Post hii inahusu huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote sikioni. Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu ambapo hutumika kusikia, Kuna wakati vitu uingia ndani yake na kuleta madhara
Dalili za mtu aliyeingiza kitu chochote sikioni inawezekana kuwa maharage, mahindi, wadudu na vitu vingine kama hivyo ambavyo hupendelewa na watoto.
Dalili za mtu aliyeingiza kitu sikioni
1. Maumivu makali
2. Maambukizi kwenye sikio
3. Kuvimba ndani ya sikio
4. Sikio kuwa jekundu
5. Kushindwa kusikia vizuri
6. Kutoka uchafu sikioni
Vifuatavyo ni vitu vinavyoweza kuingia sikioni
1. Maharage
2. Mahindi
3. Wadudu
4. Mchanga
5. Toyi
6. Makaratasi madogo madogo
Tufanyeje Ili kuepusha Hali ya kuingia maharage, mahindi na vitu vingine kwenye sikio?
1. Watoto wanapaswa kuwa na mwangalizi wakati wa kucheza
2. Watoto wadichezee vitu kama maharage na mahindi
3. Watoto na watu wazima wawe na tahadhari hasa sehemu zile zenye wadudu kama vile nyuki na wadudu wengine wanaoweza kuingia masikio.
Huduma ya kwanza
1. Usitumie vitu kama msumari, ama kijitu kuchokoa sikio ili kutoa kitu kilichoingia, kufanya hivi kunaweza kuingiza zaidi hicho kitu
2. Kama kitu kinaonekana kitoe kwa upole kwa kukishika, kama kwa kutumia vipanio maalumu vidogovidogo kama tweezers
3. inamisha sikio kwa hali ambayo tundu iliyoingiwa na kitu itaelekea chini
4. kama aliyeingia ni mdudu tumia mafuta yaliyo na uvuguvugu, yaingize sikioni kisha inamisha kichwa kama ulivyofanya hapo juu. Usitumie njia hii kwa kitua ambacho kio mdudu.
5. tumia maji, ingiza sikioni ili hicho kitu kitoke pamoja na maji. Unaweza kutumia bomba la sindano kufanya hivi.
6. mpeleke mmgonjwa kituo cha afya kama kitu kitashindikana kutoka.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!
Umeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inaelezea kuhusiana na upungufu wa maji mwilini
Soma Zaidi...Jiamini A ni katika vitamini inayojulikana sana kuboresha na kuimarisha afya vya macho na uoni. Tafiti zinaonyesha kuwa kuna kundi kubwa la watoto wanaopata tayizobla kutokuona kutokana na ukosefu wa vitamini A vya kutosha.
Soma Zaidi...Natak kufaham kuwa binadam akiwa mweupe mikononi atakuwa na upungufu wa vitamin gani?
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa fizi ambapo fizi huweza kuwa na maumivu, kuambukizwa, kuvuja damu kwenye fizi na Vidonda.
Soma Zaidi...Maziwa ni mojakati ya vinywaji ambavyo ni dawa na hutumikakutoa huduma ya kwanza pale mtu anapomeza ama kula sumu. Huduma ya kwanza hii inaweza kuokoa maisha na wakati mwingine inaweza kuwa ndio dawa kabisa wala hakuna haja ya kufika Kituo cha afya.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida ya chanjo, tunajua wazi kuwa chanjo Ina faida kubwa kwenye mwili wa binadamu na vile vile kwenye jamii kama tutakavyoona hapo chini.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vitamin
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo maradhi huambukizwa
Soma Zaidi...