picha

Kumuandaa maiti kabla ya kufa na baada ya kufa, mambo muhimu anayopasa kufanyiwa maiti wa kiislamu

3.

Kumuandaa maiti kabla ya kufa na baada ya kufa, mambo muhimu anayopasa kufanyiwa maiti wa kiislamu

3.0 MAMBO YA FARADH KWA MAITI YA MUISLAMU.

3.0 MAMBO YA FARADH KWA MAITI YA MUISLAMU.
3.1 Kuna aina Kuu mbili za Faradh.
Fardh A’in.
Ni faradh inayomlazimu kila mtu binafsi kuitekeleza, haina uwakilishi.
Mfano; kusimamisha swala, kufunga saumu, kuhiji, kutoa zaka, n.k.



Faradh Kifaya.
Ni faradh ya kuwakilishana, wachache wakitekeleza hutosheleza hitajio.
Mfano; kuswalia maiti, n.k. lakini akikosekana wa kuwakilisha, waislamu wote wanaohusika watawajibika.

3.2 Mambo ya lazima kufanyiwa maiti wa Kiislamu.
- Kila nafsi itaonja mauti (kifo). Qur’an (3:185) na (4:78).
Mambo manne yafuatayo ni lazima kufanyiwa maiti ya kiislamu:
1.Kuoshwa (Kukoshwa).
2.Kuvikwa sanda (kukafiniwa).
3.Kuswaliwa.
4.Kuzikwa.



Mambo muhimu anayofanyiwa Muislamu (mtu) anayekaribia kufa.
Mtu akikaribia kufa huwa hajiwezi kwa lolote lile pamoja na elimu, ujuzi alionao, hivyo huhitajia kufanyiwa mambo yafuatayo;
i.Kuogeshwa, kugishwa mswaki na kumpaka mafuta au manukato kama kuna uwezekano.
ii.Kumlaza kwa ubavu wa kulia au chali na kumuelekeza Qibla iwapo kuna uwezekano.
iii.Kumpa maji ya kunywa.
iv.Kutamka (kumsomea) – Shahada “Laa ilaha illallaah”
Abu Said na Abu Hurarirah wamesimulia kuwa, Mtume wa Allah amesema: “Wasomeeni watu wenu wanaokaribia kufa; ‘Laailahaillallaah”



Pia Mu’az bin Jabal amesema kuwa Mtume (s.a.w) amesema: “Yule ambaye maneno yake ya mwisho yatakuwa; “Laailahaillallaah” ataingia peponi.
(Abu Daud)
- Si lazima anayekufa aitamke kwa sauti, inaweza ikawa kimoyo moyo.



Mambo anayofanyiwa mtu (maiti) mara tu baada ya kufa.
Baada ya mtu kufa inatuwajibikia tuseme: “Innalillah wainnailaihraaji’una”. Qur’an (2:156). Kisha kumfanyia maiti mambo yafuatayo:

i.Kwa taratibu kurudishia mdomo wake usiwe wazi kwa kufunga kwa kitambaa kutoka kidevuni na kuzungushia kichwani.



ii.Kufunga macho ya marehemu na huku ukisema;
“Kwa jina la Allah na kwa kufuata mila ya Mjumbe wa Allah, Ewe Mola wetu mrahisishie mambo yake ya sasa na msahilishie mambo yake ya baadaye. Na jaalia anayokutanayo yawe bora kuliko aliyoyaacha.”



iii.Lainisha viungo vyake (miguu na mikono) kwa kukunja na kukunjua taratibu.
- Kama kuna ugumu maji ya uvuguvugu au mafuta yanaweza kutumika kulaisha na kunyoosha viungo hivyo.
- Baada ya kulainisha viungo, miguu na mikono inyooshwe na kulazwa uso ukielekezwa Qibla kwenye mkeka au kitanda kisicho na godoro.



iv.Maiti avuliwe nguo zote alizokufa nazo na kisha kufunikwa kwa shuka kubwa
- Ni vyema afunwe kitambaa tumboni au kuwekewa kitu kizito ili tumbo lisifutuke.



v.Marashi na ubani vitumike kwa wingi ili kuzima harufu ya uvundo wa maiti.


Baada ya kufanyiwa hatua hizo, sasa ni lazima maiti kufanyiwa yafuatayo:
Mambo haya ni faradh Kifaya, wakifanya wachache wanawakilisha wengine.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2984

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 web hosting    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Maandalizi kwa ajili ya kifo

Mwanadamu anatakiwa aishi huku akikumbuka kuwa ipo siki atakufa. Hivyo basi inatupata lujiandaa mapema kwa ajili ya kifo.

Soma Zaidi...
Aina za twahara na aina za najisi

Katika post hii utakwenda kuzijuwa aina za twahara katika uislamu. Utaviona vigawanyo vya twahara kulingana na maulamaa wa Fiqh

Soma Zaidi...
Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya

Mirathi katika jamii za kijahiliKatika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Kwanini lengo la funga halifikiwi na wafungaji wengi

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
JIFUNZE FIQH

Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.

Soma Zaidi...
Nadharia ya uchumi wa kiislamu

Dhana ya uchumi wa kiislamu imejegwa jui ya ukati na kati. Dhana hii imetofautiana sana na dhana nyinginezo kama ubepari na ujamaa.

Soma Zaidi...
Je manii ni twahara au najisi?

Post hii itakwenda kukufundisha hukumu ya manii kuwa ni twahara ama ni najis

Soma Zaidi...
Hadhi na haki za mwanamke katika jamii za Kigiriki hapo zamani

(a) UgirikiTunajifunza katika historia ya Ulimwengu kuwa jamii ya Wagiriki ilikuwa miongoni mwa jamii zilizoanza kustarabika.

Soma Zaidi...