JITIBU KWA KITUNGUU THAUMU: faida za kiafya za kitunguu thaumu
Kitunguu thaumu ni katika viungo vya mboga na chakula.
FAIDA ZA KITUNGUU THAUMU
Kitunguu thaumu ni katika viungo vya mboga na chakula. Karibia maeneo yote duniani wanatumia kitungiuu thaumu. Kitunguu thaumu huweza kutumika kikiwa kibichi. Wataalamu wa afya wanaeleza faida nyingi za kiafya. Wataalmu wa afya wametengeneza kidonge kwa kutumia vitunguu thaumu ili kuwezesha upatikanaji wa virutubisho vya mmea huu.
Kitunguu thaumu kina chembechembe nyingi ambazo ndizo husaidia katika tiba. Miongoni mwa chembechembe hizo ni chembechembe za salfa ziitwazo allicin. Allicin hupatikana kwenye kitunguu kibichi pindi kinapopondwa ama kutafunwa. Chembechembe nyingine ni kama diallyl disalfide na s-allyl cysteine.
Zifuatazo ni faida za kiafya za kitunguu thaumu
- Kunapatikana virutubisho vingi ndani ya kitunguu thaumu kama vitamini B6, B1 na vitamini C. madini ya calcium, copper, phosphoros, potassiumna selium.
- Hushusha presha ya damu (hypertsnsion). kitunguu thaumu sio kizuri kwa wenye presha ya kushuka, kwani itashuka sana.
- Hudhibiti cholesterol (kolesto) hivyo husaidia katika kuzuia hatari ya kupata maradhi ya moyo.
- Kitunguu thaumu kina antioxidant ambazo husaidia kupunguza hatari ya kupata maradhi ya kusahausahau
- Huimarisha mfumo wa kinga mwilini.
- Huondoa sumu za vyakula mwilini.
- Huimarisha afya ya mifupa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 web hosting 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 ai web app 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Faida za kiafya za kula mihogo
Some Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula mihogo
Soma Zaidi...Faida za kula Matunda
Sifanjema Ni za Mwenyezi Mungu aliyetupa Afya njema hata kuifanya kazi hii mpaka kufiia hapa.
Soma Zaidi...FAIDA ZA MATUNDA NA MBOGA MBALIMBALI KWA AFYA
FAIDA ZA MATUNDA Makala hii inakwenda kukuletea faida za matunda mbalimbali na mboga upatikanaji wake na faida zake kiafya.
Soma Zaidi...