Zijuwe sababu kuu zinazokufanya ukahisi maumivu makali ya tumbo kwa chini upande wa kushoto
MAUMIVU YA TUMBO KWA CHINI UPANDE WA KUSHOTO
Sehemu ya kushoto ya tumbo lako kwa chini hupatikana mwishilizo wa utumbo mkubwa. Pia kwa upande wa wanawake sehemu hii hupatikana ovari ya kushoto. Katika hali za kawaida maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto sio jambo la kuogopesha sana. Kwani maumivu haya yanaweza kuondoka yenyewe bila ya kuhitaji uangalizi wa kidaktari.
Je na wewe ni mmoja kati ya wanaosumbuliwa na maumivu ya tumbo kwa shini upande wa kushoto? Je una muda gani na tatizo hili?. makala hii ni kwa ajili yako. Hapa nitakwenda kukujuza sababu za maumivu ya tumbo sehemu ya chini upand wa kushoto.
Kama nilivyotangulia kukuijuza kuwa maumivu haya si jambo la kuogopesha. Basi ni vyema kwa haraka ukamuona daktari endapo utaona dalili zifuatazo:-
A.Homa
B.Sehemu husika kuwa na ugumu na maumivu
C.Kuvimba kwa tumbo
D.Kuona damu kwenye kinyesi
E.Kuendelea kuwa na kichefuchefu na kutapika kwa masik kadhaa
F.Kupungua uzito
G.Ngozi kuwa na njano.
Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto
1.Kuwa na shida kwenye utumbo mkubwa.
Hii hutikea pale kwenye utumbo mkubwa kunapoota kama vijifuko vijidogo. Hivi sio jambo la kuogopa sana kiafya maana mara nyingi havina madhara na hupotea vyenyewe. Hali hii huwapata sana wenye umri zaidi ya miaka 40. sasa ikitokea vijifuko hivi vimeshambuliwa na vijidudu huvimba na kuleta maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto. Dalili zake ni kama:-
A.Homa
B.Kichefuchefu
C.Kutapika
D.Tumbo kujaa na kuiwa gumu
E.Kuharisha
F.Kukosa choo
2.Gesi tumboni.
Sababu nyingine ni kujaa gesi tumboni. Gesi tumboni inaweza kusababishwa na:-
A.Kumeza hewa sana
B.Kula kupitiliza
C.Kuvuta sigara
D.Kutafuna bigjii
E.Chakula kutokumeng’enywa vyema
F.Kula vyakula vyenye gesi
G.Kuwa na bakteria kwenye utumbo mkubwa.
3.Kuvimbiwa ama chakula kutokumeng’enywa vyema tumboni. Hali hii huplekea maumivu ya tumbo kwa juu. Maumivu haya wakati mwingine husambaa na kuathiri chini ya tumbo upande wa kushoto. Mtu pia ataona dalili kama:-
A.Kiungulia
B.Kuhisi kishiba na tumbo kujaa
C.Kucheua gesi
D.kichefuchefu
4.Ngiri henia; henia ina dalili kama:-
A.Kuongezeka uvimbe maeneo ya tumboni (si kila henia)
B.Maumivu kuongezeka
C.Maumivu wakati unaponyanyua kitu
D.Kujihisi umeshiba
5. kuwa na vijiwe kwenye figo
Vijiwe vya kwenye vigo vinatokana na mkusanyiko wa madini ya chumvi. Vijiwe hivi vinaweza kutokea kwenye figo, kibofu ama maeneo mengine kwenye mfumo wa mkojo. Vijijiwe hvi vinaweza kusababisha maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto. Pia vinaweza kusababisha maumivu ya mgongo upande mmoja na nyuma pia na kwenye mbavu. Tofauti na dalili hizi pia mgonjwa anaweza kupata dalili zifuatazo:-
A.Mkojo wenye rangi ya kahawiya, nyekundu ama mawingu mawingu na haruu kali
B.Mkojo wenye maumivu makali unaotokea mra kwa mara
C.Kichefuchefu
D.Vomiting
E.Homa
Maumivu ya tumbo kwa chini uapande wa kulia kwa wanawake, husababishwa na yafuatayo:-
A.Tumbo la chango
B.Kuota tishu za tumbo la uzazi maeneo mengine
C.Kuwa na shida kwenye ovari
D.Kuwa na ujauzito uliotungia nje
E.Kuwa na ugonjwa wa PID
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inazungumzia kuhusiana na mifuko midogo midogo, iliyobubujika ambayo inaweza kuunda kwenye utando wa mfumo wako wa usagaji chakula. Wao hupatikana mara nyingi katika sehemu ya chini ya utumbo mkubwa (koloni). Hali hiyo inajulikana kama Divert
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa pre- eclampsia ni Ugonjwa ambao uwapata wanawake wajawazito uwapata pale mimba inapofikisha umri wa wiki ishilini, utokea pale ambapo Mama mjamzito huwa na kiwango kikubwa cha shinikizo la damu na pia kuwepo kwa protini
Soma Zaidi...Zijuwe sababu za kuumwa nankichwa upande mmoja wa kichwa.
Soma Zaidi...KUJIANDAA KWA AJILI YA KUMUONA DAKTARI Fanya miadi na daktari wako wa kawaida ikiwa una ishara au dalili zinazokupa wasiwasi.
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo upande wa kushoti, kwa mwanamke huwenda ikawa ni ujauzito ama shida nyingine za kiafya kama tumbo kujaa gesi, kukosa choo na kadhalika. Sasa vipi kwa wanaume ni ipi hasa sababuâ”
Soma Zaidi...Watu wengi wamekuwa wakijiuliza kuwa ukimwi huonekana baada ya muda gani toka kuathirika?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi visababishi vya maambukizi kwenye milija na, ni mambo yanayosababisha maambukizi kwenye milija na ovari.
Soma Zaidi...Malaria ni moja ya magonjwa hatari yanayoongoza katika vifo vya watoto wengi duniani walio chni ya umri wa miaka 5. Katika post hii utakwend akujifunza kuhusuugonjwa huu jinsi unavyotokea, hatuwa zake na dalili zake.
Soma Zaidi...