Sifa za wanafiki zilizotaja katika surat An-Nisaa (4:60-63, 88, 138-145)

Sifa za wanafiki zilizotaja katika surat An-Nisaa (4:60-63, 88, 138-145)

Huwaoni wale wanaodai kwamba wameamini yale yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako?

Sifa za wanafiki zilizotaja katika surat An-Nisaa (4:60-63, 88, 138-145)

(3) Sifa za wanafiki zilizotaja katika surat An-Nisaa (4:60-63, 88, 138-145)


Huwaoni wale wanaodai kwamba wameamini yale yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako? Nao wanataka wakahukumiwe kwa njia ya twaghuuti; na hali wameamrishwa kukataa njia hiyo. Na Shetani anataka kuwapoteza upotofu (upotevu) ulio mbali (na haki).(4:60)


Na wanapoambiwa "Njooni katika yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu, na (njooni) kwa Mtume," utawaona wanafiki wanajiweka mbali nawe kabisa. Basi itakuwaje utakapowafikia msiba kwa sababu ya yale iliyotanguliza mikono yao?Kisha wakakujia wakiapa "Wallahi! Hatukutaka ila wema na mapatano." Hao ndio wale ambao Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo nyoyoni mwao. Basi waachilie mbali, (lakini) uwape mawaidha na uwaambie maneno yenye taathira yatakayoingia katika nafsi (nyoyo) zao. (4:61-63)


Imekuwaje nyinyi kuwa makundi mawili katika khabari ya wanafiki, na hali Mwenyezi Mungu amewageuza kwa sababu ya yale (mabaya) waliyoyachuma? Je! Mnataka kumwona mwongofu ambaye Mwenyezi Mungu amemhukumu kuwa kapotea? Na aliyemhukumu Mwenyezi Mungu kuwa amekwisha potea hutampatia njia (ya kuambiwa mwongofu). (4:88)


Waambie wanafiki kwamba watapata adhabu inayoumiza. (Wanafiki) ambao huwafanya makafiri kuwa marafiki badala ya Waislamu. Je! Wanataka wapate utukufu kwao? Basi utukufu wote ni wa Mwenyezi Mungu. (Hauko katika mkono wa mtu). Naye amekwisha kuteremshieni katika Kitabu (hiki) ya kwamba mnaposikia Aya za Mwenyezi Mungu zinakataliwa na kufanyiwa stihzai, basi msikae pamoja nao, hata waingie katika mazungumzo mengine. (Mtakapokaa) mtakuwa kama wao. Hakika Mwenyezi Mungu atawakusanya wanafiki na makafiri wote pamoja katika Jahannam. (4:138-140)



(Wanafiki) ambao wanakungojeni (mpate msiba): basi mkipata kushinda kunakotoka kwa Mwenyezi Mungu, husema (kukwambieni): "Je! Hatukuwa pamoja nanyi?" (Na kama makafiri wamepata sehemu (ya kushinda) husema: (kuwaambia makafiri), "Je, hatukukurubia kukushindeni (tulipokuwa katika jeshi la Waislamu), tukakuzuilieni na (kudhuriwa na hao). Waislamu?" Basi Mwenyezi Mungu atahukumu baina yenu siku ya Kiyama. Na Mwenyezi Mungu hatawajaalia makafiri njia ya kuwashinda Waislamu (kabisa kabisa mpaka waiondoshe dini yao. Hawatajaaliwa kupata hayo). Wanafiki hutaka kumdanganya (hata) Mwenyezi Mungu. Naye atawaadhibu kwa sababu ya kudanganya kwao (huko). Na wanaposimama kusali husimama kwa uvivu, wanaonyesha watu (kuwa wanasali) wala hawamtaji Mwenyezi Mungu ila kidogo. (4:141-42)



Wanayumbayumba baina ya huku (kwa Waislamu na huko kwa makafiri). Huku hawako wala huko hawako. Na ambaye Mwenyezi Mungu amemhukumu kupotea, huwezi kumpatia njia (ya kuhisabika kuwa mwongofu). Enyi mlioamini! Msiwafanye makafiri kuwa marafiki badala ya Waislamu. Mnataka awe nayo (Mtume wa) Mwenyezi Mungu hoja dhahiri juu yenu (ya kuwa nyinyi wabaya)? Bila shaka wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa katika moto. Hutamkuta kwa ajili yao msaidizi (yo yote). (4:143-145)



Katika aya hizi sifa za wanafiki zinaainishwa kama ifuatavyo:
(i)Wanapendelea kuhukumiwa kwa sheria za Kitwaghuut kuliko kuhukumiwa kwa sheria za Allah (s.w)
(ii)Hawako tayari kuishi kwa kufuata Qur-an na Sunnah.
(iii)Hutumia sana viapo katika kuficha uovu wao dhidi ya Uislamu na Waislamu.
(iv)Huwafanya makafiri kuwa marafiki badala ya Waislamu.
(v)Hujikomba kwa makafiri kwa kutaraji kupata vyeo au kuonekana wa maana kwao.
(vi)Wanashirikiana na makafiri katika kuzifanyia stihizai aya za Allah (s.w) na Uislamu kwa ujumla.
(vii)Waislamu wakishinda, hujikomba kuwa pamoja nao na hujinakshi (hujigamba) kuwa wao ndiwo waliosababisha kupatikana kwa ushindi.
(viii)Makafiri wakishinda hujikomba kwao na kujinakshi kuwa ndio waliowawezesha kushinda.
(ix)Hawana msimamo. Kwa Waislamu hawapo na kwa makafiri hawapo. Hivyo hawaaminiki kote kote.
(x)Wanaposimama kuswali, husimama kwa uvivu.
(xi)Hufanya amali kwa riya (kwa kuonyesha watu). (xii Hawamtaji Mwenyezi Mungu ila kidogo tu.




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 120


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Maana ya kuamini malaika katika maisha ya kila siku
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

mtazamo wa uislamu juu ya dini
Soma Zaidi...

Adabu ya kuingia katika nyumba za watu
Enyi mlioamini! Soma Zaidi...

Mgawanyiko wa elimu usiokubalika katika uislamu
Ni mgawanyo upi wa elimu haukubaliki. Ni ipi elimul akhera na elimu dunia? (Edk form 1 Dhana ya elimu) Soma Zaidi...

Mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na maumbile yake
Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu. Soma Zaidi...

Kujiepusha na ubadhirifu (israfu) na ubakhili
Soma Zaidi...

zijue Nguzo za uislamu, imani, ihsani pamoja na dalili za qiyama
' ' ' ' ' ' ': " ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ?... Soma Zaidi...

Elimu ya mwingozo na elimu ya mazingira katika uislamu
Mahusiano kati ya elimu ya mwongizo na elimu ya mazingira katika uislamu. Soma Zaidi...

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab
Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu. Soma Zaidi...

DUA YA 1 - 10
1. Soma Zaidi...

Jifunze ni kwa namna gani Malaika waliweza kuwasiliana ana manabii Malimbali
Wakatibmeingibe Allah anapotaka kuwasiliana na wanadamu hutuma Malaika wake. Soma Zaidi...

Nafsi ya mwanaadamu
Soma Zaidi...