Yajue malengo ya kusafisha vidonda.
Posti hii inahusu zaidi malengo ya kusafisha vidonda, kwa sababu Kuna watu wengine huwa wanajiuliza kwa nini nisafishe kidonda hospitalini au kwenye kituo chochote Cha afya, yafuatayo ni majibu ya kwa Nini nisafishe kidonda.
Malengo ya kusafisha vidonda.
1. Kulinda kidonda kutokana na Maambukizi ya wadudu mbalimbali, tukumbuke kuwa vidonda vingine ni visafi na having wadudu kwa hiyo Ili kufanya kidonda kipone haraka ni kukisafisha Ili kiweze kutoingiliwa na wadudu na kuongeza maambukizi zaidi.
2. Tunasafisha vidonda Ili kuondoa unyevunyevu na kuondoa tisu zilizoharibika, kwenye vidonda uwa Kuna tisu zilizoharibika na kwa kawaida huwa ni nyeusi kwa rangi kwa hiyo tunapaswa kuondoa hizo tisu Ili zisijeendelea kuleta maambukizi zaidi na pia tunatoa unyevunyevu ambao unaweza kuwa chanzo Cha maambukizi mapya. In Kwa hiyo tunajua kuwa kuwepo kwa unyevunyevu kwenye sehemu ya kidonda na kuongezeka kwa maambukizi mapya.
3.Tunasafisha vidonda Ili tuweze kufunga vizuri sehemu mbalimbali zilizoharibika na kuifanya sehemu hiyo iweze kukaa kwenye hali inayoitajika kwa hiyo kwa wale wenye vidonda ni vizuri kusafisha kidonda kwenye sehemu za hospitalin na vituo mbalimbali vya afya Ili kuweza kuweka kidonda chako kwenye hali inayostahili hii usababisha kupona kidonda kwa haraka kuliko kawaida, kwa hiyo wote wenye vidonda nenda vituo vya afya mkapewa maelekezo zaidi.
4.Tunasafisha vidonda Ili kuongeza kiwango Cha vidonda kupona kwa haraka, ikiwa vidonda vimesafishwa kwa mda mwafaka na kw wakati bila kupitia sehemu mbalimbali ambazo usababisha ugonjwa kutopona vidonda upona haraka hata kama kina ukubwa kiasi gani, kwa hiyo kidonda kukisafishwa upona haraka, kwa hiyo wale wote wenye vidonda ambavyo mnaona ni vikubwa au vidogo vipelekwe hospitalini haraka Ili visafishwe na viweze kupona haraka.
5. Tunasafisha vidonda Ili kuweka pressure kwenye kidonda na hapo tutaweza kuzuia kuvuja kwa kidonda kwa hiyo kama Kuna kidonda pengine uwa Kuna damu kwa kusafisha kidonda tunaweza kupunguza kuvuja kwa kidonda na kusababisha kupunguza kiwango Cha damu mwilini.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 web hosting 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Huduma ya kanza kwa mgonjwa mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo
Posti hii inahusu zaidi huduma ya kwanza ya mgonjwa mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo, ni Tiba ambayo utolewa kulingana na dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Kazi za wahudumu wa afya wakati wa kutoa dawa kwa wagojwa
Hii post inahusu zaidi kazi za wahudumu wa afya wakati wa kutoa dawa, ni kanuni zinazopaswa kufuata wakati wa kutoa dawa kwa wagojwa.
Soma Zaidi...Hizi ni kazi za mapafu mwilini
Makala hii itakwenda kukufundisha kazi 5 za maafu mwilimi. Wengi tunajuwa tu kuwa mapafu yanafanya kazi ya kupumuwa. ila si hivyo tu yapo mengi zaidi.
Soma Zaidi...Kuboresha afya
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mambo yanayosaidia kuboresha afya
Soma Zaidi...Namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa
Posti hii inahusu namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa,ni njia unazopaswa kufuata wakati unamsafisha mgonjwa kinywa hasa wale walio mahututi.
Soma Zaidi...Namna ya kuwasaidia wagonjwa wa vidonda vya tumbo
Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia wagonjwa wa vidonda vya tumbo, ni njia ya kuwasaidia wagonjwa waliopata madonda ya tumbo
Soma Zaidi...