Dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama mtoto wa kike

Dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama mtoto wa kike

Posti hii inakwenda kukueleza jinsi ya kuwjuwa kama mtoto ni wa kike ama wa kiume.

Kila mwanamke mwenye mina ana hamu ya mujuwa jinsia ya mtoto wake. Huwenda ili aweze kujiandaa kununua mavazi mapema, ama kupata pongezi kutoka kwa mwenzi wake ambaye amemuahidi kuzipata endapo atakuwa na mtoto wa jinsia fulani. Dalili za mimba iwe ya mtoto wa kike ama wa kiume ni zilezile isipokuwa kuna mambo flani yanaongezeka.  Katika post hii nitakueleza dalili ambazo watu wengi wanaamini kuwa zinaonyesha jinsia ya mtoto. Hata hivyo pia nitakueleza usahihi wa maoni yao kitaalamu.

 

Dalili za kawaida za ujauzito wa mtoto bila kujali jinsia:

  1. Kutoka na matone ya damu iliyo nyepesi
  2. Kukosa hedhi
  3. Maumivu ya kichwa bila ya sababu
  4. Mwili kuongezeka joto
  5. Mapigo ya moyo kuongezeka
  6. Kupata kizungzungu
  7. Kupatwa na kichefuchefu
  8. Kuchoka bila ya kufanya kazi
  9. Maumivu ya tumbo

 

Sasa wacha tuje kwenye swali letu la awali kuhusu dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama wa kike. katika kuelezea kkila dalili nitakwenda kukuambia uhakika wa dalili hizo. Jambo la kuzingatia ni kuwa dalili pekee hazithibitishi bila ya kupata vipimo kwa kitaalamu. kwani misingi ya dalili hizo imewekwa kutokana na imani za watu vile wanavyodhani ama mazoea yao ama historia ya yale yaliowakuta.

 

Dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama wa kike:

  1. Uzito wa tumbo; Inaaminika kuwa endapo mjamzito atahisi tumbo ni zito sana basi mtoto ni wa kiume. lakini endapo tumbo siuo zito sana basi mtoto ni wa kike. Wanaamini kuwa mtoto wa kiume ni mzito kuliko wa kike. Hata hivyo nadharia hii haina uithibitisho wa kitaalamu ijapokuwa watu wanaamini hivyo.

 

  1. Kichefuchefu: Wanadai wamama kuwa endapo mjamzito atakuwa na kichefuchefu sana basi mtot ni wa kiume. na endapo hatapata kabisa ama itakuwa ni cha kawaida basi mtoto ni wa kike.

 

  1. Mabadiliko kwenye ngozi: Dhana hii ni kuwa endapo mwanamke atapata mabadiliko kwenye ngozi yake, mabadiliko ambayo yatakwenda kuharibu muonekano wa ngozi na uzuri wake basi mimba hiyo ni ya mtoto wa kike. Pia wnaamini kuwa mtoto wa kike anachukuwa urembo wa mama yake. Miongoni mwa mabbadiliko hayo ni chunusi, ngozi kupauka na kukosa mvuto. Kwa uoande mwiungine mtoto wa kiume hawezi kumfanya majamzito abadilikwe na ngazi yake. pia nadharia hii haina ushahidi wa kitaalamu kutoka kwa madaktari.

 

  1. Mabadiliko ya nywele waumini wa dhana hii wanasema kuwa mtoto wa kiume hana shida na uzuri wa mama yake. Kwa kuwa nywele ni moja ya uzuri wa mama basi zitabaki kama zilivyo. kwanamke hatakuwa na mabadiliko ya nywele akiwa na mimba ya mtoto wa kiume. Kwa upande mwingine mimba ya mtoto wa kike itamfanya nywele kunyonyoka ama kukatika. Imani hii pia haina ushahidi wa kisayansi.

 

  1. Kuchaguwa sukari na chumvi: Inaaminika kuwa mwanamke mwenye mimba ya mtoto wa kike anapenda sana vitu vitamu. lakini ikiwa mimba ni ya mtoto wa kiume anapendelea sana vitu vyenye chumvi chumvi. hata hivyo hakuna ushahidi wa kitaalamu kuthibitisha nadharia hii.

 

  1. Utofauti wa kwenye mapigo ya moyo: Wanaamini kuwa endapo mimba ni ya mtoto wa kike mapigo ya moyo huwa mengi zaidi. kwa mfano yakiwa ni zaidi ya 140 ndani ya dakika basi mimba ni ya mtoto wa kike. na yakiwa chini ya 140 mtoto ni wa kiume. nadharia hii inaonekana ni ya kitaalamu zaidi, hata hivyo haina ushahidi wa kuthibitisha.

 

Je nitajuwaje kwa uhakika kuwa mtoto ni wa kiume ama wa kike?

Sasa wacha tuangaie kitaalamu zaidi kwa namna gani utaweza kujuwa jinsia ya mtoto. Ukweli ni kwamba utaweza kuwa na uhakika wa jinsia ya mtoto kwa kutumia vipimo. Hivyo hapa nitakueleza baadhi ya vipimo ambavyo vinatumika kujuwa jinsia ya mtoto.

  1. Kwa kutumia kipimo cha damu cha DNA kwa mfano kipimo cha panorama kinachojulikana kama Noninvasive prenatal testing (NIPT). Kipimo hiki kinaweza kuonyesha jinsia ya mtoto kuanzia wiki ya 7 hadi ya 10 toka ujauzito kutungwa.

 

  1. Kwa kutumia kipimo cha utrasound: Kipimo cha utrasound hutumika kumulika ndani ya tumbo la mjaozito na kumuona mtoto na jinsia yake. kipimo hilki kinaweza kuona jinsia ya mtoto kuanzia ujauzito wa wiki ya 18 hadi 20.

 

Mwisho nimalizie kusema kuwa bila ya kutumia vipimo vya kitaalamu hatuwezi kuwa na uhakika juu y jinsia ya mtoto. Hivyo kwa mwenye kutaka kujuwa jinsia ya mtoto afanye vipimo vya kitaalamu. kwa mfano kipimo cha utrasound sio cha ghali kukifanya ukilinganisha vipimo vinginevyo.

Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 54584

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Njia za kuzuia ugumba
Njia za kuzuia ugumba

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia ugumba, ni njia ambazo utumiwa na wapenzi ambao wameshindwa kupata watoto hasa kwa wale ambao wamezaliwa wakiwa na uwezo wa kupata watoto lakini kwa sababu tofauti tofauti wanashindwa kupata watoto kwa hiyo njia zifu

Soma Zaidi...
Je mjamzito Uchungu  ukikata inakuwaje
Je mjamzito Uchungu ukikata inakuwaje

Hutokea uchungu wa kujifunguwa ukakati. Unadhani ni kitugani kinatokea.

Soma Zaidi...
Siku za kupata mimba
Siku za kupata mimba

Nitakujulisha siku ya kupata mimba na sifa zake, na namna ya kuweza kuitafuta

Soma Zaidi...
Kaka nasumbuliwa saan na tatizo la kuwasha kwenye kichwa Cha uume Sijui nifanyaje
Kaka nasumbuliwa saan na tatizo la kuwasha kwenye kichwa Cha uume Sijui nifanyaje

Je kichwa cha uume wako kinawasha, na je kinatoa majimaji kwenye njia ya mkojo, una muda ganinavtatizo hili. Na je ulishiriki ngono zembe siku za hivi karibuni?

Soma Zaidi...
 Magonjwa madogo madogo kwa Mama wajawazito.
Magonjwa madogo madogo kwa Mama wajawazito.

Posti hii inahusu zaidi magonjwa madogo madogo kwa akina Mama wajawazito, ni magonjwa ambayo hayawezi kupelekea kupoteza maisha kwa Mama mjamzito, magonjwa haya upotea ikiwa Mama atajifungua.

Soma Zaidi...
Kazi ya homoni ya testosterone
Kazi ya homoni ya testosterone

Posti hii inahusu zaidi kazi ya homoni ya testosterone, hii homoni kwa kiwango kikubwa ukutwa kwa wanaume ndiyo homoni ambayo umfanya mwanaume aonekane jinsi alivyokuwa na sifa zake zote.

Soma Zaidi...
Huduma kwa mama ambaye mimba imetoka moja kwa moja.
Huduma kwa mama ambaye mimba imetoka moja kwa moja.

Post hii inahusu zaidi huduma kwa mama ambaye mimba imetoka moja kwa moja, aina hiyo ya mimba kwa kitaalamu huitwa complete abortion.

Soma Zaidi...
Mambo yanayopelekea ugumba.
Mambo yanayopelekea ugumba.

Post huu inahusu zaidi mambo yanayopelekea ugumba kwa wanaume, ni mambo ambayo uchangia au upelekea mwanaume kukosa uzazi.

Soma Zaidi...
Mda wa kufanya tendo la ndoa baada ya kujifungua
Mda wa kufanya tendo la ndoa baada ya kujifungua

Posti hii inahusu zaidi mda ambao mama anapaswa kukaa bila kufanya tendo la ndoa mara tu baada ya kujifungua.

Soma Zaidi...