Zijue kazi za madini ya chuma mwilini
Posti hii inahusu zaidi kazi za madini ya chuma mwilini,Ni madini ambayo ufanya kazi mbalimbali mwilini na pia utokana na vyakula mbalimbali ambavyo upatikana kwenye wanyama na mimea. Zifuatazo ni kazi za madini ya chuma.
1. Madini ya chuma usaidia kusafilisha gasi ya oxygeni kutoka sehemu mbalimbali za mwili na kwenda sehemu nyingine za mwili ambapo oxgeni inahitajika.
2. Madini ya chuma usaidia katika kazi za haemoglobini ambayo ubeba gasi ya oxygeni kutoka kwenye mapafu kwenda sehemu mbalimbali za mwili na pia haemoglobini hiyo ubeba carbon dioxide kutoka kutoka kwenye sehemu mbalimbali za mwili mpaka kwenye mapafu kwa ajili ya kutafuta oxgeni kwa hiyo kazi ya kusafilisha hizi gasi mbili usaidia na madini ya chuma.
3. Madini ya chuma usaidia kusafilisha damu ya oxgeni kwenye misuli ambapo kitendo hiki kwa kitaalamu huitwa myoglobin ambayo ni sehemu ya protein kwenye misuli,kwa hiyo myoglobini asili yake ni protini ambayo inaweza kusafilisha gasi ya oksijeni kwenye misuli, hii kazi usaidiwa na madini ya chuma.
4. Madini ya chuma yanasaidia katika upumuaji kwa sababu ya kuwepo kwa cytochrome ambayo ni sehemu ya madini ya chuma, cytochrome usaidia katika kusafirisha hewa wakati wa kupumua, kwa sababu cytochrome imetengenezwa na madini ya chuma, ndo maana tunaaweza kusema kuwa madini ya chuma usaidia katika upumuaji.
5. Madini ya chuma usaidia katika kuzalisha protini hii ni kwa sababu ya kuwepo kwa baadhi ya vitu ambavyo vimetengenezwa kwa madini ya chuma ambayo usaidia kutengeneza protein kwa kitaalamu huitwa xanthine oxidase - enzyme ambayo ni sehemu ya madini ya chuma.
6.Madini ya chuma ni sehemu ya enzyme, tunajua kuwa enzyme ufanya kazi mbalimbali kwenye mwili, kwa hiyo madini ya chuma ni sehemu ya enzyme ambazo kwa kitaalamu huitwa peroxide, catalase na enzyme nyingine nyingi ambazo ufanya kazi mbalimbali kwenye mwili wa binadamu.
7.Madini ya chuma usaidia katika kuzalisha homoni ambazo utumika kufanya kazi mbalimbali kwenye mwili kama vile kuhakikisha kiwango Cha sukari kipo sawa kwenye mwili, kutengeneza protini kwenye mwili, kukua na kuzaliana na kazi zote mwilini ambazo utengenezwa na homoni.
Wapi tunaaweza kupata madini ya chuma?
1. Madini ya chuma tunaaweza kuyapata katika sehemu mbalimbali kama vile nyama, samaki, vyakula kama vile njegere, maharage,soya beans, njugu Mawe na vyakula vyote ambavyo ni jamii ya kuunde hivi vyote tunaviita kwa kitaalamu heme - iron .Kuna vyakula vingine ambavyo tunaviita non- heme iron kama vile vyakula vinavyopatikans kwenye mboga za majani, mayai na maziwa.
Nini madhara ya kukosa madini ya chuma mwilini.
1. Madini ya chuma yakikosa mwilini mtu anaweza kupata upungufu wa damu mwilini ambapo kwa kitaalamu huitwa Anaemia, ambayo upelekea mwili kuchoka, kizunguzungu, kichwa kuuma na mwili una kiss kinga mwilini kwa hiyo unaweza kupata magonjwa nyemelezi .
2. Madini ya chuma yakikosa mwilini mtu anaweza kupata ugonjwa wa kuvimba matezi ambao kwa kitaamu huitwa goitre yaani ni kuvimba kwenye shingo ambapo ugonjwa huu usababisha madhara makubwa kwa watu wengi, kwa hiyo tunapaswa kula vyakula vyenye wingi wa madini ya chuma usaidia sana katika shughuli mbalimbali kwenye mwili wa binadamu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 web hosting 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
HOMA YA DENGUE, DALILI ZAKE, TIBA YAKE, CHANGO YAKE NA INA SABABISHWA (AMBUKIZWA) NA MBU GANI
Homa ya dengue hupatikana sana Afrika, Asia na baadhi ya maeneo ya Caribbean.
Soma Zaidi...Vyakula hatari kwa afya ya moyo
Hivi ni vyakula hatari kwa watu wenye maradhi ya moyo. Vyakula hivi si salama kwa afya ya moyo
Soma Zaidi...Faida za kula Tangawizi
tangawizi ni katika viungio vya mboga vyenye faida, pia ni kinywaji, zijuwe leo faida za tangawizi
Soma Zaidi...Hizi ndio kazi za madini mwilini mwako
Post huu inakwenda kukupa orodha ya madini muhimu kwa ajili ya afya yako.
Soma Zaidi...VYAKULA HATARI KWA VIDONDA VYA TUMBO
Hivi ni vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo. mwenye vidonda vya tumbo hatakiwi kula vyakula hivi
Soma Zaidi...Faida za kiafya za kula kungumanga/nutmeg
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kungumanga/nutmeg
Soma Zaidi...