Zifahamu sifa za mtoto mchanga.
Posti hii inahusu zaidi sifa ambazo mtoto mchanga anapaswa kuwa Nazo,ni sifa ambazo lazima zionekane kwa mtoto mchanga pale anapozaliwa na zikikosa ni lazima kuja kuwa mtoto ana matatizo mbalimbali kwa hiyo zifuatazo ni sifa za mtoto mchanga kama ifuatavy
Sifa za mtoto mchanga.
1. Mwonekano mzima wa mtoto.
Kwanza kabisa mtoto anapaswa kuwa na uzito kuanzia mbili na nukta tano mpaka tatu na nukta tano na kwa kawaida urefu wa mtoto ni kuanzia hamsini sentimita, na rangi ya mtoto anapozaliwa ni rangi ya pinkie, kwa hiyo mtoto akiwa na uzito chini ya mbili na nukta tano anakuwa kwenye uangalizi kwa mda na pia akiwa na uzito kuanzia tatu na nukta tano na kuendelea tunasema kwamba ni mtoto aliyezidi kwa uzito kwa hiyo naye huwa kwenye uangalizi maalumu kwa mda na baadae anaweza kuruhusiwa na kuwa kwenye uangalizi wa wazazi.
2.Watoto waliochini ya uzito au juu ya uzito uwa kwenye uangalizi kwa sababu, zifuatazo.
Mwenye uzito mkubwa anaweza kuwa amezoea vyakula vya kutosha kutoka kwa Mama yake akiwa tumboni akizaliwa tu anapaswa kuhudumiwa mapema na kupewa glucose Ili kulinganisha na chakula alichokuwa anakipata akiwa tumboni kwa hiyo akicheleweshwa anaweza kushuka kwa sukari. Na pia mtoto akizaliwa na uzito mdogo anapaswa kuangaliwa kwa sababu ya kupata uzito unaotakiwa kwa kihakikisha kuwa Mama yake anapewa elimu ya kumtunza mtoto mpaka akafikia kuwa na uzito unaotakiwa.
3. Pia mtoto akizaliwa anapaswa kuwa na kitovu kilicho kwenye tumbo na kinatakiwa kukatwa kwa uangalizi unaofaa Ili kuweza kuzuia maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto, pia na Mama anapaswa kupewa elimu kuhusu namna ya kumtunza kitovu cha mtoto wafundishwe kuwa kitovu cha mtoto kinakauka baada ya siku kumi, pia akina Mama wanapaswa kukumbushwa kuwa waachane na tabia ya kuweka vitu visivyofaa kwenye kitovu kwa kufuata mila na desturi zao hali inayosababisha kuwepo kwa tetunus kwenye kitovu kikitunzwa visivyo.
4. Pia kitu kingine ambacho ni sifa ya mtoto ni kulia tu baada ya kuzaliwa hii ikiwa ni ishara ya uhai kwa mtoto,kwa hiyo mtoto asipolia wauguzi na wasaidizi wote wanapaswa kihakikisha mtoto analia kwa kutoa huduma ya kwanza kwa mtoto na walio wengi wanafanyiwa na wanapona na kuendelea kwenye hali ya kawaida
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano
Posti hii inahusu malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano, huduma hii ilianzishwa na WHO na UNICEF mwaka 1990 ili kuweza kuzuia Magonjwa na kuwapatia watoto lishe pamoja na hayo walikuwa na malengo yafuatayo.
Soma Zaidi...Zijue Athari za kuweka vitu ukeni.
Posti hii inahusu zaidi athari za kuweka vitu ukeni, tunajua kwa wakati huu kadri ya kukua kwa sayansi na teknolojia watu wanaendelea kugundua mbinu mbalimbali ili waweze kuwafurahisha wapenzi wao wakati wa kufanya tendo la ndoa.
Soma Zaidi...dalili za mimba baada ya tendo la ndoa na changa ndani ya wiki moja
Utajifunza dalili za mwanzoni za mimba changa kuanzia wiki moja baada ya tendo la ndoa
Soma Zaidi...Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa?
Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka siku ya kujifungua Kama mume wake pamoja na yeye akiwa Hana maambukizi ya zinaa na Kama akiona dalili zozote zile za hatari ndio hataruhusiwa kushiriki tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Madhara ya fangasi ukeni
Maambukizi ya fangasi katika sehemu za Siri za mwanamke husababishwa na fangasi wanaoitwa CANDIDA ALBICANS pia maambukizi haya hujulikana kama YEAST INFECTION. Pia hupatikana katika midomo, mpira wa kupitisha chakula,kibofu Cha mkojo ,uume na uke.
Soma Zaidi...Mm tumbo linaniuma mara kwa mara na linakua kama linages alaf kichwa kinauma mara kwa mara na nakosa choo wakati mwingine na kiuno kinauma je?inawezakua n ujauzito? Maana nilshirki tendo la ndoa siku ya tano baada ya kutoka hedhi
Dalili za mwanzo za ujauzito zinaweza kuwa ni changamoto kwamwanamke hasa ikiwa ndio mimba yake ya kwanza. Maumivu ya tumbo, kujaa kwa tumbo gesi, kukosa choo ama hamu ya kula na kadhalika huweza pia kuambatana na ujauzito.
Soma Zaidi...