Posti hii inahusu zaidi sifa ambazo mtoto mchanga anapaswa kuwa Nazo,ni sifa ambazo lazima zionekane kwa mtoto mchanga pale anapozaliwa na zikikosa ni lazima kuja kuwa mtoto ana matatizo mbalimbali kwa hiyo zifuatazo ni sifa za mtoto mchanga kama ifuatavy
1. Mwonekano mzima wa mtoto.
Kwanza kabisa mtoto anapaswa kuwa na uzito kuanzia mbili na nukta tano mpaka tatu na nukta tano na kwa kawaida urefu wa mtoto ni kuanzia hamsini sentimita, na rangi ya mtoto anapozaliwa ni rangi ya pinkie, kwa hiyo mtoto akiwa na uzito chini ya mbili na nukta tano anakuwa kwenye uangalizi kwa mda na pia akiwa na uzito kuanzia tatu na nukta tano na kuendelea tunasema kwamba ni mtoto aliyezidi kwa uzito kwa hiyo naye huwa kwenye uangalizi maalumu kwa mda na baadae anaweza kuruhusiwa na kuwa kwenye uangalizi wa wazazi.
2.Watoto waliochini ya uzito au juu ya uzito uwa kwenye uangalizi kwa sababu, zifuatazo.
Mwenye uzito mkubwa anaweza kuwa amezoea vyakula vya kutosha kutoka kwa Mama yake akiwa tumboni akizaliwa tu anapaswa kuhudumiwa mapema na kupewa glucose Ili kulinganisha na chakula alichokuwa anakipata akiwa tumboni kwa hiyo akicheleweshwa anaweza kushuka kwa sukari. Na pia mtoto akizaliwa na uzito mdogo anapaswa kuangaliwa kwa sababu ya kupata uzito unaotakiwa kwa kihakikisha kuwa Mama yake anapewa elimu ya kumtunza mtoto mpaka akafikia kuwa na uzito unaotakiwa.
3. Pia mtoto akizaliwa anapaswa kuwa na kitovu kilicho kwenye tumbo na kinatakiwa kukatwa kwa uangalizi unaofaa Ili kuweza kuzuia maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto, pia na Mama anapaswa kupewa elimu kuhusu namna ya kumtunza kitovu cha mtoto wafundishwe kuwa kitovu cha mtoto kinakauka baada ya siku kumi, pia akina Mama wanapaswa kukumbushwa kuwa waachane na tabia ya kuweka vitu visivyofaa kwenye kitovu kwa kufuata mila na desturi zao hali inayosababisha kuwepo kwa tetunus kwenye kitovu kikitunzwa visivyo.
4. Pia kitu kingine ambacho ni sifa ya mtoto ni kulia tu baada ya kuzaliwa hii ikiwa ni ishara ya uhai kwa mtoto,kwa hiyo mtoto asipolia wauguzi na wasaidizi wote wanapaswa kihakikisha mtoto analia kwa kutoa huduma ya kwanza kwa mtoto na walio wengi wanafanyiwa na wanapona na kuendelea kwenye hali ya kawaida
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Tezidume ni moja ya magonjwa hayari yanayotokea katika mwili wa mwanaume.Hapa nimekuandalia sababu za kutokea kwa tezi dume.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na huduma kwa mama wajawazito na waliojifungua.
Soma Zaidi...Mimba haipatikani kila siku, na pia mimba huingia kwa siku moja na katika muda mmoja. Baada ya mimba kutungwa hakuna tena nafasi ya kutungwa mimba nyingine.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza njia za kuhakiki Kama u-mjamzito
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni ya estrogen na dalili zake, aina hii ya homoni ikipungua mwilini uleta madhara na matatizo mbalimbali kwenye mwili.
Soma Zaidi...Inaweza kutokea ukapima mimbaikawa ipo, na baada ya wiki kadhaa unapima tena haipo. Hali hii unadhani inaweza kusababishwa na nini?
Soma Zaidi...Inatakiwa angalau nafasivkati ya mtoto na mtoto wapishane miaka miwili.
Soma Zaidi...Hii ni hali inayowapata wanaume kushindwa kuhimili tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Hali ya ujauzito huanza kutabirika Mara tu ya kujamiana, pia chemikali (hormon) za mwili huanza mchakato wa kuongeza na kupunguza utendaji kazi wa kemikali hizo mfano.follical stimulating hormon (FSH) na lutenazing hormon kuivisha yai tayari kwa kutengen
Soma Zaidi...