Post hii inahusu zaidi huduma kwa mama ambaye mimba inataka kutoka, mimba za aina hiyo kwa kitaalamu huitwa inevitable pregnant ni lazima itoke tu hata kama kuna juhudi mbalimbali za wataalamu mimba hii utoka kabisa.
Huduma kwa mama mwenye mimba inayotaka kutoka.
1. Kwanza kabisa napenda kuwakumbushia kwamba aina ya mimba hii huwa na dalili zote za mimba kutoka ambazo ni pamoja na kutokwa kwa damu nyingi ambayo uandamana na maumivu makali ya tumbo hasa tumbo la chini.kama mama ataangaliwa na wataalamu wa afya mimba uonekane kwenye mlango wa kizazi na mara nyingi kichanga kinakuwa kimeshakufa tayari kwa hiyo mama ufanyiwa uangalizi wa karibu ili kuhakikisha kwamba mimba inatoka kwa utaratibu bila kuasili maisha ya mama.
2. Kama mimba iko chini ya miezi mitatu au wiki kumi na mbili kusafishwa kunapaswa kufanyika kwa kutumia njia ya kitaalam ambayo inaitwa manual vacuum evacuation, kwa hiyo ni vizuri kabisa akina Mama kuelewa siku zao za mimba ili kuweza kupata huduma inayofaa endapo matatizo kama haya yakitokea.
3 . Kama mimba ipo zaidi ya miezi minne au zaidi ya wiki kumi na mbili mama anapaswa kupewa dawa za kuanzisha uchungu ili kuweza kujifungua kawaida dawa hizo huitwa oxtocini na siku zote upitishwa kwenye mirija ya damu, mama anapaswa kupewa taarifa zote hatua kwa hatua na pia aambiwe lengo la kupewa dawa za kuanzisha uchungu.
4. Pia mama anapaswa kutiwa moyo na kumhakikishia usalama na kumwambia kwamba ni hali ambayo utokea akina Mama wengi na pia urudia hali ya kawaida.
5. Pia jamii na watu wa karibu wa mama wanapaswa kumtia moyo mama na kuachana na mila na desturi za kwamba mimba kutoka ni aibu kwa ukoo kwa hiyo wasimtenge mama bali na wenyewe wapewe elimu kuhusu namna ya kumsaidia na kumtunza mama pale atakaporudi kwa hali ya kawaida.
6. Pia mama anapaswa kuambiwa wazi wazi siku za kubeba mimba nyingine na afahamu kwamba baada ya mimba kutoka ndani ya siku ishirini na moja anaweza kubeba mimba nyingine kwa hiyo anapaswa kutumia uzazi wa mpango ili kuepuka kubeba mimba nyingine kabla ya viungo havijawa na nguvu kuweza kutunza mimba, kwa hiyo mama akitoa mimba anapaswa kubeba mimba nyingine baada ya miezi sita.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali za kutokwa na damu baada ya hedhi hili ni tatizo ambalo uwapata wanawake wengi pamoja na akina Mama kwa sababu ya kutokwa na damu yenye utelezi baada ya hedhi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kutunza joto la mtoto mara tu anapozaliwa,tunajuwa wazi kuwa Mama anaweza kujifungulia sehemu yoyote ile kabla hajafika hospitalini kwa hiyo mtoto anapaswa kuwa na joto la mwili la kutosha i
Soma Zaidi...Hizi ni siku hatari kwa mwanamke ambazo ni ahisi kwake kubeba mimba, siku nitakueleza ni zipi na ni zipi sifa zake
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuangalia kama mtoto anapumua pindi anapozaliwa,tunajua kabisa ili kujua na kuelewa kama mtoto yuko hai ni lazima kuangalia upumuaji wa mtoto,ambapo tunaitambua pale anapolia tu.
Soma Zaidi...Mimba hatari iliyotungia nje ya mji wa mimba, ni zipi dalili zake na ni kivipo mimba inatungia nje?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi maelekezo muhimu kwa mama au mlezi wa mtoto mgonjwa. Ni maelekezo muhimu hasa wakati wa kutoa dawa kwa mtoto.
Soma Zaidi...