipokuwa wale iliyowamiliki mikono yenu ya kuume. Ndiyo Sheria ya Mwenyezi Mungu juu yenu. Na mmehalalishiwa (kuoa wanawake) minghairiya hawa..." (4:-24)

 


Aya hizi zinabainisha wanawake walioharamishwa kuwaoa kuwa ni hawa wafuatao:
1.Mwanamke aliyepata kuolewa na baba yako, (babu yako, baba wa baba yako - wa kuumeni na kikeni).
2.Mama aliyekuzaa (babu aliyezaa waliokuzaa, mama wa bibi aliyezaa aliokuzaa...).
3.Binti yako uliyemzaa (au binti aliyezaliwa na uliyemzaa...). Pia binti wa kunyonya na mwanao (na kikazi chake...).
4.Dada yako khalisa au wa kwa baba au wa kwa mama.
5.Shangazi yako- dada wa baba yako,(na dada wa babu yako...).
6.Mama mdogo; ndugu wa mama yako (au ndugu wa bibi yako...).
7.Binti wa ndugu yako mwanamume, khalisa au wa kwa baba au kwa mama (na kila aliyezaliwa naye).
8.Binti wa dada yako khalisa au wa kwa baba au kwa mama


9.Mama wa kukunyonyesha (na mama zake wa kumzaa au wa kumnyonyesha).
1O.Dada yako wa kunyonya naye (aliyenyonyeshwa na aliyekunyonyesha).


11 .Mama yake mkeo wa kumzaa au wa kumnyonyesha (na bibi yake pia wa kumzaa mama yake au wa kumnyonyesha Ama ndugu yake mama yake mkeo yaani mama mdogo wake au shangazi yake wa kuzaliwa au kunyonya; unaweza kumuoa akifa mkeo au utakapomuacha na eda ikaisha.
12.Binti wa mkeo uliyemuingilia (na mjukuu wake...).


13.Mke aliyeolewa na mwanao wa kumzaa au wa kunyonyeshwa na mkeo (na kizazi chake); si mke wa mtoto wa kupanga au mtoto wa kulea.


14.Mtu na ndugu yake pamoja (au) mtu na shangazi yake au mtu na mama yake mdogo pamoja. Akifa mke au ukimuacha na eda ikaisha unaweza kumuoa dada yake, au shangazi yake, au mama yake mdogo.


15.Mke wa mtu, bado mwenyewe hajafa wala hajamuacha ni Haram kumuoa. Wanawake hao wameharamishwa kuolewa na wanaume wanaofanana na hawa kwa upande wa kiumeni.


 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    2 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    3 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    4 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    5 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    6 Magonjwa na afya    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Swala ya kuomba mvua swalat istiqaa na jinsi ya kuiswali.
Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kujitwaharisha Najisi hafifu na najisi ndogo
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi hafifu na najisi ndogo. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kutoa zakat al fitiri na umuhimu wa zakat al fitri kwa waislamu
Hapa utajifunza kuhusu zakat al fitiri, kiwango chake, watu wanaostahili kupewa na kutoa, pia umuhimu wake katika jamii. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake
Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

image Mambo muhimu ya kuzingatia katika kujenga uchumi wa kiislamu
Nazingatio muhimu katika uchumi unaofuata sheria za kiislamu. Soma Zaidi...

image Vipi utapata uchamungu kupitia funga
Vipi lengo la funga litafikiwa na kumfanya mfungaji awe mchamungu. Soma Zaidi...

image Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu
Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako. Soma Zaidi...

image Mambo anayofanyiwa mtu anayekaribia kufa
Haya ni maandalizi anayofanyiwa mtu aliye katika kilevi cha kifo yaani sakaratul maut Soma Zaidi...

image Sera ya uchumi katika uislamu
Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu. Soma Zaidi...

image Hadathi ya kati na kati
Posti hiibinakwenda kukufundisha kuhusu hadathi ya kati na kati. Soma Zaidi...