picha

Kujiepusha na kuua nafsi bila ya Haki

Kuua nafsi bila ya Haki, ni kuiua nafsi isiyo na kosa linalostahiki hukumu ya kifo.

Kujiepusha na kuua nafsi bila ya Haki

(d) Kujiepusha na kuua nafsi bila ya Haki.



Kuua nafsi bila ya Haki, ni kuiua nafsi isiyo na kosa linalostahiki hukumu ya kifo. Hata kama mtu amefanya kosa la kustahiki kuuliwa, hatauliwa kwa mtu binafsi kuchukua sharia mkononi bali itabidi afikishwe mbele ya Kadhi na ahukumiwe kwa mujibu wa sheria ya Kiislamu.



Si nafsi ya binaadamu tu iliyoharamishwa kuuliwa pasina haki bali hata nafsi za viumbe vingine vyote ikiwa ni pamoja na wanyama wakubwa na wadogo na mimea. Kwa mfano tunaruhusiwa kuwaua wanyama kwa ajili ya manufaa kutoka kwao au kwa ajili ya kujikinga na madhara yao dhidi ya binaadamu. Pia haturuhuswi kukata au kuteketeza mimea ovyo ovyo pasina haja maalumu na kwa kuzingatia utunzaji wa mazingira.


“ Wala msiwaue watoto umasikini…”(1 7:31)


Kiutendaji kuwaua watoto kwa kuogopa umasikini si lazima kuishia kwenye kuwaua watoto waliokwisha zaliwa bali hata kuzuia mimba isitokee, kutoa mimba au kufunga kizazi bila ya sababu ya msingi ya kiafya ni katika kuua watoto. Na katika aya hizi Allah (s.w) anatahadharisha:


"… Kwa yakini kuwaua ni khatia kubwa". (17:31)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views 1643

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 web hosting     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu

Ni zipo njia wanazotumia Allah katika kuwasiliana na kuwafundisha wanadamu? (EDK form 1: Dhana ya elimu katika Uislamu).

Soma Zaidi...
KUAMINI MALAIKA

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kula mali ya Yatima

Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6).

Soma Zaidi...
Maamrisho ya kushikamana nayo

Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo: (i)Kumuabudu Allah (s.

Soma Zaidi...
Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab

Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu.

Soma Zaidi...