Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuangalia kama mtoto anapumua pindi anapozaliwa,tunajua kabisa ili kujua na kuelewa kama mtoto yuko hai ni lazima kuangalia upumuaji wa mtoto,ambapo tunaitambua pale anapolia tu.
1. Kwanza kabisa wakati tunapokuwa tunapangusa mtoto tunapaswa kuangalia upumuaji wake kwa kuangalia Dalili zote za upumuaji.
2.Vile vile Tunapaswa kusikiliza sauti inayotoka wakati wa kupumua na kuangalia jinsi kifua kinavyocheza cheza kwa kutumia sauti tunaweza kugundua kuwa mtoto yuko hai na anaweza.
3.Vili vile tunapaswa kuangalia kama mtoto anapumua haraka haraka na kwa urahisi au kuangalia kama mtoto analia kwa sababu kulia ni Dalili mojawapo ya kupumua kwa mtoto.
4. Na pia mtoto anapaswa kuonekana anapitisha hewa kwenye pua kwa urahisi sio kwa shida, ukiona anapitisha hewa kwa shida hiyo ni Dalili kwamba kuna Tatizo ambalo halijaenda sawa na pia ni lazima kumshughulikia mtoto.
5. Kwa kawaida mtoto anayepumua vizuri ni yule ambaye analia tu baada ya kuzaliwa, anapumua vizuri na kwa haraka haraka na upumuaji wake ni wa kawaida hakoromi au hakuna kitu chochote kinacholeta shida wakati wa upumuaji.
6. Na mtoto ambaye hapumui vizuri ni yule ambaye anahangaika wakati wa kupumua na anapumua kwa kutumia hewa nzito na pumzi haieleweki au kwa wakati mwingine hakuna kupumua kabisa, hali ya namna hii ikitokea huduma inapaswa kutolewa haraka.
7. Kwa wakati mwingine kuna watoto ambao wanazaliwa na hewa yao inakuwa ya shida na kwa wakati mwingine wanazaliwa wakiwa hawapumui kabisa kwa hiyo tunapaswa kuwasaidia kwa kufungua sahemu muhimu kama vile kwenye mdomo, kwenye pua au kifuani labda kuna baadhi ya vitu ambavyo vimefunga hewa isiweze kupita.
8. Pamoja na upumuaji wa shida kwa watoto kuna baadhi ya watoto wanaozaliwa wakiwa na uzito mkubwa na wanahitaji uangalizi wa karibu ili waweze kupata huduma kwa sababu walicheleweshwa wanaweza kupata matatizo mbalimbali.
9. Kwa hiyo baada ya kugundua kubwa mtoto anapumua vizuri na hana tatizo lolote ni lazima kumpeleka kifuani mwa Mama ili aendelee kuishi hapo kwa ajili ya kupata joto la Mama na kwa wale ambao hawapumui ni vizuri kabisa kuwahi kuwapeleka kwenye vituo vya afya kwa ajili ya uangalizi zaidi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
dalili za mimba zinaweza kuwa na mkanganyiko kwani zinafanana na shida nyingine za kiafya. Hali hii utaigunduwa endapo utakuwa na dalili za mimba lakini kila ukipima hakuna mimba.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu kushiriki tendo la ndoa wakati wa ujauzito faida na hasara zake
Soma Zaidi...PEP Ni dawa ambazo utumiwa na watu wanaojamiiana na watu wenye virus vya ukimwi ila wenyewe hawawezi kupata kwa sababu ya kutumia dawa hizo.
Soma Zaidi...Utajifunza dalili za minyoo, sababu za minyoo na namna ya kujiepusha na minyoo. Dalili kuu 5 za minyoo mwilini
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia Faida, hasara, na madhara ya Kufunga kizazi kwa Wanaume.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi sababu za mimba kutoka, hili ni tatizo ambalo linawakumba wanawake wengi ambapo mimba utoka kabla ya kumfikisha mda wake, kwa kawaida Ili kawaida mimba nyingi utoka zikiwa na miezi chini ya Saba au wengine wanaweza kusema kwamba mim
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID, tunaita tiba ya awali kwa sababu baada ya kupima na kugunduliwa kwamba una tatizo au changamoto ya PID ni vizuri kutumia tiba hiii baadae ndipo utumie dawa.
Soma Zaidi...Je na wewe unasumbuliwa na fangasi wenye uume. Post hii ni kwa ajili yako.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu namna unavyoweza kumtambua mtoto mwenye Ugonjwa wa Nimonia na tiba anayopaswa kupata mtoto mwenye Nimonia
Soma Zaidi...