dalili za ugonjwa wa tezi dume, na sababu za kutokea kwa tezi dume, maana ya tezi dume na athari zake
TEZI DUME SIO BUSHA, ZIJUWE DALILI ZA TEZI DUME
Watu wengi wamekuwa wakidhania kuwa tezi dume ni busha ama ngiri maji kwa jina jinngine. Hapana hii sio sahihi kabisa. Mpenzi msomaji tambuwa kuwa tezi dume sio busha na haifananni kabisa na busha. Tezi dume isipotibiwa kwa haraka inaweza kuwa hatari sana kwani ina maumivu makali sana. Sasa nini hasa hii tezi dume?. katika makala hii nitakwenda kukupa mwangaza kuhusu tezi dume., dalili za tezi dume na athari za tezi dume kwa afya ako.
Nini maana ya tezi dume
Tezi hii kitaalamu hufahamika kama prostate gland. Hii ni tezi inayopatikana katika mfumo wa uzazi wa kiume. Tezi hii inapatikana jirani na kibofu cha mkojo na mirija ya mkojo. Tezi hii ina kazi ya kuzalisha majimaji ambayo hubeba mbegu za kiume. Majimaji haya ndio yale anayotoa mwanaume anapofikia kilele. Hivyo tezi hii ni muhimu sana katika mfumo wa kizazi wa mwanaume. Tezi hii si kubwa saana inapata sentimita zisizozidi 5. lakini tezi hii hukuwa kadiri umri unavyoenda.
Kwa ufupi wa maneno ni kuwa tezi dume ipo zini ya kibofu karibu na shingo ya kibofu. Na imezunguka mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu kuja nje (urethra). hivyo mkojo unapotoka kwenye kipofu hipitia katikati kwenye tezi dume ukiwa kwenye mrija wa urethra. Urethra ndio mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu.
Vipi ugonjwa wa tezi dume hutokea?
Kama ulivyojifunza hapo juu mkojo ukiwa kwenye mrija hupita katikati ya tezi tume. Sasa tezi hii ina kawaida ya kukuwa kadiri mtu anavyopata umri zaidi. Hivyo basi kadiri tezi hii inapoongezeka ukubwa ndivyo inavyoanza kuminya mirija ya kupitisha mkojo na hatimaye huanza tatizo la ugonjwa wa tezi dume. Tatizo hili kitaalamu hufahamika kama Benign Prostatic Hyperplasia (BPH).
Nini sababu za kutokea kwa tezi duma?
Kama ilivyokwisha kutajwa hapo juu, tezi hii hukuwa kadiri mtu anavyokuwa. Kwa baadhi ya watu inapokuwa huwa kubwa kiasi cha kuanza kuminya mirija ya mkojo na kuleta shida kwenye mfumo wa mkojo. Tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa miongoni mwa mambo yanayohatarisha uwezekano wa kupata ugonjwa huu ni haya yafuatayo:-
1.Umri, kikawaida tezi dume huwapata watu wenye umri kuanzia miaka 40. ni mara chache sana kuwapata walio chini ya umri huo. Pia tezi dume kwa kiasi kikubwa huwapata walio kati ya miaka sitini na kuendelea. Hususan robo tatu ni wale walio na miaka kuanzia 60,na nusu yao ni wale walio na miaka kuanzia 80.
2.Tatizo la tezi dume pia huweza kurithiwa. Yaani kama baba yako ana tezi dume ama yeyote katika damu yako hapo mwanzo alikuwa na tezi dume, hivyo upo uwezekana na wewe kurithi tatizo hili.
3.Pia inaonakana kuwa baadhi ya rangi huathiriwa sana na tatizo la tezi dume. Tafiti zinaonesha kuwa watu walio katika bara la Asia si sana kupatwa na tezi dume kuliko watu weusi na wazungu. Hata hivyo kwa watu weusi upo uwezekano wa kupatwa na tatizo hili katika umri mdogo kuliko wengine.
4.Maradhi, tafiti zinaonyesha kuwa kuna baadhi ya maradhi huweza kupelekea kupatwa na tatizo la tezi dume. Kwa mfano watu wenye maradhi ya sukari, na maradhi ya moyo wapo hatarini kupatwa na tezi dume ukilinganisha na watu wengine.
5.Staili za maisha. Tafiti pia zinaonyesha kuwa watu wenye kiribatumbo na wasiofanya mazoei wapo hatarini kupatwa na tatizo la tezi dume.
Ni zipi dalili za ugonjwa wa tezi dume?
Dalili za tezi dume zinaweza kuwa kali ama hafifu kutoka mtu hadi mtu. Ukali wa dalili hizi hautegemei ukubwa wa tezi. Inaweza kuwa tezi ni kubwa lakini dalili zisiwe kali. Miongoni mwa dalili za tezi dume ni:-
1.Kukojoa mara kwa mara, ama kuhisi kukojoa mara kwa mara
2.Kukojoa mara kwa mara wakati wa usiku
3.Kupatwa na uzgumu kutoa mkojo
4.Mchirizi wa mkojo kuwa dhaifu
5.Mkojo kukatakata unapofika karibu a mwisho
6.Kujichafua wakati wa kukojoa
7.Kushindwa kumaliza mkojo kabisa.
8.Damu kwenye mkojo
9.Kushindwa kukojoa kabisa.
10.Kupata mkojo mchache sana
Kuwa na dalili tajwa hapo juu pekee hakuwezi kukupa uhakika kuwa una tatizo la tezi dume. Kwani dalili tajwa hapo juu zinaweza kuambatananna shida nyingine za kiafya kwa mfano:-
1.Maambukizi ya UTI
2.Kuvimba kwa tezi
3.Kupunguwa ukubwa wa mrija wa mkojo
4.Kuwepo na vijiwe kwenye kibofu
5.Kuwa na shida kwenye mfumo wa neva ambazo hudhibiti ufanyaji kazi wa kibofu
6.Kuwa na saratani
7.Kama upasuaji katika kibofu haukufanyika sawa.
Ni zipi athari za tezi dume kama haitawahi kutibiwa?
Tezi dume ni kama maradhi mengine, inatibika bila wasi. Hata hivyo endapo matibabu yatachelewa athari zifuatazo zinaweza kupatikana:-
1.Kushindwa kabisa kukojoa
2.Kupatwa na maambukizi ya UTI
3.Kupatwa na vijiwe kwenye kibofu
4.Uharibifu wa kibofu unaweza kutokea
5.Figo inaweza kuharibika
Mwisho
Mwisho napenda kumaliza kwa kusema kuwa tatizo la tezi dume linatibika bila wasi. Zipo dawa za hospitali mgonjwa anaweza kupewa. Kamatatizo lake ni kubwa zaidi anaweza kufanyiwa upasuaji. Usisite kutembeleabongoclass.com kwa makala nyingine za aya
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Kama na wewe unasumbuliwa na hali ya kupitiliza siku zako post hii itakusaidia.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi tatizo la kutanuka kwa tezi dume, ni tatizo ambalo linawakumba wanaume wengi kwa wakati huu kwa sababu ya kuwepo kwa maaambukizi kwenye tezi ambayo Usababishwa na vitu mbalimbali kama tulivyoona.
Soma Zaidi...Mdomo kuwa mchungu ni halia mabayo haiashirii ishara mbaya za kiafya. Mdomo unaweza kuwa mchungu kutokana na vyakula. Pia hutokea ikawa ni ishara ya baadhi ya maradhi, ama ni matokeo ya baadhi ya shda za kiafya. Je vipi kuhusu maumivu ya matiti na tumb?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kuongezeka uzito kwa wajawazito, Mara nyingi Mama akibeba mimba uongezeka uzito kutoka wiki ya Kwanza mpaka wiki ya mwisho ya kujifungua.
Soma Zaidi...Tofauti na mambo matano yaliyotajwa hapo juu kuwa yanapelekea ujauzito kutoka, kuna mambo mengine ambayo yanaweza kuuweka ujauzito kuwa hatarini.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi tabia mbalimbali za Ute wa ovulation kwa sababu Ute huu huwa tofauti na Ute mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa tabia zake za kipekee kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Je na wewe ni moja kati ya wake ambao wanahitajivkujuwa siku za kupata mimba. Ama siku za competes mwanamke mimba. Post hii ni kwa ajili yako.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea kwa sababu ya kuziba kwa mishipa ya uzazi, ni baadhi ya dalili ambazo ujitokeza kwa sababu ya kuwepo kwa tatizo la kuziba kwa mishipa ya uzazi.
Soma Zaidi...Utajifunza sababu za maumivu ya uume na uke wakati wa tendo la ndoa na baada ya tendo la ndoa na matibabu yake.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa mama mjamzito, kwa sababu kuna baadhi ya Dalili zikitokea kwa mama mjamzito ni vizuri kabisa kuwahi hospitali mara moja.
Soma Zaidi...